Kielelezo Patanifu cha Katiba ya Kenya - ConstitutionNet
Kielelezo Patanifu cha Katiba ya Kenya - ConstitutionNet
Kielelezo Patanifu cha Katiba ya Kenya - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
JUMAPILI, NOVEMBA 22, 2009<br />
KIELELEZO PATANIFU CHA KATIBA YA KENYA<br />
Ime<strong>cha</strong>pishwa mnamo Novemba 17, 2009 na Kamati <strong>ya</strong> Wataalam Kuhusu Marekebisho <strong>ya</strong> <strong>Katiba</strong> Kulingana na<br />
Sehemu 32(1)(a)(i) <strong>ya</strong> Sheria <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> <strong>Katiba</strong> <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>, 2008.<br />
39<br />
(ii) kuwapa kazi walimu walioajiriwa na Tume kuhudumu katika<br />
shule yoyote <strong>ya</strong> umma na taasisi nyingine.<br />
(iii) kuwapandisha vyeo na kuwahamisha walimu;<br />
(iv) kuwaadhibu na kuwadhibiti walimu;<br />
(v) kuwafuta kazi walimu; na<br />
(vi) kutekeleza majukumu mengine <strong>ya</strong>liyopewa Tume na Sheria<br />
<strong>ya</strong> Bunge.<br />
(3) Tume itachunguza viwango v<strong>ya</strong> elimu na mafunzo kwa watu wanaojiunga<br />
na taaluma <strong>ya</strong> ualimu na kutoa walimu na itashauri serikali <strong>ya</strong> kitaifa kuhusu<br />
masuala <strong>ya</strong>nayohusiana na taaluma <strong>ya</strong> ualimu.<br />
Sehemu 3 – Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong><br />
Kubuniwa na kudhibitiwa.<br />
278. (1) Kuna Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> iliyobuniwa katika utumishi wa<br />
umma.<br />
(2) Malengo <strong>ya</strong> Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> ni kuhakikisha –<br />
(a) kwamba wafungwa katika magereza nchini wamehifadhiwa salama<br />
na kwamba taasisi hizo zina mazingira <strong>ya</strong>nayofaa binadamu kuishi<br />
kulingana na <strong>Katiba</strong> na sheria;<br />
(b) kuwasimamia wahalifu katika jamii ambao wanahudumu vifungo<br />
v<strong>ya</strong> nje au ambao wanachunguzwa; na<br />
(c) kuwarekebisha wahalifu ili kuwaandaa kurudi na kuishi maisha yenye<br />
manufaa katika jamii.<br />
(3) Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> itakuwa na muundo na kudhibitiwa ili<br />
iweze –<br />
(a) kufikia viwango v<strong>ya</strong> juu v<strong>ya</strong> kitaaluma na nidhamu miongoni mwa<br />
wana<strong>cha</strong>ma wake na kupitia kwa wana<strong>cha</strong>ma hao katika kutekeleza<br />
mamlaka <strong>ya</strong>ke;<br />
(b) kukuza uwajibikaji na kuzuia ufisadi;<br />
(c ) kuzingatia viwango v<strong>ya</strong> haki za binadamu katika kutekeleza mamlaka<br />
<strong>ya</strong>ke na utendakazi wa majukumu <strong>ya</strong>ke; na<br />
(d) kutoa mafunzo kwa wana<strong>cha</strong>ma wake kufikia viwango v<strong>ya</strong> juu v<strong>ya</strong><br />
uwezo wao na kuhusiana na matumizi ma<strong>cha</strong>che <strong>ya</strong> mabavu na kuwa<br />
na uadilifu na kuheshimu haki za binadamu , uhuru wa kimsingi na<br />
heshima <strong>ya</strong> binadamu.<br />
(4) Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> itaandaliwa kuhusisha muundo wa<br />
ugatuzi.<br />
(5) Bunge litatunga sheria -<br />
(a) kubuni miundo <strong>ya</strong> kutosha kuwezesha utawala unaozingatia uwazi<br />
katika Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>;<br />
