09.11.2014 Views

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

TAARIFA YA MWENYEKITI<br />

matawi manne nchini Tanzania na tuko mbioni kufungua tawi<br />

jingine katika eneo la Kahama.<br />

Kitengo cha shirika cha Utoaji wa Huduma za kielektroniki –<br />

kikiwepo kile cha ‘NIC Mobile Banking na NIC Online Banking’,<br />

vimeimarishwa na kuongezewa kiungo muhimu cha M-pesa,<br />

ambacho kinaunganisha vitengo vyote viwili kwa mpigo. Shirika<br />

hili sasa lina mifumo miwili madhubuti ya kielectroniki iliyo<br />

na utendakazi wa shughuli za benki kwa kutumia rununu na<br />

mtandao. Mifumo hii miwili inawapatia wateja wetu fursa<br />

muafaka ya kupata huduma yoyote mahali popote.<br />

Kulingana na wingi wa wateja na kijiografia, shirika hili<br />

limefanya mkataba wa uwakala na benki ya Posta. Mkataba<br />

huu ambao umeidhinishwa na Benki kuu ya Kenya na ambao<br />

unawezesha benki ya NIC kutoa huduma kwa wateja wake<br />

kupitia mitandao ya matawi 94 kote nchini kwa njia inayofaa<br />

na isiyo na gharama ya juu.<br />

Sababu kuu ya kutaka kuyashughulikia matatizo na maendeleo<br />

ya katika Sekta ya Benki, yameendelea kuzalia mageuzi ya NIC<br />

katika bidhaa na zabuni nyingine kwa wateja. Mafunzo ya Klabu ya<br />

Mjasiriamali, pamoja na kuwatia shime wajasiriamali chipukizi,<br />

imeendelea kuwa chanzo cha kupokea Elimu na maarifa<br />

katika matarajio ya wateja – hali inayopelekea kuongezewa<br />

kwa bidhaa zaidi kaatika kitengo cha Biashara ndogo ndogo<br />

za benki (SME). Shirika limebadilisha na kurekebisha bidhaa<br />

zilizoko na pia kuzindua kampeini zitakazohakikisha kwamba<br />

wateja wetu wanaendelea kuzifahamu vyema bidhaa zetu zote<br />

kadri zinavyokua.<br />

WAFANYAKAZI<br />

Shirika la benki ya NIC lina mpango mkubwa wa kuwavutia na<br />

kukuza vipawa ili kuhakikisha kuwa lina wafanyikazi walio bora<br />

zaidi kwa mahitaji ya kibiashara ya sasa na ya siku sijazo. Bidii<br />

ya kazi kutoka kwa wafanyakazi zimeliwezesha shirika kupata<br />

matokeo bora katika miaka iliyotangulia. Waajiriwa wake<br />

hujenga uhusiano mwema na wateja, wanaotambua nafasi za<br />

kibiashara – zikiwepo kubwa na ndogo – na wanaotoa Huduma<br />

zinazowezesha NIC kukua na kuimarika kama shirika thabiti la<br />

benki.<br />

Kuna mfumo uliopendekezwa wa kusimamia na kuwapa<br />

motisha wafanyakazi kama vile mpango wa kujiendeleza<br />

kikazi na pia njia ya kutwaa majukumu katika nafasi mpya za<br />

kazi , malipo bora , mafundisho na kujiendeleza vilevile kupata<br />

maoni kuhusu utendakazi.<br />

Kupitia bidii ya mchwa na uzingativu,wafanyikazi 596 wa shirika<br />

la benki ya NIC kufikia tarehe 31 Desemba mwaka wa <strong>2011</strong>,<br />

walijitahidi mno ili kutoa huduma za kimataifa za kifedha<br />

huku wakizingatia pia maadili ya ujumla ya kuwa wataalamu,<br />

wabunifu, wenye moyo, wenye kufuata na wenye uadiliifu wa<br />

hali ya juu.<br />

USIMAMIZI BORA WA KIUSHIRIKA<br />

Benki ya NIC ina imani kubwa katika usimamizi wa kiushirika.<br />

Kamati Kuu imeandaa mfumo imara wa uongozi ili uwe kama<br />

kigezo cha jumla cha majukumu ya usimamizi wa kibiashara<br />

na maslahi mengine ya shirika. Ni katika mfumo huu ambapo<br />

maelezo ya kina yanapatikana katika kitengo cha usimamizi<br />

cha pamoja kwenye ripoti hii ili kuhakikisha kwamba malengo<br />

ya kamati na yale ya usimamizi yameainishwa na majukumu<br />

yao yote yanawalenga washika dau wote.<br />

Mafanikio ya usimamizi wa shirika katika utawala wake unazidi<br />

kutambulika na baadhi ya mashirika ya kigeni yanayojulikana<br />

katika kutathmini kwa biashara zilizowajibika. Ninafuraha<br />

kuwaeleza kwamba katika mwaka wa <strong>2011</strong> , shirika la benki ya<br />

