05.04.2016 Views

our roots

Connect2015

Connect2015

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kuimarishwa na KUTUMIwa<br />

kwa Kiswahili - Hatua Muhimu Ya<br />

Kuhakikisha Umoja Katika Jumuiya<br />

Ya Afrika Mashariki<br />

Na Aron Mtunji<br />

Kwa muda mrefu sasa, wana-Afrika<br />

Mashariki wametamani kuwa na<br />

Uhuru wa kufanya biashara pamoja,<br />

kuzitembelea nchi jirani bila ya<br />

kuwepo kwa vizuizi vyovyote na zaidi ya<br />

hayo, kuona kuwa kuna amani kati ya nchi<br />

husika. Zote hizi ni ndoto zinazoweka kuwa<br />

kweli.<br />

Ili kuwepo na mambo yote haya, kuna<br />

mengi ambayo yamefanywa, yanayotendeka<br />

sasa na yaliyo katika akili za washika dau<br />

katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika<br />

makala haya, nitazungumzia juhudi hizi na<br />

kuwaeleza jinsi kuwepo kwa lugha moja<br />

inayowaunganisha wana-Afrika Mashariki<br />

kutaziwezesha kuwa kweli.<br />

Kwanza kabisa, ili kufanya biashara,<br />

kujihusisha katika siasa au kufanya lolote<br />

lile, ni lazima kuwe na mawasiliano. Ili<br />

yote haya yatendeke, tunahitaji lugha<br />

tutakayoweza kuitumia na kuelewana, tuwe<br />

Uganda, Kenya, Tanzania, Rwanda au katika<br />

nchi yoyote ya Afrika Mashariki.<br />

Moja kati ya juhudi za kufanya hivi<br />

ni kuwepo kwa jumia iliyo na umoja.<br />

Kuvunjika kwa jumuiya ya Afrika Mashariki<br />

mwaka 1977 kulisababisha athari kubwa:<br />

kukosekana kwa ajira, kutokuwa na<br />

uaminifu kati ya nchi husika na kusitishwa<br />

ka uhuru wa wananchi wa nchi hizi<br />

kutembea ndani ya jumuiya. Pia, hakukuwa<br />

na usawa wala uhuru wa kufanya huduma<br />

za pamoja, jambo ambalo liliathiri<br />

uchumi, uhusiano, siasa na zaidi ya hayo…<br />

mawasiliano.<br />

Baada ya kufufuliwa kwa jumuiya hii,<br />

matunda ya kuwepo kwa umoja yalianza<br />

kuonekana, jambo ambalo lilikuwa funzo<br />

kwa nchi wanachama.<br />

Pili, Jumuiya ya Afrika Mashariki<br />

imehakikisha kuwa kuna ‘tume ya Kiswahili<br />

ya Afrika Mashariki.’Lengo kuu la tume<br />

hii ni kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili<br />

imeimarika, kama njia moja ya kuhakikisha<br />

kuwa kuna umoja na urahisi katika<br />

mawasiliano yanayohusisha siasa, shughuli<br />

za kifedha, shughuli za kijamii, za tamaduni,<br />

teknolojia na masomo.<br />

Mkataba uliotiwa sahihi mwaka 1999<br />

uliimarisha uhusiano kati ya nchi husika.<br />

Kipengee muhimu katika mkataba huu<br />

(137) kiliitaja lugha ya Kiswahili kama lingua<br />

franca ya nchi za Afrika Mashariki. Hivyo<br />

basi, lilikuwa jambo muhimu kwa nchi hizi<br />

kuunda baraza au chama ambacho lengo<br />

lake lingekuwa kuhakikisha kuwa lugha ya<br />

Kiswahili imetumiwa kuimarisha umoja,<br />

kuhakikisha kuwa Kiswahili kimetumiwa<br />

kama lugha ya jumuiya na kuhakikisha kuwa<br />

lugha hii imetumiwa katika mawasiliano.<br />

Kisha, mipango ya kuwasaidia walio na<br />

