Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
Financial Statements 2011 - Investing In Africa
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
TAARIFA YA MWENYEKITI<br />
<strong>2011</strong>, mgao ambao uliokuwa haujaidhinishwa kikamilifu.<br />
Wakurugenzi sasa wanapendekeza mgao wa mwisho wa mwaka<br />
wa <strong>2011</strong> wa shilling 0.25 kwa kila hisa (Shilingi milioni 99) ili<br />
kujumlisha mgao taslim wa mwaka huo wa shilingi milioni 198.<br />
(2010 – Shilingi milioni 179)<br />
Zaidi ya hayo, wakurugenzi wanapendekeza gawio la ziada<br />
kwa mwenye hisa kwenye sehemu ya hisa moja (1) ya kawaida<br />
kwa kila hisa kumi (10) za hisa za kawaida ambazo zimelipiwa<br />
kabisa.<br />
Ukijumlisha pamoja mgao taslim na gawio la ziada kwa mwenye<br />
hisa ni shilingi milioni 396.<br />
Ili kufikia mapendekezo haya, kamati ilichukua hatua za<br />
kimsingi na umakinifu za nafasi ya mtaji wa shirika pamoja na<br />
mipango na mikakati ya ukuaji iliyopo. Baada ya mazingatio ya<br />
kina, iliafikiwa kuwa Kiwango imara cha Shirika la Benki la NIC<br />
kiboreshwe zaidi na hivyo basi wakurugenzi wakapendekeza<br />
idhini ya kuongeza mtaji wa shilingi bilioni 2 wa gawio la haki<br />
kwa kila mwenye hisa kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka.<br />
Gawio la ziada na lile la haki kwa kila mwenye hisa hutegemea<br />
kuidhinishwa na Mamlaka ya Mtaji wa Masoko.<br />
MASHIRIKA-TANZU NA MAZINGIRA YA UANUAI WA<br />
KIBIASHARA<br />
Moja wapo ya nguzo ya mikakati ya Shirika inayonuiwa<br />
kudumisha, uimarisha na kuthibiti ni kukuza biashara yenye<br />
njia mbalimbali za mapato, vitengo vya kibiashara, aina za<br />
wateja na kujipanua kwenye maeneo mbalimbali.<br />
Lengo la jumla ni kuwajibika katika kupata mapato makuu<br />
na yanayodumu katika kila eneo la kibiashara na nina furaha<br />
kuripoti kuwa matawi ya biashara yalifanikiwa kupata faida<br />
katika mwaka wa <strong>2011</strong>, hivyo basi, kuchangia pakubwa katika<br />
mafanikio ya Shirika hili.<br />
Ubora uliopatikana kwenye utenda kazi wa benki ya NIC<br />
Tanzania ni wa faida ukilinganishwa na kuwekeza kwetu kwa<br />
mara ya kwanza katika mataifa ya nje. Katika mwaka wa <strong>2011</strong>,<br />
biashara zetu zilileta faida sawa na milioni 153 ikilinganishwa<br />
na shilingi milioni 133 katika mwaka wa 2010. Twatarajia<br />
utendakazi wa benki ya NIC Tanzania utakuwa bora zaidi jinsi<br />
matawi ya mitandao ya kibiashara inavyozidi kupanuka na<br />
kuanzisha bidhaa na huduma mpya. Utekelezaji wa mfumo<br />
mpya halisi wa benki, T24, utawezesha kujumuishwa kwa<br />
shughuli na huduma za kimaeneo katika kutambua uwezo wa<br />
Shirika.<br />
Mtaji wa uwekezaji kwenye Shirika la Benki ya NIC ulitia fora<br />
zaidi huku ukipata faida ya karibu maradufu sawa na milioni 60<br />
(2010-shs 32m). Biashara hizi sasa zaongoza katika ushauri wa<br />
kifedha na zinazidi kujenga soko la hisa katika masoko ya hisa<br />
na mtaji wa mikopo.<br />
Kitengo cha Udalali wa Biashara cha NIC Securities uliendelea<br />
katika soko la hisa lakini uliathirika sana na wanunuzi wa<br />
hisa wa jumla katika soko la hisa la Nairobi (Nairobi securities<br />
