Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
47<br />
3.<br />
Kwa sababu muchungaji anasubuka juu ya faida ya waminifu wote, katikati yao uko na<br />
weye, inapaswa kumupenda kama baba na musaidizi yako na kumuonyesha shukrani yako.<br />
Unamuita baba. Unafanya nzuri. Kwa sababu yeye anakuzala katika roho, sawa vile wa Kristiani<br />
wote, lakini hapna kwa maisha hii, lakini mu uzima ya milele. Basi, umupenda na weye kama<br />
baba yako. Umupenda baba yako aliyekuzala. Lakini kupita mingi inapaswa kupenda baba yako ya<br />
roho.<br />
4.<br />
Huyu anasubuka na anasaidia watu wote na weye. na weye usimusahabu ma lazima yake.<br />
Umusaidia, umutimiza kila kintu yeye eko na lazima juu ya kutumika nzuri tendo yake. Hivi hii<br />
mapendo katikati yenu na wema haitambakie bila maendeleo na faida ya roho.<br />
5.<br />
Mu dunia ni watu mengi wazaifu, wenye awatake kusikia mashauria na malipizo ya<br />
wachungaji wao na wanaishi katika mapenzi yao. Hawa wanatafuta na wanazambalala ma fasi<br />
yote matusi na masimango kupingana ya wachungaji wao. Basi, wakati utasikia moja sauti yao<br />
kibaya kupingana ya muchungaji yako, usisadiki. Funga kinywa yako na usiseme kintu kimoja<br />
kwa watu wengine. Kama utasema, utafanya zambi uzito, kwwani utaleta kwazo kwa wa ndugu<br />
wengine. Kama ni matata kuhukumu mtu moja ya bure, ngapi ni kibaya kabisa kama utahukumu<br />
na utasimanga muchungaji wako! Hii masimango wanazala funjo mnene katikati ya watu.<br />
Wanazala uzarau na kukataa utii mbele ya wachungaji wao na hivi machoko ya mkubwa yao<br />
inaenda kwa bure na bila matunda ya roho.<br />
Sopoka hii sauti nilikuwambia sasa. Macho yako kamata ya kufungula kila siku na daima.<br />
Chunga nafsi yako toka ma sauti mbaya inayezambalisha kupingana ya muchungaji yako. Lakini,<br />
kabisa sopoka weye, na usisema na usihukumu baba ya roho yako, kwa sababu utasirika Mungu<br />
na Yeye atakulipiza.<br />
6.<br />
Kama utaona makosa filani, mu uzima na kwa watu wenye heshima, usiajabu na usiache<br />
kuingia kwazo ndani ya roho yako, lakini uwaza ya kama muchungaji ni na huyu mtu sawa sisi<br />
wote.<br />
7.<br />
Kwa sababu muchungaji ya Kanisa niko mbele ya mateso mengi na tena kupingana yake<br />
wanasimama kama wa adui shetani na watumishi mbaya yake, kwa hivi na yeye eko na lazima ya<br />
saidio ya Mungu na nguvu ya Neema Yake. Sawa vile watu wote ya dunia, vile na weye ukona<br />
kazi kupaswa kuomba ya kusaidia baba yako ya ho.<br />
Furaha na heri ya nyumba inatoka ya mkubwa ya nyumba, ushindi ya wa askari inatoka ya<br />
jemadari mzuri na safari nzuri ya chombo moja inatoka ya mukubwa mwogozi yake. Basi, omba<br />
kwa Mungu juu muchungaji ya kanisa yako kuwa mwenye akili na mzuri na hivi ushirika wa<br />
Kristu itaendelea mbio ku mbele.<br />
8.<br />
Kama kwa mufano muchungaji hasimaliza hii ma sauti na shauria anasema na anafanya<br />
kupindua, ile saa kumbuka ma neno ya Kristu, ambaye alisema kwa hawa wachungaji:<br />
«Waandishi na Wafarisayo wanaketi katika kiti cha Musa; basi maneno yote wanayowaambia<br />
ninyi kutenda, muyashike na kuyatenda; lakini musitende kwa mufano wa matendo yao; kwa<br />
maana wanasema, lakini hawatendi» (Matayo 23, 2-3).<br />
47