09.11.2014 Views

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

TAARIFA YA MWENYEKITI<br />

<strong>In</strong>anifurahisha sana kuwasilisha kwenu Taarifa ya kila Mwaka<br />

ya Benki ya NIC na Taarifa ya kifedha ya Mwaka uliomalizikia<br />

tarehe 31 Disemba, <strong>2011</strong>.<br />

MAZINGIRA YA KIUCHUMI NA KIBIASHARA YA MWAKA WA<br />

<strong>2011</strong><br />

Mategemeo makubwa ya Uchumi wa taifa la Kenya yaliathirika<br />

pakubwa katika mwaka wa <strong>2011</strong> kutokana na changamoto<br />

kubwa la kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hata hivyo, licha ya<br />

changamoto hizo, uchumi ulitarajiwa kukua kwa asilimia 4.3<br />

chini ya kiwango cha asilimia 5.6 iliyopatikana mwaka wa 2010,<br />

hii ikiwa ni kulingana na mazingira ya kiuchumi yalivyokuwa.<br />

Baada ya kuanza mwaka kwa hatua nzuri kutokana na kasi<br />

na mwamko uliokuwepo mwaka wa 2010, uchumi wa Kenya<br />

uliathirika kutokana na ghasia ama vurugu huko katika<br />

Milki ya Nchi za Kiarabu na Afrika Kaskazini pamoja na jamii<br />

kutoelewana na hali ya kisiasa ambayo ilisababisha kupanda<br />

kwa bei ya mafuta. Na ni wakati huo huo ambapo tulikuwa<br />

tumekabiliwa na janga la ukame lililosababisha uhaba wa<br />

chakula na ongezeko la vyakula kuagizwa kutoka nchi za nje.<br />

Kutokana na upungufu wa chakula nchini na ongezeko la bei ya<br />

mafuta ambayo hayajasafishwa kwenye masoko ulimwenguni<br />

yalisababisha mfumuko wa bei ambao uliongezeka kutoka<br />

asilimia 5.4 kwenye mwezi Januari, <strong>2011</strong> hadi asilimia 19.7<br />

kwenye mwezi wa Novemba, 2010. Kiwango cha wastani cha<br />

mfumuko wa bei kwenye mwaka wa <strong>2011</strong> kilikuwa asilimia<br />

14.0 kikilinganishwa na asilimia 4.1 kwenye mwaka wa 2010.<br />

Ongezeko la matumizi ya kinyumbani na uwekezaji uliochangiwa<br />

na ukuaji katika sekta za kibinafsi za mkopo pia ulichangia kwa<br />

kiasi kikubwa katika mfumko wa bei.<br />

Kutokana na ongezeko la bei ya mafuta ambayo hayajasafishwa,<br />

matumizi ya hali ya juu ya kinyumbani, uwekezaji na ongezeko<br />

la mahitaji ya chakula kutoka nchi za nje na vilevile mafuta ya<br />

kuzalisha umeme yalisababisha kuanguka kwa thamani ya<br />

shilingi ya Kenya dhidi ya sarafu nyingine kuu za kimataifa.<br />

Isitoshe, kuanguka kwa thamani ya shilingi kulisababishwa pia<br />

na kuzorota kwa biashara ya nje ya nchi. Wakati huo ukame<br />

uliathiri vibaya sana uzalishaji wa chai, kahawa na bidhaa za<br />

kilimo cha bustani hali inayojumuisha kiwango kikubwa cha<br />

mazao tunayo safirisha nje ya nchi. Kwa upande mwingine,<br />

kuzorota kwa uchumi katika ukanda wa magharibi mwa Bara-<br />

Yuropa ambalo ndilo miongoni mwa masoko yetu makuu,<br />

yalipunguza mahitaji ya bidhaa zetu kutoka humu nchini. Kwa<br />

upande mwingine, athari za madeni na misukosuko katika<br />

baadhi ya mataifa ya Uarabuni, ilisababisha kudhoofika kwa<br />

Dola ya Marekani na rasilimali zilizotazamiwa na wawekezaji<br />

kuwa salama. Kutokana na mambo hayo yote kufikia Oktoba<br />

<strong>2011</strong>, kiwango cha kubadilisha shilingi dhidi ya Dola ya<br />

Marekani kilipungua hadi asilimia 25 kwa shilingi 107 kwa Dola<br />

ya Marekani na ilifikia wakati shilingi ya Kenya ilitambuliwa<br />

kuwa yenye thamani dhaifu zaidi ulimwenguni.<br />

Ili kusimamisha kuzorota kwa thamani ya shilingi ya Kenya na<br />

kuzuia mfumko wa bei, Benki Kuu ya Kenya (BKK) ilitekeleza<br />

msururu wa hatua za sera za kifedha ambazo zilihusisha<br />

kuongeza kwa haraka kwa Viwango vya Benki Kuu kutoka<br />

asilimia 5.75 hadi asilimia 18 ili kuthibiti tatizo la kubanwa kwa<br />

mzunguko wa fedha nchini na katika masoko ya uwekezaji.<br />

Tatizo hilo sugu la mzunguko wa fedha lilisababisha kupanda<br />

kwa ghafla kwa viwango vya riba. Viwango vya hazina ya fedha<br />

kwa siku 91, siku 182 na siku 364 viliongezeka kwa wastani wa<br />

kila mwezi wa asilimia 2.5, 2.7 na 3.7 katika mwezi wa Januari,<br />

<strong>2011</strong> hadi asilimia 18.3, 18.3 na 21.0 mwezi wa Disemba, <strong>2011</strong><br />

