08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Seyyid Sheikh


Mtungaji:-<br />

Swahib Sujjada:<br />

Sheikh Salim Bin Mbarak (Dar-wesh – Mti mkavu)<br />

P. O. Box 8105,<br />

Zawia kuu – Arusha,<br />

Tanzania. (E.A).<br />

i.


Swahib Sujjada,<br />

<strong>Al</strong> habib Sheikh Salim Bin Mbarak.<br />

(Dar-wesh Mti Mkavu).<br />

ii.


Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan<br />

(Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz).<br />

First Addition Toleo la kwanza<br />

iii.


Swahib Sujjada:<br />

<strong>Al</strong> Habib Sheikh Salim Mbarak<br />

(Mti - Mkavu).<br />

iv.


Yaliyomo:<br />

No. Ukurasa.<br />

1. Dibaji……………………………………….. vi.<br />

2. Utangulizi…………………………………... vii.<br />

3. Jina lake la kuzaliwa……………………….. 1.<br />

4. Nasabu yake..………………………………. 2.<br />

5. Makuzi yake na kusoma Qur an.………........ 2.<br />

6. Kutafuta Ilmu ……………………………… 3.<br />

7. Masheikh zake…………………………….. 4.<br />

8. Umaarufu wake kwa kusoma……………… 5.<br />

9 Kusomesha kwake Ilmu……………..…….. 7.<br />

10. Namna ya Twariqa ilvyoenea….………….. 8.<br />

11. Siri ya Ilmu ya Tasawfu ..………………..... 10.<br />

12. Sifa za Seyyid Abdul Qadir…..…………… 11.<br />

13. Wake zake na watoto wake……………….. 12.<br />

14. Wasia wake kwa mwanawe A`bdul Razaq.. 13.<br />

15. Karama zake……………............................ 13.<br />

16. Kifo cha Seyyid Abdul Qadir Jaylani (Qsa).. 27.<br />

v.


DIBAJI:<br />

Sifa zote njema zinamstahiki ALLAH ambaye<br />

amefundisha kwa wasta wa kalamu. Na akamfundisha Mwana<br />

Adam lile asilolijua. Na Rehma na Amani Zimwendee Bwana<br />

Mtume Saw na Ahly zake watukufu na Maswahaba wake watiifu.<br />

Kwa ridhaa ya mtunzi wa kitabu hiki ambae ni kiongozi<br />

mkuu na Mlezi wa Twariqatul-Qadiriya– Rrazziqiya–Jaylaniya <strong>Al</strong><br />

habib Sheikh Salim ibn Mbarak –(Dar-weish Mti mkavu) –<br />

(Radhia ALLAH Anhu). Naandika Dibaji ya kitabu hiki kwa<br />

munassaba wa kuya yakinisha yaliyomo kwenye kitabu hiki.<br />

Kwa hakika kitabu hiki kimeelezea historia na sifa kadhaa<br />

za Bwana wa Mawalii Seyyid Sheikh Abdul-Qadiri- Jaylani<br />

(Qada-sa-Llahu-Siral-Aziz)<br />

Basi ukiwa utajaaliwa kusoma kitabu hiki utamjua vilivyo<br />

alivyo Walii wa Mwenyezi Mungu na Uasili wa Twariqa kwa<br />

ujumla.<br />

Insha-<strong>Al</strong>lah tunamuomba <strong>Al</strong>lah amjaalie kila la kheri mtunzi<br />

wa kitabu hiki Sheikh Salim amjaalie Mahaba zaidi ya kudarisisha<br />

hususan kwa kutunga vitabu vingi zaidi vitavyotoa Ilmu na<br />

muongozo wa ibada za Kitwariqa kwa misingi ya Kitassawfu.<br />

Aamiin Aamiin Aamiin wal-hamdulillahi Rabbil-A`alamiin<br />

Khalifa Mohamed Omar.<br />

Mwenyekiti wa Twariqatul-Qadiriya-Rrazziqiya-<strong>Al</strong>-Jaylaniya<br />

Makao Makuu Ya Twariqa – Zawiya Kuu<br />

S.L.P. 8105<br />

Arusha.<br />

Tanzania (E.A)<br />

vi.


UTANGULIZI:<br />

“Assalamu alay–kum warah–matullahi –Taala wabarakatuh”.<br />

Namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kunijaalia fikra<br />

na utashi wa kuandika kitabu hiki nilichokitambulisha kwa jina la<br />

Ghawth–l–A`adham, Seyyid Sheikh – Abdul – Qadir-Jaylani.<br />

(Qad-sa-Llahu-Siral-A`ziz)<br />

Makusudio yangu makubwa katika kuandika kitabu hiki ni<br />

kuelezea sifa na mwenendo wa maisha ya Bwana wa Mawalii na<br />

kipenzi cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume (Saw).<br />

Ni Matarajio yetu Historia hii tuliyoiandika ndani ya kitabu<br />

hiki itahifadhika na kujenga kumbukumbu juu ya maisha ya watu<br />

wema kwa ujumla. Kuwakumbuka watu wema na kufuatisha<br />

matendo mema ni ufunguo wa kheri hapa duniani na Akhera.<br />

Insha <strong>Al</strong>lah Mwenyezi Mungu amjaalie kila la kheri msomaji<br />

wa kitabu hiki na amjaalie kuwa na matendo mema.<br />

“Eee Mwenyezi Mungu tujaalie sote<br />

mwishilio mwema na utujaalie kuwa<br />

watu wa peponi”<br />

(Aamiin).<br />

Sheikh Salim Ibn Mbarak – (Dar-weish – Mti Mkavu).<br />

S.L.P 8105<br />

Zawiya Kuu – Arusha.<br />

Tanzania (E.A).<br />

vii.


viii.


i. Maisha ya Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />

Seyyid Abdul Qadir ni Muajemi. Naye ni mashuhuri si<br />

katika Ardhi tu, bali hata Mbinguni pia. Yeye ni Sheikh wa<br />

Waislam na ni kiigizo kwa Mawalii na watu wema. Seyyid Abdul<br />

Qadir alikuwa Imamu wa Siddikin na A`arifiyn.<br />

Sharafu yake kwa Mawalii wenzake ni kama Sharafu ya<br />

Nabii Muhammad kwa Mitume wenzake.<br />

ii. Kuzaliwa kwake:<br />

Seyyid Abdul Qadir alizaliwa katika kijiji cha Jeilan huko<br />

Iraq. <strong>Al</strong>izaliwa usiku wa kuamkia Mwezi mosi wa Ramadhani<br />

mwaka 470. A.H.<br />

Bi Fatma alichukua mimba ya mtoto huyo na hali ya kuwa<br />

umri wake ni miaka 60. Wakati ambao hapana tamaa ya kupata<br />

mtoto yeyote.<br />

Siku hiyo aliyomzaa Seyyid Abdul Qadir ilizagaa Nuru<br />

ambayo ilitapakaa kijiji kizima. Mambo hayakuwa hayo tu, lakini<br />

hapakuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuuangalia uso wake kwa<br />

mng‟aro na haiba yake.<br />

Tabia zake zafanana na zile za Seyydina Muhammad<br />

(Saw). Uzuri wake ni ule kama wa Nabii Yusuf (A.s). Ukweli wake<br />

unalingana na Seyyidna Abu-Bakar. (R.a) Haki yake ni kama ile ya<br />

Seyyidna Omar (R.a), na upole wake wa Seyyidna Othman. (Ra).<br />

iii. (a) Nasabu yake kwa kuumeni<br />

Yeye ni Seyyid Abdul Qadir bin Mussa bin Abdillah<br />

1.


