Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Maa</strong>mbukizi ya VVU<br />
VVU huishi kwenye mwili wa mtu aliyeambukizwa. Virusi huishi kwenye<br />
majimaji yaliyoko kwenye:<br />
1. Shahawa<br />
2. Majimaji ukeni<br />
3. Damu<br />
4. Maziwa ya mama<br />
Kwa hiyo shahawa, majimaji ukeni, damu na maziwa ya mama ni<br />
hatari kuambukiza VVU.<br />
Majimaji mengine mwilini kama mate, machozi, jasho na mkojo havina<br />
virusi vingi vinavyoweza kuambukiza. Kwa hiyo mate, machozi, jasho na<br />
mkojo siyo hatari kwa kuambukiza VVU.<br />
Njia pekee ya kuambukiza VVU ni kutoka kwenye shahawa, majimaji<br />
ukeni, damu au maziwa ya mama ameshaambukizwa na kuingia kwenye<br />
damu ya mtu mwengine.<br />
Njia zifuatazo zinaambukiza VVU:<br />
1. Kujamiiana na mtu mwenye VVU bila kutumia kondom.<br />
Kujamiiana bila kondom ni njia kuu ya kuambukizwa<br />
VVU.<br />
2. Kushirikiana sindano, wembe, visu vya kukata mwili, mswaki na<br />
vyombo vingine vinavyoweza kuwa na damu yenye VVU.<br />
3. Mwanamke anaweza kuambukiza mtoto wake akiwa tumboni,<br />
wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.<br />
9 KISWAHILI