matatizo ya kimawasiliano kwa lugha ya<br />

Kiswahili, kubadilishana kwa waalimu na<br />

wanafunzi wa Kiswahili baina ya shule za<br />

nchi husika na kuzisaidia serikali za nchi hizi<br />

katika juhudi za kuimarisha Kiswahili ni kati<br />

ya ajenda walizokuwa nazo.<br />

Lengo kuu lilikuwa kuwepo kwa vituo<br />

vya utafiti vya Kiswahili katika nchi za Afrika<br />

Mashariki, kuwepo kwa waalimu wa lugha<br />

hii ambao wangeifunza katika vyuo vilivyo<br />

katika nchi hizi na kuleta mabadiliko katika<br />

MTAALA unaotumiwa katika shule za Afrika<br />

mashariki, hasa zile za masomo ya juu kwa<br />

kukifanya Kiswahili kuwa kati ya lugha rasmi<br />

zinazotumiwa.<br />

Kufikia sasa, Marais wan chi za Afrika<br />

Mashariki wameunga mkono hatua hii.<br />

Rais wa Kenya, Mheshimiwa Kenyatta<br />

akiongea katika mkutano wa EALA (East<br />

African Legislative Assembly) tarehe ishirini<br />

na sita Novemba, mwaka alfu mbili kumi na<br />

tatu alipongeza juhudi za Jumuiya ya Afrika<br />

Mashariki kwa kukifanya Kiswahili kuwa<br />

Lingua Franca. Aliongeza kuwa juhudi hizi<br />

ni kati ya mambo muhimu yanayohitajika<br />

iwapo tungependa kuiona Afrika Mashariki<br />

ikiwa na umoja wa aina yoyote ile.<br />

Katika mkutano kama huu uliofanyika<br />

Bujumbura tarehe ishirini na tatu oktoba,<br />

mwaka alfu mbili kumi na tatu, Mheshimiwa<br />

Mike Sebalu alidokeza kuwa ingekuwa<br />

vyema iwapo nchi za Afrika Mashariki<br />

zingeweza kuwa na mpango wa kielimu<br />

ambao ungewawezesha waalimu wa<br />

Kiswahili kufanya kazi katika shule za nchi<br />

hizi ili kuiimarisha lugha yenyewe, hasa<br />

katika nchi yake. Alisema, “Madam speaker,<br />

it would be a good idea to have teachers from<br />

the United Republic of Tanzania crossing<br />

to Uganda to teach.” na kuongeza kuwa<br />

Kiswahili kimetiliwa mkazo katika katiba ya<br />

Uganda, na ni jukumu lao kuhakikisha kuwa<br />

ndoto yao imeonekana. Aliongeza, “We<br />

hope soon, Kiswahili would be introduced in<br />

schools in Uganda to bolster its popularity.”<br />

Kufikia sasa kuna maendeleo<br />

yanayoonyesha juhudi za jumuiya ya Afrika<br />

Mashariki, kama vile kuwepo kwa mitandao<br />

ya kiteknolojia inayotoa huduma kwa lugha<br />

ya Kiswahili: (Microsoft Office 2010 pack.<br />

Windows 7 Kiswahili local language pack)<br />

Ni dhahiri kuwa ili ndoto ya kuwa na<br />

jumuiya yenye nguvu iwe ya kweli, tunahitaji<br />

lugha moja ya mawasiliano kati ya nchi<br />

zetu. Bila shaka, tunakihitaji Kiswahili, na<br />

si kukihitaji tu, bali kukienzi pia. Asilimia<br />

kubwa ya Jamii za Afrika Mashariki ni za<br />

ki-Bantu, hivyo basi haitakuwa vigumu<br />

kwa jamii hizi kukijua Kiswahili kwani lugha<br />

yenyewe ina asili ya ki-Bantu.<br />

Ili jamii hizi ziweze kuienzi lugha hii,<br />

itavibidi vyuo vya Elimu kutilia mkazo<br />

utumizi wake katika Mtaala.<br />

44 • DaystarConnect 2015

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!