in Yahya bin Muhammad bin Daudi bin Mussa bin Abdillah Bin<br />

Mussa bin Abdillahi bin Hassan bin Seyyid Hassan bin <strong>Al</strong>ly bin<br />

Abi Talib. Yaani nduguye Mtume (Saw).<br />

(b). Nasabu yake kwa kukeni.<br />

Yeye ni mtoto wa Bi Fatma Bint Seyyid Abdillah Sawmaiy<br />

Bin Seyyid Mahmoud bin Issa Bin Muhammad Bin <strong>Al</strong>i Bin Mussa<br />

Bin Jaafari Swadiq Bin Muhammad Bin Seyyidna Hussein Bin<br />

<strong>Al</strong>ly Bin Abi Talib.<br />

Unapoangalia nasabu zake zote yaani kukeni na kuumeni, utaona<br />

kama zimekutana kwa Seyyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib; yaani nduguye<br />

Mtume (Saw).<br />

iv. Kukua kwake na kusoma Qur ani<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa akikua na akiishi katika hali<br />

nzuri. Mji wake uliingia neema kubwa kabisa baada ya kuzaliwa<br />

kwake. Seyyid Abdul Qadir alipewa Uwalii na hali ya kuwa ni<br />

mtoto kama Nabii Isa alivyopata Utume katika hali hiyo hiyo.<br />

Ishara zilizoonyesha kama yeye ni Walii ni nyingi na katika<br />

hizo ni:-<br />

(i) Kutamka „Hatifu‟ maneno siku ya mwanzo<br />

alipopelekwa chuoni kusoma Qur an. Maneno<br />

yenyewe ni haya “Mfanyieni nafasi ya kukaaWalii wa<br />

Mwenyezi Mungu”.<br />

(ii) Kusifiwa kwake na „Abdal‟ kwa kusema: “Mtoto<br />

2.


huyu atakuwa na mambo matukufu<br />

atakayosifiwa mwishoni kwake”.<br />

(iii). Bishara ya Mtume aliyompa Baba yake<br />

usingizini - “kwamba atamzaa mtoto ambaye<br />

atakuwa na mambo matukufu atakayosifiwa<br />

mwishoni kwake”.<br />

v. Kutafuta Ilmu:<br />

Seyyid Abdul Qadir alipotimia miaka 18, alimwomba<br />

ruhusa mama yake kusafiri kwa kutafuta Ilmu ambayo ni wajibu<br />

kwa kila Mwislamu mwanamke na mwanaume. <strong>Al</strong>iondoka kwenda<br />

Baghdad pamoja na Nabii Khidhri. Lakini kabla ya kuingia ndani<br />

ya Mji wa Baghdad; Nabii Khidhri alimpa Seyyid Abdul Qadir<br />

sharti ambalo atakapolitekeleza ndipo atapompeleka kwa Masheikh<br />

kusoma. Sharti yenyewe ni kukaa pale nje ya mji na kufanya ibada<br />

kwa muda wa miaka mitatu kamili. Seyyid Abdul Qadir alikubali.<br />

Tangu siku ile Nabii Khidhri hakupapita tena mpaka mwaka<br />

ukamalizika.<br />

Baada ya kutimia mwaka mmoja, Nabii Khidhri alikwenda<br />

kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Seyyid Abdul Qadir alipomwona<br />

Nabii Khidhri alimsimamia. Lakini Nabii Khidhri alikataa<br />

kunyanyukiwa na kumwambia akae kitako.<br />

Siri ya kuwekwa Seyyid Abdul Qadir peke yake kwa<br />

muda wote ule, apate kuitakasa roho yake na ile sehemu<br />

inayoharibiwa na Shetani. Vitisho alivyokuwa akivipata mahala<br />

pale havikuwa na mfano. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda Walii<br />

wake na akamhifadhi na kila baya na vitisho. Ulipotimia mwaka<br />

wa tatu. Nabii Khidhri alikwenda mahala pale kwa ajili ya<br />

kumchukua Seyyid Abdul Qadir.<br />

3.


Juu ya kuwa wamo ndani ya safari pamoja, Seyyid Abdul<br />

Qadir kabisa alikuwa hamjui mtu anayefuatana naye. Lakini alikuja<br />

kumjua baadaye hapo alipokwenda Baghdad kumkagua.<br />

Seyyid Abdul Qadir alisoma kwa juhudi na ari kubwa na<br />

aliwashinda wenzake wote kwa Ilmu na ufasaha wa lugha. Na<br />

alikuwa jogoo mkubwa wa Madhehebu ya Shafi na Hambali. Na<br />

alikuwa akijibu na akifutu masuali kwa Madhehebu hayo mawili.<br />

Lakini yeye mwenyewe alikuwa akifuata madhehebu ya Hambal.<br />

vi. Katika baadhi ya Ilmu alizosoma.<br />

(i) Qur an (Tafsiri)<br />

(ii) Fiqh<br />

(iii) Hadith<br />

(iv) Usuli-fiq<br />

(v) Tarikh (historia)<br />

(vi) Tasawuf<br />

(vii) Lugha. n.k.<br />

vii. Masheikh zake:<br />

Seyyid Abdul Qadir amesoma Ilmu kwa Masheikh wengi<br />

na kila mmoja katabahari katika fanni mbalimbali. Masheikh<br />

wenyewe ni:-<br />

1 Sheikh Abdil-Wafa <strong>Al</strong>i Bin Ukayl.<br />

2. Sheikh Abi Said-al-Mubaraq.<br />

3. Sheikh Abdil Khatib Mahfudh<br />

Kaludhany.<br />

4.