(b) kuruhusu mpango, usimamizi na utendakazi wa Huduma <strong>ya</strong><br />
Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>; na<br />
(c) kwa jumla kudhibiti Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>.<br />
Mkurugenzi Mkuu<br />
279. (1) Kuna ofisi buniwa <strong>ya</strong> Mkurugenzi –Mkuu wa Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong><br />
Ken<strong>ya</strong>.<br />
(2) Mkurugenzi – Mkuu atateuliwa na Rais wa Kitaifa, kwa ushauri wa Tume<br />
<strong>ya</strong> Utumishi wa umma na baada <strong>ya</strong> kuidhinishwa na Bunge.<br />
(3) Mtu atateuliwa kuwa Mkurugenzi- Mkuu iwapo mtu huyo ana sifa zifaazo<br />
kitaaluma na –<br />
(a) amehudumu katika Huduma <strong>ya</strong> Marekebisho <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> kwa angalau<br />
miaka kumi; au<br />
(b) ana uzoefu mpana katika usimamizi na utendajikazi kuhusu<br />
huduma za marekebisho.<br />
(4) Mkurugenzi-Mkuu atahudumu kwa muhula wa miaka mitano na ataweza<br />
kuteuliwa kwa kipindi kingine <strong>cha</strong> mwisho <strong>cha</strong> miaka mitano.<br />
(5) Kifungu 297 (3) kuhusiana na sifa za kuajiriwa zinazohitajika na Tume<br />
zitazingatiwa katika kumwajiri Mkurugenzi-Mkuu.<br />
SURA YA KUMI NA SABA<br />
Sehemu 1- Taasisi za Usalama wa Taifa<br />
Kanuni na misimamo<br />
280. (1) Usalama wa Taifa ni ulinzi wa mipaka <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>, watu wake, mali <strong>ya</strong>o,haki<br />
na uhuru, na maslahi mengine <strong>ya</strong> kitaifa dhidi <strong>ya</strong> vitisho v<strong>ya</strong> ndani na nje.<br />
(2) Usalama wa taifa la Ken<strong>ya</strong> utaimarishwa na kuhakikishwa kulingana na<br />
kanuni zifuatazo –<br />
(a) usalama wa taifa unaongozwa na mamlaka <strong>ya</strong> <strong>Katiba</strong> hii na Bunge;<br />
(b) Usalama wa taifa utatekelezwa kwa kuzingatia sheria, ikiwemo<br />
sheria <strong>ya</strong> kimataifa, na kwa kuheshimu kikamilifu utawala wa kisheria,<br />
demokrasia, haki za binadamu na uhuru wa kimsingi;<br />
(c) taasisi za usalama wa kitaifa zitaheshimu tamaduni mbalimbali za<br />
jamii nchini Ken<strong>ya</strong> katika kutekeleza majukumu <strong>ya</strong>ke; na<br />
(d) uajiri katika taasisi za usalama wa taifa utaakisi mseto wa watu wa<br />
Ken<strong>ya</strong> katika viwango sawa.<br />
Taasisi za usalama wa taifa<br />
281. (1) Taasisi za usalama wa taifa ni -<br />
(a) Vikosi v<strong>ya</strong> Ulinzi wa Ken<strong>ya</strong>;<br />
(b) Huduma za Taifa za Upelelezi; na<br />
(c) Huduma <strong>ya</strong> Polisi wa Ken<strong>ya</strong>.<br />
(2) Lengo la kimsingi la taasisi za usalama wa taifa na mfumo wa usalama ni<br />
kulinda maslahi <strong>ya</strong> watu wa Ken<strong>ya</strong> na mali <strong>ya</strong>o na haki na uhuru, na mamlaka<br />
, amani, umoja wa kitaifa na mipaka <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>.<br />
(3) Katika utekelezaji wa majukumu <strong>ya</strong>o, taasisi za usalama wa taifa na kila,<br />
mwana<strong>cha</strong>ma wa taasisi hizo hataruhusiwa -<br />
(a) kuwa na upendeleo kwa njia yoyote,<br />
(b) kuendeleza maslahi <strong>ya</strong> <strong>cha</strong>ma chochote <strong>cha</strong> kisiasa wala sera zake;<br />
(c) kuhujumu maslahi <strong>ya</strong> kisiasa au mpango wa kisiasa ambao ni halali<br />