NIC lilishinda ,sasa kwa mwaka wa pili mfululizo, Tuzo la Jumla<br />

la Mabingwa wa Utawala na Usimamizi Bora, lililodhaminiwa na<br />

ICSPAK, Benki Kuu Ya Kenya, Halmashauri ya Manufaa Baada<br />

ya Kustaafu na Halmashauri ya Kuthibiti Bima, na wengine<br />

wengi. Benki ya NIC pia ilitangazwa kuwa mshindi katika kitengo<br />

cha Viwango vya Ubora vya Kimataifa vya Utoaji wa Ripoti za<br />

Kifedha (IFRS) pia waliibuka wa pili katika shindalo la Tuzo la<br />

(FiRE), shindano ambalo liliandaliwa na Soko la Hisa la Nairobi<br />

(NSE), Taasisi Ya Wahasibu ya Kenya (ICPAK) na Halmashauri<br />

ya Masoko ya Mtaji (CMA).<br />

JUKUMU LA KIJAMII<br />

Kuwajibikia jamii huwa ni kiungo muhimu sana katika kanuni za<br />

utendakazi za Benki ya NIC. Shirika linanuia kuwapa thamani<br />

washika dau na wabia wake wote na kadhalika kuchangia<br />

ipasavyo katika mazingira, kifedha na maslahi ya kijamii kwa<br />

wateja, wafanyakazi wake, na wanajamii ambao ndio nguzo kuu<br />

ya biashara ya Benki ya NIC.<br />

Katika mwaka wa <strong>2011</strong>, shirika liliendelea kusaidia kwenye<br />

hatua za masomo, mazingira na michezo. Hali kadhalika,<br />

lilijitwika jukumu la kuyashughulikia mahitaji mengine<br />

yanayochipuka.<br />

Katika sehemu ya Elimu, shirika hili liliingia ubia na asasi<br />

muhimu ikiwepo ile ya Palm House Foundation na Edumed<br />

Trust, mashirika yanayowasaidia watoto kifedha ili kuendelea<br />

kimasomo. Hawa huwa ni watoto werevu na wenye vipawa lakini<br />

hawana uwezo wa kifedha. NIC huchukua jukumu la kuwasaidia<br />

wanajamii kupitia kwa mashirika hayo mawili. Kwa kuwasaidia<br />

watoto hawa katika shule za upili na kuwapa ushauri, shirika<br />

la benki ya NIC huwapa nafasi ya kuboresha maisha yao na ya<br />

familia zao.<br />

Kupitia ‘Junior Achievements Kenya’ ambayo ni sehemu ya<br />

‘Junior Achievements Worldwide’, shirika lililosaidia vijana wa<br />

Kikenya ili kuwawezesha kujiandaa kikazi kwa siku za usoni,<br />

kuwapa maarifa na kuwafunza mbinu za ujasiri-amali kupitia<br />

kwa miradi ama programu za JA.<br />

Kadhalika, Shirika la Benki ya NIC huwapatia wanafunzi nafasi<br />

za masomo ya kila mwaka ya huko nyanjani. Masomo haya ya<br />

nyanjani huwawezesha mwanafunzi kuyazoea mazingira ya<br />

kuajiriwa<br />

Kuhusu mazingira katika mwaka wa <strong>2011</strong> ukiwa mwaka wa<br />

tatu mfululizo, shirika lilihusika katika kampeini ya ‘’Tupande<br />

Pamoja” shughuli ya kupanda miti kwenye msimu wa Krismasi.<br />

Tupande paamoja ni kampeini iliyowashirikisha wafanyakazi wa<br />

NIC na wale wa UNEP , vile vile shirika la Misitu nchini kwa<br />

16 • NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong>

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!