4. Sheikh Abi – Hassan Muhammad.<br />

5. Sheikh Kadhi Abi Said.<br />

6. Sheikh Yahya Bin <strong>Al</strong>i.<br />

7. Sheikh Abi Ghalib Muhhamad bin Abdul<br />

Karim.<br />

8 Sheikh Abu Said Muhammad bin Abdul<br />

Karim.<br />

9. Sheikh Muhammed bin Muhammed<br />

10 Sheikh Abubakar Ahmed bin Ahmed<br />

11. Sheikh Abu Jafar bin Ahmed<br />

12. Sheikh Abu Kassim <strong>Al</strong>i bin Ahmed<br />

13. Sheikh Abu Talibu Abdul Kadir bin<br />

Muhammad<br />

14. Sheikh Abdul Rahman bin Yusuf.<br />

15. Sheikh Abdul Rahaman bin Ahmed<br />

16. Sheikh Abu - Barakat Hibatullah<br />

17. Sheikh Abdul-Izzi Muhammed bi<br />

Mukhtar.<br />

18 Sheikh Abu – Nasri Muhammed<br />

19. Sheikh Abu – Ghalib Ahmad<br />

20. Sheikh Abu – Abdalla Yahya<br />

21. Sheikh Abu – Hassan Mubarak<br />

22. Sheikh Mansur Abdul Rahman<br />

23. Sheikh Abu Barakat Taibat Akuly.<br />

viii. Umaarufu wake kwa kusoma<br />

Sifa za Seyyid Abdul Qadir zilizagaa kwa Ilmu yake.<br />

Ingawa wengi walifurahi kwa mambo hayo, lakini mahasidi wake<br />

walikuwa wakikereka - Nao ni katika nafsi ya wanachuoni<br />

wenzake.<br />

Siku moja walimjia wanachuoni 100 wakati alipokuwa<br />

akisomesha ili kumhoji. Na kila mmoja katika hao alikuwa na<br />

suala mbalimbali, na muradi wao ashindwe ili afedheheke.<br />

5.


Wakati huo watapata kueneza kama hajui kitu kuliko wao. Mara tu<br />

wale wanachuoni walipofika pale walikaa kitako kumsikiliza.<br />

Baada ya kukaa, Seyyid Abdul Qadir alikiimanisha kichwa chake.<br />

Na wakati huo lilimtoka pande la Nuru kifuani mwake<br />

likanyakuwa yote waliyoyadhibiti katika vifua vyao. Mara wakawa<br />

wanababaika na kuwayawaya, huku wanapiga makelele wakirarua<br />

nguo zao mfano wa wenda wazimu. Wote walivua vilemba vyao na<br />

wakamwendea Sheikh pale alipokaa. Kila mtu alikuwa akinyanyua<br />

mguu wa Seyyid Abdul Qadir na kujiwekea kichwani kwake. Hii<br />

ni ishara kuonyesha kama wameridhika na kukinai kuwa ni<br />

Mwanachuoni na amewazidi. Na kila mtu alipokuwa akifanya hayo<br />

yeye alikuwa akimkumbatia.<br />

Waliporudi vikaoni mwao, yote waliyokuwa wameyasahau<br />

wakayakumbuka tena. Seyyid Abdul Qadir alimwambia kila mtu<br />

suala aliyokusudia kuuliza na akampa jawabu nzuri ambayo hata<br />

yeye mwenyewe hakufikiria. Wote walistaajabu na walimpa heko.<br />

ix. Muda wa kutoa waadhi<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitoa waadhi mara tatu kila<br />

wiki kwa muda wa miaka 40. Masheikh, Mafaqih na wanachuoni<br />

wengi wa Baghdad walikuwa wakimiminika kumsikiliza waadhi<br />

wake.<br />

Naam, Katika jumla ya wasikilizaji wa waadhi; Mayahudi<br />

na Manasara walikuwamo.<br />

Taathira kubwa ilipatikana kila waadhi aliokuwa akiutoa<br />

kwani Mayahudi na Manasara wengi kabisa walisilimu. Na<br />

miongoni mwa Waislamu wengi wafanyao maasi walitubu katika<br />

maasi yao.<br />

6.


Ama masomesho yake yalizidi kupatia utukufu. Kwani Bibi<br />

mmoja alijitolea nafsi yake aolewe na Seyyid Abdul Qadir bila<br />

mahari yoyote, isipokuwa alimpa sharti moja, nayo ni<br />

kuwasomosha watu Ilmu kwa muda maalum. Muda ulipotimia,<br />

Bibi yule aliolewa kama alivyotamani.<br />

X. Kusomesha kwake Ilmu:<br />

Katika chuo chake, Seyyid Abdul Qadir alikuwa<br />

akisomesha Ilmu 13 za sheria. Na katika Ilmu hizo 13, aliweka<br />

darsa moja kusomesha Madhehebu mbalimbali na darsa nyinginezo<br />

alikuwa akisomesha Hitilafu za Wanachuoni. Baada ya sala ya<br />

<strong>Al</strong>fajiri, alikuwa akisomesha Tafsir ya Qur an na akisomesha<br />

Hadithi za Mtume (Saw) Darsa hizo zilikuwa zikisomwa na kila<br />

mtu aliyetaka. Ama Ilmu za Madhehebu mbalimbali, Khitilafu za<br />

Wanachuoni, Adabu, Fiq na Usuli Dini zilikuwa zikismwa na<br />

Mawalii tu.<br />

Wakati wa Adhuhuri, ilikuwa ikisomwa Qur an kwa Kiraa<br />

(visomo) 7. Darsa ilikuwa ikihudhuriwa na wanafunzi 650<br />

waliokuwa mahodari sana. Wasomaji wake wakubwa wa Qur ani<br />

walikuwa Sheikh Masoud al Hashimiy na Sheikh Abdul Wahab bin<br />

Abdul Qadir (mwanawe).<br />

xi. Kufutu kwake masuala<br />

Katika fatwa zake, Sheikh alikuwa halazi suala wala<br />

alikuwa hafikiri, Bali alikuwa hanafutu mara moja tu. Kabla ya<br />

kufutu au kujibu suala yoyote, ilikuwa ikisomwa Qur an. Jawabu<br />

zake zilikuwa ama za kuandika au za mdomo. Na jawabu zake<br />

zilikuwa zikiwafurahisha watu kwa ustadi wake.<br />

7.