mtawalia. Mwezi wa Januari, <strong>2011</strong> viwango vya mikopo katika<br />

benki kwa benki vilisimamia katika kiwango cha wastani cha<br />

asilimia1.2 na zikaazimia kumaliza mwaka zikiwa na kiwango<br />

cha wastani cha asilimia 21.8.<br />

Kufikia mwisho wa mwaka, Benki Kuu ya Kenya ilikuwa<br />

imefaulu kurudisha hadhi ya shilingi yake na Dola ya Marekani<br />

kupitia kwenye hazina ya fedha ulimwenguni. Huduma ya<br />

Ziada ya Upatikanaji wa Mkopo pia iliboresha zaidi thamani ya<br />

shilingi ya Kenya katika robo ya nne ya mwaka. Kiwango cha<br />

ubadilishanaji wa fedha kufikia mwisho wa mwaka wa <strong>2011</strong><br />

kilifikia kiwango cha wastani wa shilingi 85.1 dhidi ya Dola ya<br />

Marekani.<br />

Wakati ambapo hatua thabiti zilipochukuliwa na Benki Kuu ya<br />

Kenya na kuleta mafanikio katika kuyatimiza malengo yake ya<br />

kuboresha thamani ya shilingi ya Kenya, wakati huu, ni lazima<br />

kuzingatia katika utawala wa viwango vya juu vya riba ambavyo<br />

haviwezi kumudu ukuaji wa uchumi wa mda mrefu na hasara<br />

iliyopo. Hali hii hususan itaathiri Sekta ya Benki ambapo baadhi<br />

ya wateja na wenye kukopa watashindwa kutimiza malengo yao<br />

na kuhudumia mikopo yao ipasavyo na kusababisha matukio<br />

mengi ya kuwa na mikopo mingi isiyolipwa.<br />

Swala la kimsingi zaidi, changamoto nyingi ambazo<br />

zimesababisha mtafaruku huu wa malipo bado<br />

haujashughulikiwa. Gharama ya juu ya kufanya biashara nchini<br />

Kenya imefanya uzalishaji wa bidhaa za humu kutokuwa na<br />

ushindani na kusababisha kuagizwa kwa bidhaa za wanunuzi<br />

na zile zilizotengenezwa nje ya nchi kuletwa kutoka huko<br />

ughaibuni. Kutokuwa na ufanisi katika sekta ya kilimo<br />

imemaanisha kuwa hata baada ya mwaka wa mafanikio ya<br />

kuwepo kwa mvua nyingi bado kuna uhaba wa chakula na<br />

kusababisha umuhimu wa kuagiza chakula kutoka nchi za nje.<br />

Nikiongezea ni kuwa Kenya kwa mda mrefu sasa imekuwa<br />

ikitegemea sana utalii na kuuza bidhaa za msingi za kitamaduni<br />

ambazo zina thamani ndogo, jambo ambalo linatufungia uwezo<br />

wetu wa kupata kiwango cha juu cha pesa za kigeni. Ikiwa sera<br />

na hatua thabiti hazitatekelezwa ili kuzithibiti changamoto hizo,<br />

basi nchi hii itazidi kuathirika kiuchumi kutokana na matatizo<br />

ya usawa wa malipo.<br />

Matokeo ya soko la hisa yalikandamiza mafanikio kuanzia<br />

mwanzo wa mwaka wa <strong>2011</strong> kutokana na “mabadiliko ya kanuni<br />

za uwekezaji kwa wajasirili-amali” yaliyoonekana kwenye<br />

masoko ya kifedha ulimwenguni ambayo yalisababishwa na<br />

tatizo la viwango vya mikopo huko barani Yuropa na kuwepo kwa<br />

wawekezaji wa kigeni katika masoko ya Afrika Kaskazini. Katika<br />

sehemu ya pili ya mwaka, matokeo haya yasiyofaa yalipaliliwa<br />

makaa na viwango vya juu vya riba ambavyo vilisababisha<br />

wawekezaji kuhamisha hazina zao kwenye bidhaa bora za<br />

uzalishaji. Ubora wa hisa ulianguka kila mahali na kusababisha<br />

kupungua kwa asilimia 30 katika kiwango cha hisa cha Soko la<br />

Ubadilishanaji wa Hisa la Nairobi (NSE-20) na kufikia kiwango<br />

cha mwisho cha alama 3,123 mwaka huo wa <strong>2011</strong> kutoka kwa<br />

NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong> • 13

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!