chini <strong>ya</strong> <strong>Katiba</strong> hii; au<br />
(d) kutii amri yoyote isiyokuwa halali.<br />
(4) Mtu hataruhusiwa kubuni shirika linalohusiana na usalama wa taifa au<br />
shirika wa kijeshi isipokuwa inavyoruhusiwa na <strong>Katiba</strong> hii au Sheria <strong>ya</strong> Bunge.<br />
(5) Taasisi za uslama wa taifa zitakuwa chini <strong>ya</strong> mamlaka <strong>ya</strong> raia.<br />
(6) Bunge litatunga sheria kuruhusu kushughulikia majukumu, utaratibu na<br />
usimamizi wa taasisi za usalama wa taifa.<br />
Kubuniwa kwa Baraza la Usalama wa Taifa<br />
282. (1) Kuna Baraza buniwa la Usalama wa Taifa lenye –<br />
(a) rais wa taifa<br />
(b) Naibu Rais wa taifa;<br />
(c) Waziri Mkuu,<br />
(d) Waziri anayehusika na ulinzi;<br />
(e) Waziri anayehusika na mashauri <strong>ya</strong> kigeni;<br />
(f) Waziri anayehusika na usalama wa taifa;<br />
(g) Mwanasheria Mkuu<br />
(h) Mkuu wa Majeshi <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>;<br />
(i) Mkurugenzi –Mkuu wa Huduma <strong>ya</strong> Kitaifa <strong>ya</strong> Upelelezi; na<br />
(j) Inspekta-Mkuu wa Huduma <strong>ya</strong> Polisi <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>.<br />
Majukumu <strong>ya</strong> Baraza la Usalama wa Taifa<br />
283. (1) Baraza la Usalama wa Taifa –<br />
(a) Litaunganisha sera za humu nchini, za kigeni na za kijeshi kuhusiana<br />
na usalama wa kitaifa ili kuwezesha taasisi za usalama wa taifa<br />
kushirikiana kikamilifu;<br />
(b) kutathmini na kuchunguza malengo, kujitolea ,na hatari kwa Taifa<br />
kuhusiana na usalama wa nchi; na<br />
(c) kuanzisha sera kuhusu masuala <strong>ya</strong> maslahi <strong>ya</strong> pamoja <strong>ya</strong> kiusalama<br />
<strong>ya</strong> taasisi za kiusalama na kudhibiti taasisi hizo.<br />
(2) Baraza la Usalama wa Taifa litatoa ripoti kwa Bunge kila mwaka kuhusiana<br />
na hali <strong>ya</strong> usalama nchini Ken<strong>ya</strong>.<br />
(3) Baraza la Usalama wa Taifa linaweza kwa idhini <strong>ya</strong> Bunge –<br />
(a)kupeleka wanajeshi nje <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong> kwa minajili <strong>ya</strong> –<br />
(i)kutekeleza majukumu <strong>ya</strong> Umoja wa Mataifa <strong>ya</strong> kudumisha amani<br />
pamoja na majukumu mengine; au<br />
(ii) kuidhinisha wanajeshi wa kigeni kutumwa Ken<strong>ya</strong>.<br />
Sehemu 2 - Majeshi <strong>ya</strong> Ulinzi wa Ken<strong>ya</strong><br />
Kubuniwa kwa Vikosi v<strong>ya</strong> Ulinzi wa Ken<strong>ya</strong> na Baraza la Ulinzi<br />
284. (1) Kuna vikosi buniwa v<strong>ya</strong> Ulinzi wa Ken<strong>ya</strong> vinavyohusisha –<br />
(a) Ken<strong>ya</strong> Army;<br />
(b) Ken<strong>ya</strong> Air Force; na<br />
(c) Ken<strong>ya</strong> Navy.<br />
(2) Mtu hatabuni kikosi <strong>cha</strong> majeshi au kundi lenye hadhi <strong>ya</strong> kijeshi isipokuwa<br />
inavyoruhusiwa katika <strong>Katiba</strong> hii.<br />
(3) Kuna Baraza la Ulinzi lililobuniwa linalohusisha –<br />
(a) Waziri anayehusika na ulinzi ambaye atakuwa mwenyekiti;<br />
(b)Naibu Waziri anayehusika na ulinzi ambaye atakuwa naibu<br />
mwenyekiti;<br />
(c )Mkuu wa Majeshi <strong>ya</strong> Ken<strong>ya</strong>;<br />
<strong>Katiba</strong> mp<strong>ya</strong>, Ken<strong>ya</strong> Moja