xii. Namna ya Twariqa ilivyoenea<br />

Asili ya Twariqa inatokea kwa Mwenyezi Mungu. Yeye<br />

akamfundisha Seyyidna Jibril As, na Seyyidna Jibril akamfundisha<br />

Seyyidna Muhammad (Saw), tena Nabii Muhammad akamfundisha<br />

Seyyidna <strong>Al</strong>i (R.a) Baadaye ikaendelea kwa Masheikh hawa hata<br />

nao wakaifikisha hapa Tanzania na mwenginepo:-<br />

1. Seyyidna Hassan al Busry.<br />

2. Seyyidna Arif Samdany<br />

3. <strong>Al</strong>habibul Ajemy.<br />

4. Daud Taiy<br />

5. Maaruf al Karkhy.<br />

6. Sharif Sakaty<br />

7. Abi Kasim al Juneid<br />

8. Abu Bakar Shily<br />

9. Abu Fadhi Abdul Wahid<br />

10. Abu Faraj Tusy<br />

11. Seyyidna Abdul Hassan<br />

12. Seyyidna Abu Said –al – Makhzumy.<br />

13. Seyyid Abdul Kadir al Jeilany na kadhalika.<br />

xiii. Siri ya Ilmu ya Twariqa<br />

Ilmu ya twariqa imefanywa kwa Qur an na Hadithi za<br />

Mtume (Saw) pamoja na mambo yafuatayo:-<br />

(i) Kusafisha moyo<br />

(ii) Ukarimu<br />

(iii) Ustahamilivu<br />

(iv) Kuwasamehe waliokuudhi<br />

(v) Kuacha au kujiepusha na maasi<br />

(vi) Kufanya Ibaada kwa jitihada.<br />

8.<br />

.


Faida. i.<br />

Hizi Twariqa ziko namna nyingi, nazo zinapata kama 17.<br />

Katika hizo ni Qadiry, Shadhily, Nakshahabandy, Indarusy<br />

n.k.<br />

Ama Twariqa yoyote akiifuata mtu kama<br />

inavyohitajia, basi itaweza kumfikisha kwa Mwenyezi<br />

Mungu. Kwani lengo lao ni moja tu lakini kwa yote hayo<br />

niliyoeleza inapasa kupatikana Sheikh Mwongofu wa<br />

kukupa „Ijaza‟ na kukufundisha njia za kupita na kukupa<br />

wasia. Huyu mtu anayepewa „Ijaza‟ na Sheikh huitwa<br />

„Muridi‟ Kwa hivyo kila Murid ajitahidi sana kutekeleza<br />

ahadi atakazopewa na Sheikh wake.<br />

Faida ii.<br />

Yatakiwayo kwa Muridi<br />

1. Kutubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />

2. Kufanya Ibaada kiasi ya uwezo wake.<br />

3. Kufanya mambo yalio halali<br />

4. Kuacha mambo yaliyo haramu.<br />

5. Kumdhukuru Mungu<br />

6. Kushikamamna na “Laa ila ha illa Llah” hasa baada<br />

ya kila Sala mara 165 na wakati mwngine kiasi ya<br />

kuweza kwake.<br />

7. Kusoma sana Qur an kwa kila hali.<br />

8. Kuwasamehe wenye kukuudhi.<br />

9. Kuwa mstahamilivu.<br />

10. Kuwa karimu<br />

11. Kuacha husda, kijicho, choyo, uwongo wa<br />

kuwasengenya watu.<br />

12. Kudumu na udhu.<br />

13. Kumsalia Mtume (S.a.w) kwa wingi.<br />

9.


xiv. Siri ya Ilmu ya tasawuf:<br />

Ilmu ya Tasawfu imefanywa kwa mambo yafuatayo:-<br />

Faida:-<br />

(i) Ukarimu.<br />

(ii) Kuridhia hukumu ya Mungu.<br />

(iii) Subira<br />

(iv) Ishara<br />

(v) Upweke<br />

(vi) Kuvaa nguo za sufi<br />

(vii) Kwenda sana<br />

(viii) Umaskini.<br />

Katika hizo sifa nane zilizotajwa hapo juu, zimechukuliwa<br />

kutokana na Mitume wanane mbalimbali:-<br />

1. Ukarimu: Ilikuwa sifa kubwa sana ya Nabii Ibrahim<br />

(Asw).<br />

2. Ridhaa: (kuridhia), ni sifa ya Nabii Is-haq. (As).<br />

3. Subra: Ni sifa ya Nabii Ayub, (A.s)<br />

4. Ishara: Ni sifa ya Nabii Zakaria (A.s)<br />

5. Sufi: Ni kivazi cha Nabii Yahya (A.s)<br />

6. Upweke: Ni sifa ya Nabii Yusufu (A.s)<br />

7. Kwenda : Ni sifa ya Nabii Issa, (As) na ndio maana<br />

akaitwa „Masihi‟<br />

8. Umaskini: Ni sifa ya Nabii Muhammad (Saw).<br />

10.


xv. Sifa za Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa karim sana na mwenye sifa na<br />

tabia nzuri za kupigiwa mfano. <strong>Al</strong>ikuwa na kimo cha wastani, si<br />

mrefu sana wa kuchusha wala hakuwa mfupi. <strong>Al</strong>ikuwa mwekundu<br />

wa weupe. <strong>Al</strong>ikuwa na nyusi nzuri sana. Mwili wake ulikuwa<br />

mwembamba, macho yake yalikuwa yenye haiba kubwa. Kifua<br />

chake kilikuwa kipana chenye Ilmu nyingi. <strong>Al</strong>ikuwa mkali kama<br />

babu yake Sayyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib. Ama ndevu zake zilikua<br />

ndefu namna zile za Nabii Harun (As).<br />

Seyyid Abdul Qadir alikua na cheo au makamo matukufu<br />

mbelel ya Mwenyezi Mungu. Katika Ulimwengu alikuwa ni mtu<br />

mwenye kusikilizwa sana sauti. Sauti yake iliokuwa nzuri na<br />

nyororo kama lulu. Anaposema husema upesi upesi. Hakupata<br />

kupenga makamasi wala kutema makohozi. Mwisho inzi hakupata<br />

kumtua juu ya mwili wake.<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa mnyenyekvu na mkweli.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa na kawaida ya kumtolea mtu salamu mwanzo kila<br />

wanapokutana naye.<br />

Aidha alikuwa akikaa na maskini kama alivyokuwa<br />

akifanya Nabii Muhammad (Saw). Pamoja na utukufu aliokuwa<br />

nao, alikuwa akiwasimamia watoto wadogo na alikuwa<br />

akiwatukuza watu wazima kama ilivyokuwa ada yake Mtume<br />

(Saw). Ingawa alikuwa akiwasimamia watoto lakini hakupata<br />

kumsimamia mtu yeyote katika watu watukufu.<br />

Seyyid Abdul Qadir hakupata kugonga mlango wa<br />

Mfalme au waziri yeyote kwa kumtaka haja ya kilimwengu.<br />

Kazi yake ilikuwa ni kuamrisha mema na kukataza maovu.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa akila na wageni na marafiki zake.<br />

Kadhalika alikuwa akiwapa nguo na chakula maskini.<br />

Vile vile alikuwa akiwapa zawadi nzuri nzuri wanapomwendea<br />

kwake. Kwa ukarimu wake hakupata kumrejesha mtu yeyote<br />

aliyemwomba wakati wa shida, seuze wakati wa raha.<br />

11.


