TPSEAL 2010 Financial Results. - Serena Hotels
TPSEAL 2010 Financial Results. - Serena Hotels
TPSEAL 2010 Financial Results. - Serena Hotels
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Notisi Kuhusu Mkutano Wa Pamoja Wa Mwaka<br />
Notisi inatolewa hapa kwamba mkutano wa 39 wa pamoja wa mwaka<br />
wa Kampuni utafanyika Mei 31, 2011 katika Ukumbi wa Mikutano<br />
ya kimataifa wa Kenyatta International Confrence Centre kuanzia saa<br />
tano asubuhi ili kuangazia maswala yafuatayo ya kibiashara:<br />
SHUGHULI ZA KAWAIDA<br />
1. Kuthibitisha kumbukumbu za mkutano wa thalathini na nane wa<br />
pamoja wa mwaka uliofanyika Mei 24, <strong>2010</strong>.<br />
2. Kupokea, kuangazia na endapo itaonekana kuwa sawa, kupitisha<br />
hesabu ya pesa kwa kipindi cha mwaka uliomalizika Desemba 31<br />
<strong>2010</strong> pamoja na ripoti kutoka kwa Wakurugenzi na Wakaguzi wa<br />
pesa.<br />
3. Kuidhinisha kutolewa kwa malipo ya mwisho ya mgawo wa faida<br />
wa mwaka <strong>2010</strong> wa shilingi 1.25 kwa kila hisa ikitegema ushuru<br />
ulioshikiliwa pale inapohitajika kwa wanachama ambao majina yao<br />
yatakuwa kwenye sajili kufikia Mei 31, 2011. Malipo ya mgawo wa<br />
faida yatatolewa kabla au kufikia Juni 20, 2011.<br />
4. Kuchagua Wakurugenzi<br />
(a) Bw. Ghislain de Valon aliteuliwa mwaka 2011 kujaza nafasi<br />
iliyokuwa wazi. Anastaafu kwa mujibu wa kifungu nambari 109<br />
cha sheria za kampuni na kwa kuwa hali inamruhusu, amejitokeza<br />
tena kuchaguliwa.<br />
(b) Bw. Kabir Hyderally anastaafu kwa zamu kwa mujibu wa vifungu<br />
nambari 110, 111 na 112 vya sheria za Kampuni na kwa kuwa hali<br />
inamruhusu, amejitokeza tena kuchaguliwa.<br />
(c) Bw. Mahmood Manji anastaafu kwa zamu kwa mujibu wa<br />
vifungu nambari 111 na 112 vya sheria za Kampuni na kwa hali<br />
inamruhusu , amejitokeza tena kuchaguliwa.<br />
(d) Bw. Kungu Gatabaki anastaafu kwa zamu kwa mujibu wa vifungu<br />
nambari 110, 111 na 112 vya sheria za Kampuni na kwa kuwa hali<br />
inamruhusu, amejitokeza tena kuchaguliwa.<br />
5. Kuidhinisha malipo ya wakurugenzi ya mwaka <strong>2010</strong>.<br />
6. Kuteua PricewaterhouseCoopers kama wakaguzi wa pesa wa<br />
kampuni kwa mujibu wa sehemu ya 159 (2) ya sheria za<br />
makampuni (Cap 486). PricewaterhouseCoopers wameonyesha<br />
nia yao ya kuendelea na jukumu hili.<br />
7. Kuidhinisha malipo ya wakaguzi wa pesa kwa kipindi cha mwaka<br />
<strong>2010</strong> na kuwapa ruhusa wakurugenzi kuamua malipo ya wakaguzi<br />
hao.<br />
8. Kutekeleza shughuli nyingine ya kawaida ya kibiashara ya<br />
mkutano mkuu wa pamoja wa mwaka.<br />
SHUGHULI MAALUMU<br />
9. Kurekebisha vifungu vya sheria<br />
Kuzingatia na endapo itakubalika, kupitisha maazimio yafuatayo<br />
ambayo yatapendekezwa kama maazimio ya kawaida:<br />
(i) Kwamba vifungu vya sheria vya kampuni vibatilishwe na kuingiza<br />
kifungu kifuatacho kama kifungu nambari 68.<br />
‘’ Notisi yoyote au hati nyingine inaweza kutolewa na kampuni kwa<br />
mwanachama au mkurugenzi yeyote wa kampuni aidha kwa mtu<br />
binafsi au kutumia sanduku la barua ( kupitia barua pale ambapo<br />
huduma hii inapatikana) au kupitia telegramu, teleksi, kipepesi au<br />
barua pepe iliyotumwa kwa mwanachama au mkurugenzi kama<br />
huyo kupitia anwani iliyosajiliwa kama inavyodhihirishwa kupitia<br />
sajili ya wanachama au rekodi nyingine za kampuni iwe anwani<br />
kama hiyo ni ya humu nchini au nje ya nchi ya Kenya au kupitia<br />
teleksi, kipepesi, telegramu au barua pepe iliyotajwa au kwa kutumia<br />
tangazo la magazeti mawili ya kila siku yanayosambazwa<br />
kote nchini au kupitia tangazo kwa njia ya elektroniki. Katika hali<br />
ambapo umiliki wa hisa utakuwa wa pamoja, notisi zozote kupitia<br />
barua, telegramu, kipepesiau barua pepe, itatolewa kwa mmoja wa<br />
wamiliki hao ambaye jina lake litakuwa la kwanza kwenye sajili<br />
ya wanachama na notisi ikitolewa itachukuliwa kama inatosha<br />
kwa wamiliki wote wa pamoja. Katika hali ya notisi ya mkutano ya<br />
pamoja wa mwaka, notisi kama hii itatolewa kupitia:<br />
(a) Kuchapishwa kwa notisi iliyo na muhtasari wa taarifa za matumizi<br />
ya pesa na ripoti ya wakaguzi wa pesa kupitia magazeti mawili ya<br />
kila siku yanayosambazwa kote nchini kwa siku mbili mfululizo au;<br />
(b) Kutuma notisi moja kwa moja kwa kila mwanachama kupitia<br />
mbinu za elektroniki (ikiwemo kipepesi na barua pepe) au kupitia<br />
sanduku la posta huku notisi ikiwa na taarifa hizo za matumizi ya<br />
pesa , hati nyingine na ripoti kama inavyohitajika kisheria.’’<br />
(ii) Kifungu cha sheria nambari 156 kifutiliwe mbali kama kilivyo na<br />
mahali pake kuwa kama ifuatavyo:<br />
‘’ Mgawo wowote wa faida, riba au kiwango chochote cha pesa<br />
kitakachotolewa kwa pesa taslimu kwa mmiliki wa hisa kilipwe<br />
kupitia:<br />
(a) Hundi au dhamana itakayotumwa kupitia sanduku la barua kwa<br />
mmiliki kama huyu kwa anwani yake inayojulikana na katika hali<br />
ambapo umiliki ni wa pamoja, itumwe kwa mmiliki ambaye jina<br />
lake limesajiliwa mbele katika sajili ya wanachama kulingana na<br />
hisa au<br />
10 TPS EASTERN AFRICA LIMITED ANNUAL REPORT AND FINANCIAL STATEMENTS <strong>2010</strong>