Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
VVU na ukimwi<br />
Ukimwi ni ugonjwa hatari ya ngono. Inasabibishwa na virusi viitwavyo<br />
VVU. VVU inamaana ya ‘virusi vya ukimwi’ (VVU). Virusi hivi hudhuru<br />
mwili polepole na baadaye mwili hushindwa kupambana na magonjwa<br />
mengine. Mwishoni mtu anaweza kufa kwa ajili ya magonjwa<br />
yanayosababbishwa na VVU.<br />
Mtu akiambukizwa anaweza kuchukuwa muda mrefu bila kuelewa<br />
kwamba VVU ipo kwenye mwili wake. VVU ipo kwenye shahawa,<br />
majimaji ukeni, damu na maziwa ya mama aliyeambukizwa. Huwezi<br />
kuelewa kuwa mtu ana VVU mwilini kwa kuangalia kwa macho tu. Njia<br />
pekee ya kuelewa kuwa mtu ameshaambukizwa VVU ni kupima damu<br />
kwenye kliniki au hospitalini.<br />
Ukimwi inamaana kwamba ‘upungufu wa kinga mwilini’. Ukimwi ni<br />
matokeo ya mwisho wa mwili kushindwa kukinga magonjwa. Wa<strong>Maa</strong>sai<br />
hutumia jina ‘biitia’ kama ukimwi. Ni vizuri zaidi kutumia jina ukimwi<br />
kwani bittia ni jina la zamani lakini ukimwi ni ugonjwa mpya (ukimwi<br />
imegundukika 1981).<br />
Kwa sababu watu wengi hawajui kwamba wameshaambukizwa, au wenzi<br />
wao wameambukizwa, hawaendi kupima na hawajikingi wao wenyewe<br />
wala kuwakinga wenzao. Ina maana kwamba mtu anaweza kuambukiza<br />
watu wengi kabla dalili yake kuonekana.<br />
Hakuna tiba wala chanjo ya VVU. Mtu aliye na VVU, virusi vitakaa<br />
mwilini maishani. Siku hizi kuna madawa (ARVs) hospitalini yanayoweza<br />
kupunguza makali ya VVU mwilini na kusaidia kuongeza muda kutoka<br />
kuambukizwa VVU hadi kuwa na dalili ya kuumwa. Lakini madawa haya<br />
hayatibu VVU moja kwa moja. Ni muhimu kukumbuka kuwa VVU ni<br />
virusi hatari sana na inasabibisha matatizo makubwa.<br />
7 KISWAHILI