Mavazi yake yalikuwa ya fahari, kama mavazi ya kifalme. Mavazi<br />

hayo aliyavaa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.<br />

Siku moja alipita mtu mwenye haja na akavua nguo hizo<br />

akampa yeye. <strong>Al</strong>itoa Joho ambalo thamani yake yadi moja ni<br />

Dinari 20; yaani Sh. 240/-<strong>Al</strong>itoa na kilemba ambacho thamanai<br />

yake ni Dinari 70,000 yaani sh. 840,000/- .<br />

xvi. Wake zake<br />

Seyyid Abdul Qadir hapo mwanzoni mwake alikaaa muda<br />

mrefu sana bila ya kuoa. <strong>Al</strong>ikaa muda mrefu kwa Ibaada na<br />

alichelea kuvaana na mambo ya ndoa asije akashughulika na<br />

akapunguza Ibaada zake kwa mshughuliko wa wakeze. Siku moja<br />

aliendewa na Mtume(Saw) akamwambia aoe. Kwa kupata nasaha<br />

hiyo ndipo alipooa, na alioa wake wanne.<br />

xvii Watoto wake:<br />

Watoto aliozaa Seyyid Abdul Qadir ni 49. Katika hao 27<br />

walikuwa watoto wanaume na 22 walikuwa wanawake.<br />

Hawa wafuatao ni miongoni mwa hao watoto wa kiume wa<br />

Seyyid Abdul Qadir aliowaacha baada ya kufa:-<br />

1. Sheikh Abdul Wahab<br />

2. Sheikh Abdul Razak<br />

3. Sheikh Abdul Aziz<br />

4. Sheikh Abdul Jabbar<br />

5. Sheikh Abdul Ghafur<br />

6. Sheikh Abdul Ghina<br />

12.


Faida:-<br />

Sayyid Abdul Qadir alipokuwa akiumwa siki moja aliwahi<br />

kuzimia. Wakawa wanawe na wakeze wanalia, Mara tu baada ya<br />

kupata fahamu, alisema, “Msilie nitapona, kwani mgongoni<br />

mwangu bado yuko mtoto mmoja Yahya” wale watu walidhania ati<br />

maneno ya kigonjwa. Kumbe ni ya kizima. Kwani alipona katika<br />

ule ugonjwa, na alimzaa huyo Yahya kama alivyosema. Mtoto<br />

huyo alimpata kwa Suria wake Halima. Mtoto huyo ndiye<br />

aliyekuwa kitinda-Mimba.<br />

xviii Wasia wake juu ya mwanawe, Abdul-Razak.<br />

1. Kumcha Mungu.<br />

2. Kumtii Mungu.<br />

3. Kufuata sharia<br />

4. Kuhifadhi mipaka ya Mungu<br />

5. Kuwatunza na kuwarehemu mafukara<br />

6. Kuwatukuza Masheikh<br />

7. Kuishi na ndugu kwa wema.<br />

8. Kuacha kugombana ila kwa mambo ya Dini ikiwa<br />

inavunjwa.<br />

9. Kutomtegemea mtu kwa kumfanyia kazi zake.<br />

xvii. Karama za Seyyid Abdul Qadir.<br />

(maana ya karama).<br />

Karama ni mambo ya ajabu yenye kudhibiti kwa Mawalii.<br />

Ama mambo kama hayo yanapotokana na Mitume huitwa<br />

„Miujiza‟.<br />

13.


Kwa hakika Seyyid Abdul Qadir alikuwa na karama nyingi mno.<br />

Karama zilikuwa ni dalili za kuonyesha kama alikuwa ni Walii. Na<br />

kila zikizidi ni ishara au ni dalili ya kuonyesha utukufu wa daraja<br />

yake kwa Mwenyezi Mungu.<br />

Kila Muridi wa Seyyid Abdul Qadir, ajue kama<br />

amebahatika mno. Kwani Muridi wake hafi ila awe ametubia, kwa<br />

Mungu, Na huko Ahera hatoingia Motoni.<br />

Mwenyezi Mungu atudumishie mapenzi yetu kwa Seyyid<br />

Abdul Qadir hasa, na Mawalii wengine kwa jumla.Tena Mwenyezi<br />

Mungu atuepushe na madhambi makubwa na madogo pia.<br />

Amin! Amin! Amin!<br />

Hizi ni baadhi ya katika karama zake:<br />

Kwenda mbinguni<br />

1. Hekaya:-<br />

Seyyid Abdul Qadir alikwenda Mbinguni, si kwa kiwili<br />

wili na roho, bali ni kwa roho tu. Huko ni kusema alikwenda<br />

Miiraji. Naye alisimama mahala pale pale „Kaaba kawsayn‟<br />

ambapo alisimama Mtume wakati alipokwenda Miiraji, Huko<br />

alimwona Seyyidna Israil, aliiona Lawhil-Mahfudh na Kursy, Si<br />

tu; bali aliiona mpaka Nuru ya Mwenyezi Mungu (Jalla -Jalaluhu).<br />

Wakati alipofika hapo “Kaaba Kawsayni” alipewa amri ya<br />

kusimama na akaambiwa “Njoo, usiogope. Tumeyakunja mapazia<br />

yetu. Hebu inama unywe upate kuniona.<br />

“Neema iliyoje, mtu kuiona Nuru ya Mwenyezi Mungu”.<br />

14.


Kuwasalisha Mawalii hewani:<br />

2. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitafutwa na<br />

Masheikh wa Baghdad wa Twariqa ya Fawqany. Waliambiwa<br />

kama amekwenda upande wa Mto Tigris. Huko walimwona<br />

anakwenda juu ya maji na huku samaki wa mle mtoni<br />

wanamwendea makundi makundi wakimtolea salam na wakimbusu<br />

mkono wake kwa mboni za macho yao.<br />

Mara tu waliponyanyua macho yao juu waliliona zulia<br />

kubwa rangi ya kijani lililopambwa kwa dhahabu na fedha yenye<br />

kung‟aa. Mtu yeyote akiliangalia atadhania kama labda ni lile zulia<br />

la Nabii Suleiman. Na pale juu ya zulia palikuwa na kitabu<br />

kielezacho utukufu wa Sayyid Abdul Qadir. (Q.s.a).<br />

Ulipoingia wakati wa Adhuhuri kiasi cha saa 6.30; wale<br />

Masheikh wa Baghdad waliwaona Mawalii wengi sana<br />

wamefuatana na wakubwa wao wanakwenda kwenye zulia. Na<br />

pale penye zulia walikuwa wamekaa “Rijalul – ghayb” (Mawalii)<br />

na mkubwa wao yuko mbele. Ulipofika wakati wa kusali, yule mtu<br />

aliyekaa mbele; alikimu Sala na walisimama Mawalii wote huku<br />

wakitazamana nani atakayesalisha. Mara alipita mbele Seyyid<br />

Abdul Qadir kusalisha. <strong>Al</strong>iwasalisha wale Mawalii pamoja na<br />

