Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
TAARIFA YA MWENYEKITI<br />
<strong>In</strong>anifurahisha sana kuwasilisha kwenu Taarifa ya kila Mwaka<br />
ya Benki ya NIC na Taarifa ya kifedha ya Mwaka uliomalizikia<br />
tarehe 31 Disemba, <strong>2011</strong>.<br />
MAZINGIRA YA KIUCHUMI NA KIBIASHARA YA MWAKA WA<br />
<strong>2011</strong><br />
Mategemeo makubwa ya Uchumi wa taifa la Kenya yaliathirika<br />
pakubwa katika mwaka wa <strong>2011</strong> kutokana na changamoto<br />
kubwa la kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hata hivyo, licha ya<br />
changamoto hizo, uchumi ulitarajiwa kukua kwa asilimia 4.3<br />
chini ya kiwango cha asilimia 5.6 iliyopatikana mwaka wa 2010,<br />
hii ikiwa ni kulingana na mazingira ya kiuchumi yalivyokuwa.<br />
Baada ya kuanza mwaka kwa hatua nzuri kutokana na kasi<br />
na mwamko uliokuwepo mwaka wa 2010, uchumi wa Kenya<br />
uliathirika kutokana na ghasia ama vurugu huko katika<br />
Milki ya Nchi za Kiarabu na Afrika Kaskazini pamoja na jamii<br />
kutoelewana na hali ya kisiasa ambayo ilisababisha kupanda<br />
kwa bei ya mafuta. Na ni wakati huo huo ambapo tulikuwa<br />
tumekabiliwa na janga la ukame lililosababisha uhaba wa<br />
chakula na ongezeko la vyakula kuagizwa kutoka nchi za nje.<br />
Kutokana na upungufu wa chakula nchini na ongezeko la bei ya<br />
mafuta ambayo hayajasafishwa kwenye masoko ulimwenguni<br />
yalisababisha mfumuko wa bei ambao uliongezeka kutoka<br />
asilimia 5.4 kwenye mwezi Januari, <strong>2011</strong> hadi asilimia 19.7<br />
kwenye mwezi wa Novemba, 2010. Kiwango cha wastani cha<br />
mfumuko wa bei kwenye mwaka wa <strong>2011</strong> kilikuwa asilimia<br />
14.0 kikilinganishwa na asilimia 4.1 kwenye mwaka wa 2010.<br />
Ongezeko la matumizi ya kinyumbani na uwekezaji uliochangiwa<br />
na ukuaji katika sekta za kibinafsi za mkopo pia ulichangia kwa<br />
kiasi kikubwa katika mfumko wa bei.<br />
Kutokana na ongezeko la bei ya mafuta ambayo hayajasafishwa,<br />
matumizi ya hali ya juu ya kinyumbani, uwekezaji na ongezeko<br />
la mahitaji ya chakula kutoka nchi za nje na vilevile mafuta ya<br />
kuzalisha umeme yalisababisha kuanguka kwa thamani ya<br />
shilingi ya Kenya dhidi ya sarafu nyingine kuu za kimataifa.<br />
Isitoshe, kuanguka kwa thamani ya shilingi kulisababishwa pia<br />
na kuzorota kwa biashara ya nje ya nchi. Wakati huo ukame<br />
uliathiri vibaya sana uzalishaji wa chai, kahawa na bidhaa za<br />
kilimo cha bustani hali inayojumuisha kiwango kikubwa cha<br />
mazao tunayo safirisha nje ya nchi. Kwa upande mwingine,<br />
kuzorota kwa uchumi katika ukanda wa magharibi mwa Bara-<br />
Yuropa ambalo ndilo miongoni mwa masoko yetu makuu,<br />
yalipunguza mahitaji ya bidhaa zetu kutoka humu nchini. Kwa<br />
upande mwingine, athari za madeni na misukosuko katika<br />
baadhi ya mataifa ya Uarabuni, ilisababisha kudhoofika kwa<br />
Dola ya Marekani na rasilimali zilizotazamiwa na wawekezaji<br />
kuwa salama. Kutokana na mambo hayo yote kufikia Oktoba<br />
<strong>2011</strong>, kiwango cha kubadilisha shilingi dhidi ya Dola ya<br />
Marekani kilipungua hadi asilimia 25 kwa shilingi 107 kwa Dola<br />
ya Marekani na ilifikia wakati shilingi ya Kenya ilitambuliwa<br />
kuwa yenye thamani dhaifu zaidi ulimwenguni.<br />
Ili kusimamisha kuzorota kwa thamani ya shilingi ya Kenya na<br />
kuzuia mfumko wa bei, Benki Kuu ya Kenya (BKK) ilitekeleza<br />
msururu wa hatua za sera za kifedha ambazo zilihusisha<br />
kuongeza kwa haraka kwa Viwango vya Benki Kuu kutoka<br />
asilimia 5.75 hadi asilimia 18 ili kuthibiti tatizo la kubanwa kwa<br />
mzunguko wa fedha nchini na katika masoko ya uwekezaji.<br />
