You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
29<br />
D.<br />
Mwanzo ya zambi inaanza kwa ajili ya fundisho mbaya ya watoto wetu. Hawa watoto,<br />
wenye awakupate ma shauria na mafundisho nzuri, wakati watakomea wanaingia ndani ya<br />
kiwanja ya zambi na matendo mbaya. Wazazi wekona jukumu mnene kwa sababu awakusopoke<br />
nzuri watoto wao. Na mweye wa mama na wa baba musikieni hii mambo! . . .<br />
E.<br />
Inasukumu mu zambi tena na zwezo mbaya.<br />
Hii mambo tunaiona na sisi kila siku. Wenye watu wanakunywa vinyo na ingine kila siku<br />
wanapenda kulewa; wenye wanaiba hawaweze kusimama hii kazi mbaya yao ya kuiba, wenye<br />
zambi ya mwili wanapenda kufanya hii zambi kila siku na hivi wote wenye zambi wanapenda<br />
kufata zwezo mbaya yao kama iko na namna na kila siku. Nikusema zwezo inawakokota kama<br />
kamba na inawatupa mu zambi. Sawa vile huyu mwenye njaa anaomba mukate na mwenye<br />
kunywa anaomba maji vile na wale watu wanapenda kutelemuka mu zambi yao.<br />
Ninawaza hii ni maneno ya tano kwa ajili yao kila mtu anapenda kukosa mbele ya Mungu na<br />
zambi yake. Lakini weye, ndugu wangu, unayependa kuokolewa na kuonyesha imani yako mu<br />
uzima yako, sindana kila siku bila usimamisho kupingana ya kila zambi. Hii yote maneno, sababu<br />
na nyakati ya zambi ni wa adui wasiyo mapendo ya wokovu yako: Mwili kama nyama makari<br />
anataka kwa matakio na zambi mbaya kusimama juu ya roho yako. Shetani adui yako, ambaye<br />
anachukia wokovu yako hasisimame kuuzi na kukombana mu uzima yako kila siku na usiku.<br />
Majaribu ya dunia wanavimba na wanakomea matakio mbaya ya mwili yako kila siku, sawa vile<br />
pepo inavimba moto. Lakini mambo ya sikitiko ni hii: Kwa yule mtu alizombelea kazi moja<br />
kimbaya, yeye hasiweze kusimamisha hii matakio yake, kiwa sababu ndani yake inazala sawa<br />
moja nguvu ya mbili kwa mwili yake.<br />
Sindano kupingana ya zambi<br />
Ninaichika ya kama sindano kupingana ya zambi ni nguvu sana; lakini ni lazima kabisa.<br />
Watu mengi wanakombana na wanashinda ma taifa wengine; lakini hawa ni watumwa na<br />
watumishi kwa matakio na zambi yao. Hakuna ushindi kuliko utukufu toka hii ushindi ya maungo<br />
yetu. Taji na utukufu bila ushindi hakuna. Ushindi vila sindano kupingana ya adui hakuna.<br />
Ndugu wangu, twende kuanza hii sindano juu ya kupata na saidio ya Kristu ushindi ya<br />
utukufu na tutakamata toka Huyu Mungu taji ya fazila na tutatukuzwa kwa milele ndani ya<br />
Ufalme wake. Sasa twende kuandika mawazo filani juu ya kupata nguvu kwa hii sindano yetu:<br />
A.<br />
Unasikia na kombana kusikia na akili yako neno ya Mungu. Ndani ya hii fundisho ya<br />
Mungu tunafamia sisi zambi na fazila; paka vile tutaepuka zambi na tutafata fazila ya Mungu:<br />
«Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya<br />
watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; ili mutu wa Mungu<br />
awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo jema». (Barua ya mbili ya Timoteo 3, 16-<br />
17). Neno ya Mungu ni kisu ya Roho (Wa Efeso 6, 17), na kwa hii kisu tunakata adui yetu, adui ya<br />
nafsi yetu.<br />
B.<br />
Mungu eko ma fasi yote. Pahali fasi sisi tuko Yeye ni karibu yetu. Kila kazi sisi tunafanya,<br />
tunaifanya mbele ya ma Macho Takatifu yake. Basi, namna gani tutafanya zambi na tutakanyanga<br />
mapenzi Yake takatifu mbele ya ma Macho yake?<br />
Unasikia haya na unaogopa kusimama na kibego mbele ya mfalme wa inchi ao mbele ya<br />
musaidizi yake. Lakini haya na heshima ngapi mingi inapaswa kuonyesha kama unasimama<br />
mbele ya Mungu? Usisahabu ya kama kila zambi ni kibego na uzulumu mbele Yake.<br />
29