mkubwa wao, pamoja na Masheikh wa Baghdad na mkubwa wao.<br />

Baada ya kusali Seyyid Abdul Qadir alinyanyua mikono yake juu<br />

kuomba. <strong>Al</strong>iomba hivi:- “Ewe Mola Mtukufu, ninakuomba<br />

asife Murid wangu mwanamume au mwanamke mwenye<br />

kunipenda ila awe ametubia kwa Mola wake”. Baada ya<br />

kuomba, walisikia Malaika wakiitikia “Amiin”. Na walisikia sauti<br />

isemayo:<br />

“Furahi, hakika nimeikubali dua yako”.<br />

Hakika Mungu ndiye Mtukufu, na humpa utukufu yeyote<br />

amtakaye. Heri iliyoje ya kumwomba Mungu na akakujibu papo<br />

kwa papo.<br />

15.


Kumbusu mtume mkono wake.<br />

3. Hekaya:<br />

Seyyid Abdul Qadir alipokwenda Madina kumzuru Mtume<br />

(Saw) muda wa siku 40 alisimama mbele ya kaburi. Ilipotimia siku<br />

ya 40 alimwomba autoe mkono wake nje (kutoka kaburini) ili<br />

aubusu. Pale pale Mtume (Saw) aliutoa mkono wake na Seyyid<br />

Abdul Qadir aliushika na kuubusu. Tena alijiwekea juu ya kichwa<br />

chake. <strong>Al</strong>hamdulillah, utukufu ulioje wa karama.<br />

Kukutana na Mtume kwenye membari.<br />

4. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alisimama kwenye<br />

membari kutoa waadhi. Mara akashuka na akasimama kimya<br />

kitambo hivi kwa adabu na heshima. Baadaye akasimama na<br />

akatoa waadhi.<br />

Mara alipokwisha kutoa waadhi, watu walimwuliza<br />

yaliyomtokea. <strong>Al</strong>ijibu ya kuwa wakati ule Mtume alikuja pale na<br />

akampisha pale alipokaa. Na alipokuwa anaondoka alimwambia<br />

asimame na atoe waadhi alioukusudia.<br />

Kufuturu nyumba 70.<br />

5. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipewa taarifa na watu 70<br />

mablimbali, akafuturu kwao. Ulipofika wakati wa kufuturu, kila<br />

mtu alifurahi kumwona Seyyid Abdul Qadir kuhudhuria kwake.<br />

Habari hiyo ilitapakaa Baghdad nzima. Lakini mmoja katika<br />

watumishi wake alikua akikanya kama<br />

16.


si kweli, kwa sababu yeye alimwona kakaa juu ya takia lake wala<br />

hakutoka. Mwisho mwenyewe SEyyid Abdul Qadir<br />

aliyathibitisha maneno wayasemayo watu kuwa ni kweli.<br />

<strong>Al</strong>imwambia yule mtumishi wake, “Ni kweli nimekwenda kufuturu<br />

kwa watu 70. mmoja mmoja”.<br />

Kumfufua maiti aliyekwisha kuoza<br />

6. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipita katika kijiji, na<br />

aliwakuta watu wawili wanashindana. Mmoja kati ya hao alikuwa<br />

Mwislam na wa Pili alikuwa Mkristo. Seyyid Abdul Qadir<br />

aliwauliza sababu ya kushindana kwao. Yule Mwislam alijibu<br />

“Huyu Mkristo eti anasema kuwa Mtume wao ni bora kuliko<br />

Mtume wetu. Na mimi nasema kuwa Mtume wetu ndiye bora<br />

zaidi”. Seyyid Abdul Qadir alimwuliza yule Mkristo. “Dalili gani<br />

uliyonayo inaonyesha kuwa Nabii Isa ni bora kuliko Nabii<br />

Muhammad (Saw)?” Yule Mkristo alijibu, “ Mtume wetu alikuwa<br />

akifufua maiti.” Tena Seyyid Abdul Qadir alimwambia Mkristo.<br />

“Mimi vilevile nafufua maiti wala si mtume, bali ni mfuasi wake<br />

tu. “Tena Seyyid Abdul Qadir. alimuliza Mkirsto, “Je nikimfufua<br />

maiti utamwamini Nabii Muhammad?” “ Ndiyo, alisema Mkristo.<br />

Tena alisema Seyyid Abdul Qadir alimwambia yule Mkristo,<br />

“Nionyeshe kaburi la mtu aliyekufa zamani.”<br />

Yule Mkristo alifuatana na Seyyid Abdul Qadir na yule<br />

kijana kwenda kwenye kaburi ambalo mwenyewe keshaoza<br />

zamani. Walipofika pale Seyyid Abdul Qadir alimuliza yule<br />

Mkristo “Mtume wenu alikuwa akiwafufua maiti wenu kwa<br />

maneneo gani?” Yule Mkristo alisema, “<strong>Al</strong>ikuwa akimsemeza<br />

maiti kwa kumwambia asimame kwa idhini ya Mungu. Seyyid<br />

Abdul Qadir alimwambia Mkristo<br />

“Mimi nitamfufua kwa idhini yangu” Mara baada ya kusema<br />

17.


Vile, Seyyid Abdul Qadir alimwambia maiti “Simama kwa idhini<br />

yangu”. Saa ile ile alitoka hali ya kuwa yu hai. Yule Mkirsto<br />

kuona vile basi hakusita ila alitoa shabaha mbiombio, na<br />

kumwamini Nabii Muhammad (Saw) mbele ya Seyyid Abdul<br />

Qadir (k.s.a).<br />

Haramia kumgeuza kuwa kutbu:<br />

7. Hekaya:-<br />

Seyyid Abdul Qadir alipokuwa anarudi Madina kwenda<br />

Baghdad, alikumbana na haramia njiani akimngojea mtu ye yote<br />

apitae amnyang‟anye vitu alivyokuwa navyo. Seyyid Abdul Qadir<br />

alipofika pale alimwuliza yule mtu, “Nani wewe?” Yule mtu<br />

alisema kuwa yeye ni haramia. Pale pale Seyyid Abdul Qadir<br />

alikashfiwa na aliona jina lake ni miongoni mwa watu waovu.<br />

Lakini yule mwizi ilimpitia katika roho yake na akawaza kuwa<br />

asiwe huyu ndiye Seyyid Abdul Qadir. Mara tu alivyofikiri vile na<br />

Seyyid Abdul Qadir alimwambia, “Mimi ndiye Abdul Qadir.” Yule<br />

mtu aliposikia vile mara alianguka chini ya miguu ya Seyyid Abdul<br />

Qadir na akasema, “Ewe Bwana wangu, Abdul Qadir kipenzi cha<br />

Mungu.” Muda ule ule Seyyid Abdul Qadir alisikia akiambiwa,<br />

“Ewe Ghawth Mtukufu, mfundishe huyo mwizi njia ya haki”. Tena<br />

Seyyid Abdul Qadir alimfundisha njia ya haki yule mwizi na<br />

mwishoni alikuwa ni mmoja katika Makutbu (Mawalii).<br />

Kusilimu kafiri kwa kuona karama za seyyid<br />

Abdul Qadir.<br />

18.


8. Hekaya:-<br />

Mtu mmoja alitamani kwenda kumzuru Seyyid Abdul<br />

Qadir, kwa wingi wa sifa zake anazozisikia. Pindi alipofika<br />

Baghdad, alipita mahali ambapo, walikuwapo farasi 40 wakila<br />

majani pasina kuchungwa. Farasi hao walikua wake Seyyid Abdul<br />

Qadir. <strong>Al</strong>ipozidi kuwaangalia aliwaona wanayo minyororo ya<br />

dhahabu na fedha na matandiko yao ni ya hariri. Basi ikamjia fikra,<br />

“<strong>Al</strong>a! Vipi Walii mkubwa kama huyu ashughulikie mambo kama<br />

haya ya kilimwengu? Haya niliyoyaona kwake hata wafalme<br />

hawana.”<br />

Yule mgeni alipata maradhi makubwa sana kabla ya kufika<br />

alikokusudia. Kwa hiyo ilimbidi afikie nyumba nyingine badala ya<br />

nyumba ya Seyyid Abdul Qadir. Madaktari wengi walikwenda<br />

kumwangalia kwa kutaka kumtibu.<br />

Mwisho alikwenda Daktari mmoja wa Kinasara ambaye<br />

alisema kama mgonjwa yule dawa yake ni maini ya Farasi wenye<br />

sifa kadha. Watu walishughulika sana kuwatafuta. Lakini<br />

aliyekuwa na Farasi hao ni Seyyid Abdul Qadir tu. Siku ya pli watu<br />

walimwendea Seyyid Abdul Qadir kumwomba. Naye aliwapa bure<br />

farasi mmoja na kunywa dawa nyingine, Yule mgonjwa alipata<br />

nafuu kidogo. Kuona vile, watu walizidi kumwendea na<br />

kumwomba tena na waliendelea mpaka farasi wote 40 wakesha.<br />

Baada ya kupoa, yule mgeni alimuaga mwenyeji wake na<br />

akaenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir na kumshukuru kwa wema<br />

aliomfanyia hata akapata nafuu. Seyyid Abdul Qadir alimwambia<br />

yule mgeni “Ewe kijana, hao farasi mimi niliwanunua kwa sababu<br />

yako wewe; kwa kuona unayo mapenzi makubwa juu yangu. Na<br />

ulipotia azma ya kuja kunizuru mimi nilijua kama utaumwa na<br />

dawa yako ni maini ya farasi. Lakini wewe pale ulipopita karibu<br />

yao na ukawaona, roho yako iliharibika na ukaleta fikra mbaya juu<br />

yangu.” Tena yule kijana alimwomba msamaha na kumtaka radhi<br />

kwa tukio hilo.<br />

19.


Seyyid Abdbul Qadir alimwita yule Daktari Mnasara akampa ile<br />

minyororo ya dhahabu pamoja na yale matandiko ya hariri. Pale<br />

yule Mnasara alisilimu mbele ya Sheikh Seyyid Abdul Qadir kwa<br />

kuona mambo ya siri na karama zake.<br />

Kufuturu chakula cha peponi:<br />

9. Hekaya:-<br />

Seyyid Abdul Qadir alikaa Riadha siku 40 kwa kufanya<br />

Ibada. Siku zote hizo alikuwa ndani ya Siami (funga). Ilimpitia<br />

rohoni mwake kutokufuturu kitu chochote isipokuwa maji mpaka<br />

Mwenyezi Mungu amteremshie chakula cha peponi.<br />

Ilipofika siku ya 38, aliona sakafu ya nyumba inapasuka na<br />

alimwona mtu mwenye birika ya dhahabu katika mkono mmoja na<br />

katika mkono wa pili alikuwa amechukua sahani ya fedha yenye<br />

matunda. Tena hivyo vitu aliviweka mbele ya Seyyid Abdul Qadir.<br />

Seyyid Abdul Qadir aliuliza, “Vitu gani hivi?” Yule<br />

mtumishi alijibu, “Hivyo ni vyakula nimepewa nikuletee.” Seyyid<br />

Abdul Qadir alisema: “Mtume amekataza kulia vyombo vya<br />

dhahabu na fedha. Viondoe hivyo vitu“. Yule Rohani alitoka mbio<br />

na vyombo vyake. Lakini ulipofika wakati wa kufuturu, alishuka<br />

Malaika na sahani iliyojaaa chakula. Yule Malaika alisema: “Ewe<br />

Ghawthil-A`adham, hii ni dhifa yako inayotoka kwa Mwenyezi<br />

Mungu. Seyyid Abdbul Qadir alipokea kile chakula akala yeye<br />

pamoja na wengi wa marafiki zake. Na Mwenyezi Mungu<br />

humruzuku amtakae pasina kudhani kama ataipata riziki hiyo kwa<br />

muda huo.<br />

20.


Mtoto wa kike kugeuka mwanaume.<br />

10.Hekaya:-<br />

Mtu mmoja alimwendea Seyyid Abdul Qadir kumtaka<br />

amuombee dua ili apate mtoto mwanamme. Ghawth alijibu,<br />

“Nimeshakuombea kwa Mungu na atakupa huyo umtakaye”. Yule<br />

Bwana alimpata mtoto, lakini alikuwa mwanamke. Kwa hivyo<br />

alimchukua mpaka kwa Sheikh na kumwambia, “Mimi nilimtaka<br />

mtoto wa kiume, si wa kike”. Seyyid Abdul Qadir alisema: “Basi<br />

mfunike nguo na umrudishe nyumbani, utaona yatakayotokea“.<br />

Mara tu alipofika nyumbani alimwona yule mtoto wa kike<br />

amegeuka kuwa mtoto wa kiume. Kama alivyotaka hasa.<br />

Tajiri kuwaona ngamia wake waliopotea:<br />

11. Hekaya:-<br />

Siku moja Tajiri mmoja alikuwa akisubiri msafara ili<br />

afuatane nao kwenda kufamya biashara. <strong>Al</strong>ikuwa na ngamia 6<br />

ambao amewatwisha magunia ya sukari.<br />

Walipofika katikati ya njia. Ngamia wake walipotea pamoja<br />

na mizigo yao. <strong>Al</strong>iwatafuta sana, lakini hakuwaona. Basi akapiga<br />

ukelele, “Ewe Seyyid Abdul Qadir, ngamia wangu wamepotea<br />

pamoja na mizigo yao”. Kutazama mbele yake alimwona mtu<br />

amevaa nguo nyeupe anampungia mkono, <strong>Al</strong>ipokwenda kule<br />

hakumwona yule mtu bali aliwaona wale ngamia wake pamoja na<br />

mizigo yao.<br />

Ndege kusikiliza maneno:<br />

21.