Exchange)na kupata faida ya shilingi milioni 11 kabla ya kutozwa<br />
ushuru (<strong>2011</strong>-shs 20m) Kampuni tanzu hii sasa zaweza kupata<br />
mapato bora pindi soko la hisa likifidia gharama zake.<br />
Kampuni tanzu za maswala ya fedha, ikiwepo NIC <strong>In</strong>surance<br />
Agents, walipata faida ya kupigiwa mfano ya shilingi milioni 17<br />
(2010- shs milioni 5)<br />
Kwa jumla, kampuni-tanzu za shirika zilichangia asilimia 7%<br />
(au shilingi milioni 244) ya mwaka katika kuongezeka kwa faida<br />
ya Shirika kabla ya kutozwa ushuru.<br />
Matokeo ya kuridhisha kutoka kwa kampuni-tanzu zetu,<br />
hususan, benki ya NIC Tanzania, na muungano unaoendelea<br />
wa Jumuiyya ya Afrika Mashariki ulichochea shirika<br />
kutafuta nafasi zaidi katika upanuzi kwenye maeneo mapya<br />
ya kuwekeza. Baada ya upembuzi yakinifu, kamati ilipitisha<br />
kuanzisha kwa kampuni-tanzu ya benki ya biashara nchini<br />
Uganda. Kampuni-Tanzu mpya ya benki ya NC Uganda<br />
itawezesha shirika kupanuka kijiografia katika mataifa matatu<br />
ya Muungano wa Afrika Mashariki. Kuanzishwa kwa kampunitanzu<br />
hii kwa mtaji wa shilingi milioni 961 (shilingi bilioni 25<br />
pesa za Uganda) kutategemea kuidhinishwa rasmi na wenye<br />
hisa katika Mkutano wa Mkuu kila mwaka.<br />
UTOAJI WA HUDUMA NA BIDHAA<br />
Shirika limeamua kutoa huduma za kifedha zitazopatikana kwa<br />
urahisi na zinazofaa kwenye upanuzi wa maeneo na hivyo basi<br />
limeendelea kuboresha uwezo wake wa kiteknolojia.<br />
Mfumo madhubuti wa utekelezaji wa shughuli za benki na<br />
unaofahamika kama T24, na uliotoka kwa shirika la Temenos,<br />
ndio sasa unaendelea kutekelezwa. Mfumo huu wa kifahari<br />
utawezesha shirika hili kutoa huduma zinazofaa na za kimataifa<br />
kwa wateja na uwe msingi wa bidhaa nyingine bora na mageuzi<br />
yatakayozinduliwa. Mfumo huu pia unashughulikiwa kwenye<br />
kampuni-tanzu na hii ni ishara kwamba bidhaa na huduma zote<br />
za NIC zitapatikana katika maeneo yote.<br />
Kwa sasa, mpango wa kupanua matawi unaendelea. Hata<br />
hivyo mpango huu unaendelea kufaulu baada ya kupokelewa<br />
vyema na wateja. Katika mwaka wa <strong>2011</strong> shirika lilifungua<br />
matawi saba kwenye eneo hilo ili kutumia na kuwahi nafasi<br />
muruwa za uwekezaji kwenye soko, na kadhalika kuhakikisha<br />
kwamba wateja katika mji mkubwa na unaopanuka wa Nairobi<br />
wanafuraahia na kufikia kwa urahisi huduma za shirika.Matawi<br />
mapya yamefunguliwa katika maeneo ya Village Market,<br />
Sameer Business Park, Galleria Mall, Karen Office Park na Taj<br />
Mall (Embakasi). Pia tulifungua tawi katika mji wa Eldoret ili<br />
kushugulikia eneo kubwa la Bonde la Ufa ambapo tawi la Nyali<br />
lilihamishiwa sehemu inayofaa zaidi. Kwa faida na manufaa ya<br />
wateja muda wa huduma za benki umeongezwa kwenye baadhi<br />
ya matawi.<br />
Kwenye eneo la Afrika Mashariki, shirika limefungua tawi<br />
la pili huko jijini Dar es Saalam kwa lengo la kushughulikia<br />
msongomano wa biashara karibu na mtaa wa Kariokor na<br />
vituo vya biashara vya Ilala. Tawi la Ilala na matawi mengine<br />
ya zamani katika miji ya Arusha na Mwanza kufikisha idadi ya<br />
NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong> • 15