Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
TAARIFA YA MWENYEKITI<br />
matawi manne nchini Tanzania na tuko mbioni kufungua tawi<br />
jingine katika eneo la Kahama.<br />
Kitengo cha shirika cha Utoaji wa Huduma za kielektroniki –<br />
kikiwepo kile cha ‘NIC Mobile Banking na NIC Online Banking’,<br />
vimeimarishwa na kuongezewa kiungo muhimu cha M-pesa,<br />
ambacho kinaunganisha vitengo vyote viwili kwa mpigo. Shirika<br />
hili sasa lina mifumo miwili madhubuti ya kielectroniki iliyo<br />
na utendakazi wa shughuli za benki kwa kutumia rununu na<br />
mtandao. Mifumo hii miwili inawapatia wateja wetu fursa<br />
muafaka ya kupata huduma yoyote mahali popote.<br />
Kulingana na wingi wa wateja na kijiografia, shirika hili<br />
limefanya mkataba wa uwakala na benki ya Posta. Mkataba<br />
huu ambao umeidhinishwa na Benki kuu ya Kenya na ambao<br />
unawezesha benki ya NIC kutoa huduma kwa wateja wake<br />
kupitia mitandao ya matawi 94 kote nchini kwa njia inayofaa<br />
na isiyo na gharama ya juu.<br />
Sababu kuu ya kutaka kuyashughulikia matatizo na maendeleo<br />
ya katika Sekta ya Benki, yameendelea kuzalia mageuzi ya NIC<br />
katika bidhaa na zabuni nyingine kwa wateja. Mafunzo ya Klabu ya<br />
Mjasiriamali, pamoja na kuwatia shime wajasiriamali chipukizi,<br />
imeendelea kuwa chanzo cha kupokea Elimu na maarifa<br />
katika matarajio ya wateja – hali inayopelekea kuongezewa<br />
kwa bidhaa zaidi kaatika kitengo cha Biashara ndogo ndogo<br />
za benki (SME). Shirika limebadilisha na kurekebisha bidhaa<br />
zilizoko na pia kuzindua kampeini zitakazohakikisha kwamba<br />
wateja wetu wanaendelea kuzifahamu vyema bidhaa zetu zote<br />
kadri zinavyokua.<br />
WAFANYAKAZI<br />
Shirika la benki ya NIC lina mpango mkubwa wa kuwavutia na<br />
kukuza vipawa ili kuhakikisha kuwa lina wafanyikazi walio bora<br />
zaidi kwa mahitaji ya kibiashara ya sasa na ya siku sijazo. Bidii<br />
ya kazi kutoka kwa wafanyakazi zimeliwezesha shirika kupata<br />
matokeo bora katika miaka iliyotangulia. Waajiriwa wake<br />
hujenga uhusiano mwema na wateja, wanaotambua nafasi za<br />
kibiashara – zikiwepo kubwa na ndogo – na wanaotoa Huduma<br />
zinazowezesha NIC kukua na kuimarika kama shirika thabiti la<br />
benki.<br />
Kuna mfumo uliopendekezwa wa kusimamia na kuwapa<br />
motisha wafanyakazi kama vile mpango wa kujiendeleza<br />
kikazi na pia njia ya kutwaa majukumu katika nafasi mpya za<br />
kazi , malipo bora , mafundisho na kujiendeleza vilevile kupata<br />
maoni kuhusu utendakazi.<br />
Kupitia bidii ya mchwa na uzingativu,wafanyikazi 596 wa shirika<br />
la benki ya NIC kufikia tarehe 31 Desemba mwaka wa <strong>2011</strong>,<br />
walijitahidi mno ili kutoa huduma za kimataifa za kifedha<br />
huku wakizingatia pia maadili ya ujumla ya kuwa wataalamu,<br />
wabunifu, wenye moyo, wenye kufuata na wenye uadiliifu wa<br />
hali ya juu.<br />
USIMAMIZI BORA WA KIUSHIRIKA<br />
Benki ya NIC ina imani kubwa katika usimamizi wa kiushirika.<br />
Kamati Kuu imeandaa mfumo imara wa uongozi ili uwe kama<br />
kigezo cha jumla cha majukumu ya usimamizi wa kibiashara<br />
na maslahi mengine ya shirika. Ni katika mfumo huu ambapo<br />
