our roots
Connect2015
Connect2015
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kuimarishwa na KUTUMIwa<br />
kwa Kiswahili - Hatua Muhimu Ya<br />
Kuhakikisha Umoja Katika Jumuiya<br />
Ya Afrika Mashariki<br />
Na Aron Mtunji<br />
Kwa muda mrefu sasa, wana-Afrika<br />
Mashariki wametamani kuwa na<br />
Uhuru wa kufanya biashara pamoja,<br />
kuzitembelea nchi jirani bila ya<br />
kuwepo kwa vizuizi vyovyote na zaidi ya<br />
hayo, kuona kuwa kuna amani kati ya nchi<br />
husika. Zote hizi ni ndoto zinazoweka kuwa<br />
kweli.<br />
Ili kuwepo na mambo yote haya, kuna<br />
mengi ambayo yamefanywa, yanayotendeka<br />
sasa na yaliyo katika akili za washika dau<br />
katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika<br />
makala haya, nitazungumzia juhudi hizi na<br />
kuwaeleza jinsi kuwepo kwa lugha moja<br />
inayowaunganisha wana-Afrika Mashariki<br />
kutaziwezesha kuwa kweli.<br />
Kwanza kabisa, ili kufanya biashara,<br />
kujihusisha katika siasa au kufanya lolote<br />
lile, ni lazima kuwe na mawasiliano. Ili<br />
yote haya yatendeke, tunahitaji lugha<br />
tutakayoweza kuitumia na kuelewana, tuwe<br />
Uganda, Kenya, Tanzania, Rwanda au katika<br />
nchi yoyote ya Afrika Mashariki.<br />
Moja kati ya juhudi za kufanya hivi<br />
ni kuwepo kwa jumia iliyo na umoja.<br />
Kuvunjika kwa jumuiya ya Afrika Mashariki<br />
mwaka 1977 kulisababisha athari kubwa:<br />
kukosekana kwa ajira, kutokuwa na<br />
uaminifu kati ya nchi husika na kusitishwa<br />
ka uhuru wa wananchi wa nchi hizi<br />
kutembea ndani ya jumuiya. Pia, hakukuwa<br />
na usawa wala uhuru wa kufanya huduma<br />
za pamoja, jambo ambalo liliathiri<br />
uchumi, uhusiano, siasa na zaidi ya hayo…<br />
mawasiliano.<br />
Baada ya kufufuliwa kwa jumuiya hii,<br />
matunda ya kuwepo kwa umoja yalianza<br />
kuonekana, jambo ambalo lilikuwa funzo<br />
kwa nchi wanachama.<br />
Pili, Jumuiya ya Afrika Mashariki<br />
imehakikisha kuwa kuna ‘tume ya Kiswahili<br />
ya Afrika Mashariki.’Lengo kuu la tume<br />
hii ni kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili<br />
imeimarika, kama njia moja ya kuhakikisha<br />
kuwa kuna umoja na urahisi katika<br />
mawasiliano yanayohusisha siasa, shughuli<br />
za kifedha, shughuli za kijamii, za tamaduni,<br />
teknolojia na masomo.<br />
Mkataba uliotiwa sahihi mwaka 1999<br />
uliimarisha uhusiano kati ya nchi husika.<br />
Kipengee muhimu katika mkataba huu<br />
(137) kiliitaja lugha ya Kiswahili kama lingua<br />
franca ya nchi za Afrika Mashariki. Hivyo<br />
basi, lilikuwa jambo muhimu kwa nchi hizi<br />
kuunda baraza au chama ambacho lengo<br />
lake lingekuwa kuhakikisha kuwa lugha ya<br />
Kiswahili imetumiwa kuimarisha umoja,<br />
kuhakikisha kuwa Kiswahili kimetumiwa<br />
kama lugha ya jumuiya na kuhakikisha kuwa<br />
lugha hii imetumiwa katika mawasiliano.<br />
Kisha, mipango ya kuwasaidia walio na<br />
matatizo ya kimawasiliano kwa lugha ya<br />
Kiswahili, kubadilishana kwa waalimu na<br />
wanafunzi wa Kiswahili baina ya shule za<br />
nchi husika na kuzisaidia serikali za nchi hizi<br />
katika juhudi za kuimarisha Kiswahili ni kati<br />
ya ajenda walizokuwa nazo.<br />
Lengo kuu lilikuwa kuwepo kwa vituo<br />
vya utafiti vya Kiswahili katika nchi za Afrika<br />
Mashariki, kuwepo kwa waalimu wa lugha<br />
hii ambao wangeifunza katika vyuo vilivyo<br />
katika nchi hizi na kuleta mabadiliko katika<br />
MTAALA unaotumiwa katika shule za Afrika<br />
mashariki, hasa zile za masomo ya juu kwa<br />
kukifanya Kiswahili kuwa kati ya lugha rasmi<br />
zinazotumiwa.<br />
Kufikia sasa, Marais wan chi za Afrika<br />
Mashariki wameunga mkono hatua hii.<br />
Rais wa Kenya, Mheshimiwa Kenyatta<br />
akiongea katika mkutano wa EALA (East<br />
African Legislative Assembly) tarehe ishirini<br />
na sita Novemba, mwaka alfu mbili kumi na<br />
tatu alipongeza juhudi za Jumuiya ya Afrika<br />
Mashariki kwa kukifanya Kiswahili kuwa<br />
Lingua Franca. Aliongeza kuwa juhudi hizi<br />
ni kati ya mambo muhimu yanayohitajika<br />
iwapo tungependa kuiona Afrika Mashariki<br />
ikiwa na umoja wa aina yoyote ile.<br />
Katika mkutano kama huu uliofanyika<br />
Bujumbura tarehe ishirini na tatu oktoba,<br />
mwaka alfu mbili kumi na tatu, Mheshimiwa<br />
Mike Sebalu alidokeza kuwa ingekuwa<br />
vyema iwapo nchi za Afrika Mashariki<br />
zingeweza kuwa na mpango wa kielimu<br />
ambao ungewawezesha waalimu wa<br />
Kiswahili kufanya kazi katika shule za nchi<br />
hizi ili kuiimarisha lugha yenyewe, hasa<br />
katika nchi yake. Alisema, “Madam speaker,<br />
it would be a good idea to have teachers from<br />
the United Republic of Tanzania crossing<br />
to Uganda to teach.” na kuongeza kuwa<br />
Kiswahili kimetiliwa mkazo katika katiba ya<br />
Uganda, na ni jukumu lao kuhakikisha kuwa<br />
ndoto yao imeonekana. Aliongeza, “We<br />
hope soon, Kiswahili would be introduced in<br />
schools in Uganda to bolster its popularity.”<br />
Kufikia sasa kuna maendeleo<br />
yanayoonyesha juhudi za jumuiya ya Afrika<br />
Mashariki, kama vile kuwepo kwa mitandao<br />
ya kiteknolojia inayotoa huduma kwa lugha<br />
ya Kiswahili: (Microsoft Office 2010 pack.<br />
Windows 7 Kiswahili local language pack)<br />
Ni dhahiri kuwa ili ndoto ya kuwa na<br />
jumuiya yenye nguvu iwe ya kweli, tunahitaji<br />
lugha moja ya mawasiliano kati ya nchi<br />
zetu. Bila shaka, tunakihitaji Kiswahili, na<br />
si kukihitaji tu, bali kukienzi pia. Asilimia<br />
kubwa ya Jamii za Afrika Mashariki ni za<br />
ki-Bantu, hivyo basi haitakuwa vigumu<br />
kwa jamii hizi kukijua Kiswahili kwani lugha<br />
yenyewe ina asili ya ki-Bantu.<br />
Ili jamii hizi ziweze kuienzi lugha hii,<br />
itavibidi vyuo vya Elimu kutilia mkazo<br />
utumizi wake katika Mtaala.<br />
44 • DaystarConnect 2015