Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Magonjwa ya ngono<br />
Magonjwa ya ngono yanaweza kuambukizwa kwa jinsia zote kwa njia ya<br />
kujamiiana.<br />
Magonjwa ya ngono yanaweza kuwa na dalili mbaya, huzuinisha na<br />
isiyoridhisha. Lakini tatizo kubwa kwa magonjwa haya ni kwamba mara<br />
nyingi hayaonyeshi dalili kabisa. Kwa maana hii unaweza kuwa na<br />
maambukizo bila kujua. Kwa hiyo unaweza kuambukizwa na<br />
kuwaambukiza watu wengine, bila kufahamu.<br />
Kama magonjwa ya ngono hayatatibiwa na madawa hospitalini yanaweza<br />
kuleta matatizo makubwa ambayo yatasababisha magonjwa kama kansa,<br />
ugonjwa wa moyo, kuumwa na macho, kuumwa na ubongo, kuumwa na<br />
mifupa, kuumwa na viungo vya mwili, na kutoa mimba. Pia yanaweza<br />
kuleta ugumba (kutopata watoto) na kuharibu kabisa kizazi cha<br />
mwanaume au cha mwanamke.<br />
Kama una ugonjwa ya ngono, au mwenzi wako anayo, ni muhimu kutibiwa<br />
haraka kliniki au hospitalini. Na wale uliojamiiana nao labda<br />
umeshawaambukiza na wasione dalili zozote. Na pia ni muhimu kuwaeleza<br />
wale uliojamiiana nao kuwa umeathirika ili wapate matibabu haraka.<br />
Kama wenzi wako hawakupata matibabu haraka wanaweza<br />
kupata matatizo makubwa kiafya, wanaweza kuambukiza<br />
watu wengine, na wanaweza kukuambukiza wewe tena.<br />
5 KISWAHILI