maelezo ya kina yanapatikana katika kitengo cha usimamizi<br />
cha pamoja kwenye ripoti hii ili kuhakikisha kwamba malengo<br />
ya kamati na yale ya usimamizi yameainishwa na majukumu<br />
yao yote yanawalenga washika dau wote.<br />
Mafanikio ya usimamizi wa shirika katika utawala wake unazidi<br />
kutambulika na baadhi ya mashirika ya kigeni yanayojulikana<br />
katika kutathmini kwa biashara zilizowajibika. Ninafuraha<br />
kuwaeleza kwamba katika mwaka wa <strong>2011</strong> , shirika la benki ya<br />
NIC lilishinda ,sasa kwa mwaka wa pili mfululizo, Tuzo la Jumla<br />
la Mabingwa wa Utawala na Usimamizi Bora, lililodhaminiwa na<br />
ICSPAK, Benki Kuu Ya Kenya, Halmashauri ya Manufaa Baada<br />
ya Kustaafu na Halmashauri ya Kuthibiti Bima, na wengine<br />
wengi. Benki ya NIC pia ilitangazwa kuwa mshindi katika kitengo<br />
cha Viwango vya Ubora vya Kimataifa vya Utoaji wa Ripoti za<br />
Kifedha (IFRS) pia waliibuka wa pili katika shindalo la Tuzo la<br />
(FiRE), shindano ambalo liliandaliwa na Soko la Hisa la Nairobi<br />
(NSE), Taasisi Ya Wahasibu ya Kenya (ICPAK) na Halmashauri<br />
ya Masoko ya Mtaji (CMA).<br />
JUKUMU LA KIJAMII<br />
Kuwajibikia jamii huwa ni kiungo muhimu sana katika kanuni za<br />
utendakazi za Benki ya NIC. Shirika linanuia kuwapa thamani<br />
washika dau na wabia wake wote na kadhalika kuchangia<br />
ipasavyo katika mazingira, kifedha na maslahi ya kijamii kwa<br />
wateja, wafanyakazi wake, na wanajamii ambao ndio nguzo kuu<br />
ya biashara ya Benki ya NIC.<br />
Katika mwaka wa <strong>2011</strong>, shirika liliendelea kusaidia kwenye<br />
hatua za masomo, mazingira na michezo. Hali kadhalika,<br />
lilijitwika jukumu la kuyashughulikia mahitaji mengine<br />
yanayochipuka.<br />
Katika sehemu ya Elimu, shirika hili liliingia ubia na asasi<br />
muhimu ikiwepo ile ya Palm House Foundation na Edumed<br />
Trust, mashirika yanayowasaidia watoto kifedha ili kuendelea<br />
kimasomo. Hawa huwa ni watoto werevu na wenye vipawa lakini<br />
hawana uwezo wa kifedha. NIC huchukua jukumu la kuwasaidia<br />
wanajamii kupitia kwa mashirika hayo mawili. Kwa kuwasaidia<br />
watoto hawa katika shule za upili na kuwapa ushauri, shirika<br />
la benki ya NIC huwapa nafasi ya kuboresha maisha yao na ya<br />
familia zao.<br />
Kupitia ‘Junior Achievements Kenya’ ambayo ni sehemu ya<br />
‘Junior Achievements Worldwide’, shirika lililosaidia vijana wa<br />
Kikenya ili kuwawezesha kujiandaa kikazi kwa siku za usoni,<br />
kuwapa maarifa na kuwafunza mbinu za ujasiri-amali kupitia<br />
kwa miradi ama programu za JA.<br />
Kadhalika, Shirika la Benki ya NIC huwapatia wanafunzi nafasi<br />
za masomo ya kila mwaka ya huko nyanjani. Masomo haya ya<br />
nyanjani huwawezesha mwanafunzi kuyazoea mazingira ya<br />
kuajiriwa<br />
Kuhusu mazingira katika mwaka wa <strong>2011</strong> ukiwa mwaka wa<br />
tatu mfululizo, shirika lilihusika katika kampeini ya ‘’Tupande<br />
Pamoja” shughuli ya kupanda miti kwenye msimu wa Krismasi.<br />
Tupande paamoja ni kampeini iliyowashirikisha wafanyakazi wa<br />
NIC na wale wa UNEP , vile vile shirika la Misitu nchini kwa<br />
16 • NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong>