09.11.2014 Views

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

Financial Statements 2011 - Investing In Africa

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

TAARIFA YA MWENYEKITI<br />

<strong>2011</strong>, mgao ambao uliokuwa haujaidhinishwa kikamilifu.<br />

Wakurugenzi sasa wanapendekeza mgao wa mwisho wa mwaka<br />

wa <strong>2011</strong> wa shilling 0.25 kwa kila hisa (Shilingi milioni 99) ili<br />

kujumlisha mgao taslim wa mwaka huo wa shilingi milioni 198.<br />

(2010 – Shilingi milioni 179)<br />

Zaidi ya hayo, wakurugenzi wanapendekeza gawio la ziada<br />

kwa mwenye hisa kwenye sehemu ya hisa moja (1) ya kawaida<br />

kwa kila hisa kumi (10) za hisa za kawaida ambazo zimelipiwa<br />

kabisa.<br />

Ukijumlisha pamoja mgao taslim na gawio la ziada kwa mwenye<br />

hisa ni shilingi milioni 396.<br />

Ili kufikia mapendekezo haya, kamati ilichukua hatua za<br />

kimsingi na umakinifu za nafasi ya mtaji wa shirika pamoja na<br />

mipango na mikakati ya ukuaji iliyopo. Baada ya mazingatio ya<br />

kina, iliafikiwa kuwa Kiwango imara cha Shirika la Benki la NIC<br />

kiboreshwe zaidi na hivyo basi wakurugenzi wakapendekeza<br />

idhini ya kuongeza mtaji wa shilingi bilioni 2 wa gawio la haki<br />

kwa kila mwenye hisa kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka.<br />

Gawio la ziada na lile la haki kwa kila mwenye hisa hutegemea<br />

kuidhinishwa na Mamlaka ya Mtaji wa Masoko.<br />

MASHIRIKA-TANZU NA MAZINGIRA YA UANUAI WA<br />

KIBIASHARA<br />

Moja wapo ya nguzo ya mikakati ya Shirika inayonuiwa<br />

kudumisha, uimarisha na kuthibiti ni kukuza biashara yenye<br />

njia mbalimbali za mapato, vitengo vya kibiashara, aina za<br />

wateja na kujipanua kwenye maeneo mbalimbali.<br />

Lengo la jumla ni kuwajibika katika kupata mapato makuu<br />

na yanayodumu katika kila eneo la kibiashara na nina furaha<br />

kuripoti kuwa matawi ya biashara yalifanikiwa kupata faida<br />

katika mwaka wa <strong>2011</strong>, hivyo basi, kuchangia pakubwa katika<br />

mafanikio ya Shirika hili.<br />

Ubora uliopatikana kwenye utenda kazi wa benki ya NIC<br />

Tanzania ni wa faida ukilinganishwa na kuwekeza kwetu kwa<br />

mara ya kwanza katika mataifa ya nje. Katika mwaka wa <strong>2011</strong>,<br />

biashara zetu zilileta faida sawa na milioni 153 ikilinganishwa<br />

na shilingi milioni 133 katika mwaka wa 2010. Twatarajia<br />

utendakazi wa benki ya NIC Tanzania utakuwa bora zaidi jinsi<br />

matawi ya mitandao ya kibiashara inavyozidi kupanuka na<br />

kuanzisha bidhaa na huduma mpya. Utekelezaji wa mfumo<br />

mpya halisi wa benki, T24, utawezesha kujumuishwa kwa<br />

shughuli na huduma za kimaeneo katika kutambua uwezo wa<br />

Shirika.<br />

Mtaji wa uwekezaji kwenye Shirika la Benki ya NIC ulitia fora<br />

zaidi huku ukipata faida ya karibu maradufu sawa na milioni 60<br />

(2010-shs 32m). Biashara hizi sasa zaongoza katika ushauri wa<br />

kifedha na zinazidi kujenga soko la hisa katika masoko ya hisa<br />

na mtaji wa mikopo.<br />

Kitengo cha Udalali wa Biashara cha NIC Securities uliendelea<br />

katika soko la hisa lakini uliathirika sana na wanunuzi wa<br />

hisa wa jumla katika soko la hisa la Nairobi (Nairobi securities<br />

Exchange)na kupata faida ya shilingi milioni 11 kabla ya kutozwa<br />

ushuru (<strong>2011</strong>-shs 20m) Kampuni tanzu hii sasa zaweza kupata<br />

mapato bora pindi soko la hisa likifidia gharama zake.<br />

Kampuni tanzu za maswala ya fedha, ikiwepo NIC <strong>In</strong>surance<br />

Agents, walipata faida ya kupigiwa mfano ya shilingi milioni 17<br />

(2010- shs milioni 5)<br />

Kwa jumla, kampuni-tanzu za shirika zilichangia asilimia 7%<br />

(au shilingi milioni 244) ya mwaka katika kuongezeka kwa faida<br />

ya Shirika kabla ya kutozwa ushuru.<br />

Matokeo ya kuridhisha kutoka kwa kampuni-tanzu zetu,<br />

hususan, benki ya NIC Tanzania, na muungano unaoendelea<br />

wa Jumuiyya ya Afrika Mashariki ulichochea shirika<br />

kutafuta nafasi zaidi katika upanuzi kwenye maeneo mapya<br />

ya kuwekeza. Baada ya upembuzi yakinifu, kamati ilipitisha<br />

kuanzisha kwa kampuni-tanzu ya benki ya biashara nchini<br />

Uganda. Kampuni-Tanzu mpya ya benki ya NC Uganda<br />

itawezesha shirika kupanuka kijiografia katika mataifa matatu<br />

ya Muungano wa Afrika Mashariki. Kuanzishwa kwa kampunitanzu<br />

hii kwa mtaji wa shilingi milioni 961 (shilingi bilioni 25<br />

pesa za Uganda) kutategemea kuidhinishwa rasmi na wenye<br />

hisa katika Mkutano wa Mkuu kila mwaka.<br />

UTOAJI WA HUDUMA NA BIDHAA<br />

Shirika limeamua kutoa huduma za kifedha zitazopatikana kwa<br />

urahisi na zinazofaa kwenye upanuzi wa maeneo na hivyo basi<br />

limeendelea kuboresha uwezo wake wa kiteknolojia.<br />

Mfumo madhubuti wa utekelezaji wa shughuli za benki na<br />

unaofahamika kama T24, na uliotoka kwa shirika la Temenos,<br />

ndio sasa unaendelea kutekelezwa. Mfumo huu wa kifahari<br />

utawezesha shirika hili kutoa huduma zinazofaa na za kimataifa<br />

kwa wateja na uwe msingi wa bidhaa nyingine bora na mageuzi<br />

yatakayozinduliwa. Mfumo huu pia unashughulikiwa kwenye<br />

kampuni-tanzu na hii ni ishara kwamba bidhaa na huduma zote<br />

za NIC zitapatikana katika maeneo yote.<br />

Kwa sasa, mpango wa kupanua matawi unaendelea. Hata<br />

hivyo mpango huu unaendelea kufaulu baada ya kupokelewa<br />

vyema na wateja. Katika mwaka wa <strong>2011</strong> shirika lilifungua<br />

matawi saba kwenye eneo hilo ili kutumia na kuwahi nafasi<br />

muruwa za uwekezaji kwenye soko, na kadhalika kuhakikisha<br />

kwamba wateja katika mji mkubwa na unaopanuka wa Nairobi<br />

wanafuraahia na kufikia kwa urahisi huduma za shirika.Matawi<br />

mapya yamefunguliwa katika maeneo ya Village Market,<br />

Sameer Business Park, Galleria Mall, Karen Office Park na Taj<br />

Mall (Embakasi). Pia tulifungua tawi katika mji wa Eldoret ili<br />

kushugulikia eneo kubwa la Bonde la Ufa ambapo tawi la Nyali<br />

lilihamishiwa sehemu inayofaa zaidi. Kwa faida na manufaa ya<br />

wateja muda wa huduma za benki umeongezwa kwenye baadhi<br />

ya matawi.<br />

Kwenye eneo la Afrika Mashariki, shirika limefungua tawi<br />

la pili huko jijini Dar es Saalam kwa lengo la kushughulikia<br />

msongomano wa biashara karibu na mtaa wa Kariokor na<br />

vituo vya biashara vya Ilala. Tawi la Ilala na matawi mengine<br />

ya zamani katika miji ya Arusha na Mwanza kufikisha idadi ya<br />

NIC Bank Limited • Annual Report & <strong>Financial</strong> <strong>Statements</strong> <strong>2011</strong> • 15

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!