08.06.2013 Views

Ufunuo - kanisalakristo

Ufunuo - kanisalakristo

Ufunuo - kanisalakristo

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kwakuwa Yesu anakuja. Kwakuwa Kristo anakuja tena kutuchukua nyumbani hivyo twahitaji kwenda<br />

kwake 22:17-21. Ndio maana Roho, Bibi Arusi na Mungu wanasema “Njoo.”<br />

Falsafa (Theory):<br />

Kuna aina mbali mbali za tafsiri ya falsafa (theories) katika kitabu cha <strong>Ufunuo</strong>. Nyingi kati ya hizo hazina<br />

msingi wowote. Lakini kadili tunavyojifunza kitabu hiki tunahitaji kuwa na mawazo pevu kwa kuangalia<br />

ujumla katika maandiko. Kama kuna mtazamo tunaoweza kuuamini na mtazumo huo ni tofauti na<br />

mafundisho mengine basi hatuwezi kuuacha hivihivi. Hatuwezi kuamini jambo ambalo ni tofauti na<br />

maandiko mengine ya Biblia. Lakini tunachopaswa kukumbuka ni kwamba kitabu kiliandikwa kwa<br />

Wakristo wa sehemu ya baadae katika karne ya kwanza. Na Imani tuliyonayo ni lazima iwe kwa faida yao.<br />

Yaonekana kuwapo falsafa kuu nne kwenye hiki kitabu. Hata hivyo pengine zipo maelfu ya falsafa ndogo.<br />

Moja yajionyesha kuwa ya baadae. Maana yake ni kwamba mambo yaliyoandikwa katika sura ya 4 -20.<br />

Bado hayajatimia. Wanaanini kuwa yatatimizwa atakaporudi Yesu. Na Falsafa ya pili na ya kihistoria<br />

kwamba mambo yamewekwa kwenye historia ambayo inachukua nafasi mpaka Yesu atarudi tena<br />

yanafundishwa zaidi na Wakathoriki. falsafa ya tatu mtazamo wa utimilifu ikiwa na maana kwamba kila<br />

kitu kilitimia wakati wa kipindi cha kuandika katika mtazamo ya misingi ya unabii wa kipindi cha mwisho<br />

wa binadamu Falsafa (Theory) ya nne ni mtazamo wa kiroho ukimaanisha kuwa maono yote na unabii<br />

haukuwa halisi sio kwamba unahusu jambo maalumu.<br />

Hizi Falsafa (Theory) zote zimesomwa kwa miaka mingi na watu wameamua kuzifuata lakini watu pia<br />

wamekuta matatizo mengi katika falsafa hizi. Hivyo njia rahisi ya kujifunza kitabu cha <strong>Ufunuo</strong> ni kujifunza<br />

bila kuweka mambo yote katika falsafa tukiwa tunakumbuka kuwa katika kitabu hiki hakikuandikwa kwa<br />

ajili yetu kiliandikwa ili kuwasaidia wazee wetu kuwapa imani kwa maswali yao mengi kuhusiana na jinsi<br />

walivyoamini kwa muda mrefu.<br />

Zipo pia falsafa (Theory) tofauti zenye misingi ya utawala wa miaka 1,000 tunayoisoma katika kitabu<br />

hiki. Hizo Falsafa tuzisikiazo kila mara kwenye madhehebu kwanza ni ya umileniam ni falsafa<br />

iliyogawanyika lakini pointi yake kuu ni kuwa Kristo alishindwa kuweka ufalme wake wakati wa kipindi<br />

cha utawala wa Rumi na, atarudi kutawala kutoka kiti cha Daudi kwa miaka 1,000 kutoka Yerusalem. Pia<br />

kuna kipindi baada ya mileniam wanaamini kuwa Yesu atarudi baada ya kuwa ametawala miaka 1,000 na<br />

hapo kuna wamileniam wanaamini kuwa miaka 1,000 inaonyesha kipindi kisicho na mwisho.<br />

Tarehe:<br />

Kitabu kinazo tarehe kuu mbili ambazo zimependekezwa na watu siku hizi. Wengine wanadai kitabu<br />

kimeandikwa wakati fulani kabla ya kuharibiwa kwa Yerusalem 67 -69 Bk. Na wengine wanaamini kitabu<br />

kimeandikwa wakati wa utawala wa Douisian karibu 95-96 Bk.<br />

Twaweza kuona katika kitabu hiki kuwa Wakristo katika Asia Ndogo walikuwa chini ya uangalizi mkubwa<br />

- wakati wa utawala wa Kiroma kabla ya kuharibiwa Yerusalem Wakristo walikuwa hawana mateso yoyote<br />

lakini Domitian aliyetawala toka 81-96 Bk. Aliwatawala Wakristo kwa ukali akiamini kuwa alikuwa<br />

Mungu na anaongea kwa Mamlaka ya Mungu hivyo adha ikatokea Asia Ndogo mpaka mwisho wa utawala<br />

wa Domintian.<br />

Namba Za Biblia:<br />

Moja - Umoja, upekee, peke yake angalia Efe. 4:3-5.<br />

Mbili - Namba mbili inaonyesha nguvu na hatari kwa maisha ya kizamani. Wakati fulani Yesu<br />

aliwatuma wanafunzi wake wawili wawili. Musa alituma wapelelezi wake wawili wawili. Nuhu<br />

aliingiza wanyama wawili wawili. Katika <strong>Ufunuo</strong> 11 tunaona mashahidi wawili wanasimamia<br />

mshahidi mwenye nguvu. Wanyama (Beasts) wawili wanaonekana kama adui mwenye nguvu.<br />

Tuangalia Yoh. 15:26-27; Luka 10:1.<br />

Tatu - Ni mfano wa Uungu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu) Mt. 3:13-17; 28:18-20.<br />

4

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!