Tatizo hilo sugu la mzunguko wa fedha lilisababisha kupanda<br />
kwa ghafla kwa viwango vya riba. Viwango vya hazina ya fedha<br />
kwa siku 91, siku 182 na siku 364 viliongezeka kwa wastani wa<br />
kila mwezi wa asilimia 2.5, 2.7 na 3.7 katika mwezi wa Januari,<br />
<strong>2011</strong> hadi asilimia 18.3, 18.3 na 21.0 mwezi wa Disemba, <strong>2011</strong><br />
mtawalia. Mwezi wa Januari, <strong>2011</strong> viwango vya mikopo katika<br />
benki kwa benki vilisimamia katika kiwango cha wastani cha<br />
asilimia1.2 na zikaazimia kumaliza mwaka zikiwa na kiwango<br />
cha wastani cha asilimia 21.8.<br />
Kufikia mwisho wa mwaka, Benki Kuu ya Kenya ilikuwa<br />
imefaulu kurudisha hadhi ya shilingi yake na Dola ya Marekani<br />
kupitia kwenye hazina ya fedha ulimwenguni. Huduma ya<br />
Ziada ya Upatikanaji wa Mkopo pia iliboresha zaidi thamani ya<br />
shilingi ya Kenya katika robo ya nne ya mwaka. Kiwango cha<br />
ubadilishanaji wa fedha kufikia mwisho wa mwaka wa <strong>2011</strong><br />
kilifikia kiwango cha wastani wa shilingi 85.1 dhidi ya Dola ya<br />
Marekani.<br />
Wakati ambapo hatua thabiti zilipochukuliwa na Benki Kuu ya<br />
Kenya na kuleta mafanikio katika kuyatimiza malengo yake ya<br />
kuboresha thamani ya shilingi ya Kenya, wakati huu, ni lazima<br />
kuzingatia katika utawala wa viwango vya juu vya riba ambavyo<br />
haviwezi kumudu ukuaji wa uchumi wa mda mrefu na hasara<br />
iliyopo. Hali hii hususan itaathiri Sekta ya Benki ambapo baadhi<br />
ya wateja na wenye kukopa watashindwa kutimiza malengo yao<br />
na kuhudumia mikopo yao ipasavyo na kusababisha matukio<br />
mengi ya kuwa na mikopo mingi isiyolipwa.<br />
Swala la kimsingi zaidi, changamoto nyingi ambazo<br />
zimesababisha mtafaruku huu wa malipo bado<br />
haujashughulikiwa. Gharama ya juu ya kufanya biashara nchini<br />
Kenya imefanya uzalishaji wa bidhaa za humu kutokuwa na<br />
ushindani na kusababisha kuagizwa kwa bidhaa za wanunuzi<br />
na zile zilizotengenezwa nje ya nchi kuletwa kutoka huko<br />
ughaibuni. Kutokuwa na ufanisi katika sekta ya kilimo<br />
imemaanisha kuwa hata baada ya mwaka wa mafanikio ya<br />
kuwepo kwa mvua nyingi bado kuna uhaba wa chakula na<br />
kusababisha umuhimu wa kuagiza chakula kutoka nchi za nje.<br />
Nikiongezea ni kuwa Kenya kwa mda mrefu sasa imekuwa<br />
ikitegemea sana utalii na kuuza bidhaa za msingi za kitamaduni<br />
ambazo zina thamani ndogo, jambo ambalo linatufungia uwezo<br />
wetu wa kupata kiwango cha juu cha pesa za kigeni. Ikiwa sera<br />
na hatua thabiti hazitatekelezwa ili kuzithibiti changamoto hizo,<br />
basi nchi hii itazidi kuathirika kiuchumi kutokana na matatizo<br />
ya usawa wa malipo.<br />
Matokeo ya soko la hisa yalikandamiza mafanikio kuanzia<br />
mwanzo wa mwaka wa <strong>2011</strong> kutokana na “mabadiliko ya kanuni<br />
za uwekezaji kwa wajasirili-amali” yaliyoonekana kwenye<br />
masoko ya kifedha ulimwenguni ambayo yalisababishwa na<br />
tatizo la viwango vya mikopo huko barani Yuropa na kuwepo kwa<br />
wawekezaji wa kigeni katika masoko ya Afrika Kaskazini. Katika<br />
sehemu ya pili ya mwaka, matokeo haya yasiyofaa yalipaliliwa<br />
makaa na viwango vya juu vya riba ambavyo vilisababisha<br />
wawekezaji kuhamisha hazina zao kwenye bidhaa bora za<br />
uzalishaji. Ubora wa hisa ulianguka kila mahali na kusababisha<br />
kupungua kwa asilimia 30 katika kiwango cha hisa cha Soko la<br />
Ubadilishanaji wa Hisa la Nairobi (NSE-20) na kufikia kiwango<br />
cha mwisho cha alama 3,123 mwaka huo wa <strong>2011</strong> kutoka kwa<br />
NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong> • 13