12. Hekaya:-<br />

Siku moja alikaa Seyyid Abdul Qadir, anazungumza. Basi<br />

akasema: “Lau kama Mwenyezi Mungu angetaka kumleta Ndege<br />

rangi ya kijani kusikilza maneno yangu, basi angekuja”. Baada ya<br />

kumaliza kusema hivi, mara alitokea ndege mzuri wa rangi ile ile<br />

ya kijani. <strong>Al</strong>iingia ndani ya mkono wa kanzu yake kusikiliza<br />

maneno wala hakonekana tena mahala alikokwenda.<br />

Kukatika ndege vipande vipande:<br />

13. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Andul Qadir alikuwa akizungumza, Mara<br />

akaja ndege mzuri wa rangi ya kijani akatua mbele yake ili<br />

kusikiliza maneno yake. Seyyid Abdul Qadir akasma, “Lau<br />

ningemwambia huyu ndege kufa na kukatika vipande vipande basi<br />

angalikufa.” Basi pale pale alianguka na akakatika vipande.<br />

Kuhujumiwa simba mbele ya banda la farasi<br />

14. Hekaya:-<br />

<strong>Al</strong>ikuwapo Walii mmoja jina lake Sheikh Ahmad<br />

Zamdah. Sheikh Ahmad alikuwa akipanda simba na kutembea<br />

naye anapokwenda kwa Mawalii wengine. Pale anapofika humtaka<br />

mwenyeji wake ampe Ng‟ombe mmoja, yaani chakula cha simba<br />

wake. Siku moja yule Sheikh Ahmad alifika Baghdad na akaenda<br />

kwa Seyyid Abdul Qadir.<br />

22.


Basi akamwambia: “Mimi ninayo desturi, pahala ninapofika<br />

hupewa ng‟ombe na kumpa Simba wangu ale, Sasa unasemaje?”<br />

“Nitampa ng‟ombe anayevuta maji”. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir.<br />

<strong>Al</strong>ipokuwa anakwenda kwenye ng‟ombe alipitia pale penye<br />

banda la Farasi wa Ghawth. Pale alikaa mbwa mmoja na<br />

mwanawe. <strong>Al</strong>ipopita Sheikh Ahmad walimfuata. Yule mbwa<br />

alimweka pale alipokaa simba. Mara simba alitaka kumshambulia<br />

mbwa wa Seyyid Abdul Qadir, lakini bahati mbaya mbwa<br />

alimhujumu vikali simba yule na alimwua. Tena Sheikh Ahmad<br />

alirudi kwa Seyyid Addul Qadir na kumtaka radhi kwa<br />

yaliyotokea. Vile vile alitubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />

Kifo cha ndege mia:<br />

15. Hekaya:-<br />

Ilitokea siku moja Seyyid Abdul Qadir alikaa pahala<br />

akifanya Ibada zake. Juu kikapita kikundi kikubwa cha Ndege mia.<br />

Walipomwona Seyyid Abdul Qadir wote walishuka wakatua na<br />

wakamzunguka. Pale walipokaa wakawa wanafanya kelele. Seyyid<br />

Abdul Qadir akatazama juu akasema, “Ewe Mola hawa ndege<br />

wananishughulisha hapa”. Ndege wote walikufa saa ile ile.<br />

<strong>Al</strong>ipowaona wote ni maiti alisema “Ewe Mola unajua sababu ya<br />

kifo chao”. Kusema vile mara wote walifufuka na kwenda zao.<br />

Kujitenga kwenye magofu ya baghdad:<br />

16. Hekaya:-<br />

Seyyid Abdul Qadir alijitenga kwenye magofu kwa muda<br />

23.


usiopungua miaka 25 akifanya Ibada. Siku moja alisikia sauti<br />

iliyomwambia, “Rudi Mjini watu wanakuhitaji kwa manufaa ya<br />

Akhera“. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir:- "Mimi nimekuja huku<br />

kufanya Ibaada kwa kutafuta salama ya Dini yangu, na kuepuka na<br />

fitina za Baghdad“. Kusikia vile tena akaambiwa.“Rudi na<br />

utasalimika Mungu akipenda“. Kusikia vile Seyyid Abdul Qadir<br />

alirudi huku moyo wake umejaa siri za Mungu.<br />

Maneno kujitokeza:<br />

17. Hekaya:-<br />

Kila alipokuwa akikaa Ghawth-A`adham walikuwa<br />

hawaondoki Mawalii – Iwapo amekaa kimya basi maneno hutaka<br />

kujitokeza na kufika mpaka kwenye koo. Basi yakifika hapo hua<br />

hawezi tena kunyamaza bali huwapa siri katika elimu ya “Hakika”.<br />

Unyayo wangu uko shingoni mwa kila walii:<br />

17. Hekaya:-<br />

Maneno haya alipewa idhini na Mtume kuyasema. Na siku<br />

alipoyatamka Baghdad, Mawalii wote wa Ulimwengu mzima<br />

waliyasikia na kila mmoja aliinamisha shingo yake kwa kuridhia<br />

maneno yaliyotamkwa.<br />

Yasemekana walii mmoja wa Damask, Sheikh Rasalam<br />

alisema: “Ewe Mwenyezi Mungu, ninakushuhudiza wewe na<br />

Malaika wako kuwa nimeyasikia maneno ya Bwana<br />

24.


wa Mawalii na nimeyakaribisha. Tena akanyoosha shingo yake<br />

kuonyesha kuwa ameridhia.<br />

Nuru katika kidole chake.<br />

18.Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdbul Qadir aliondoka usiku pamoja<br />

na Masheikh watatu kwenda kuzuru kaburi la Imam Aba Hanifa,<br />

Usiku huo ulikuwa na giza kubwa sana. Hapa na hapo huwezi<br />

kupaona. Lakini Seyyid Abdul Qadir alipofika penye jiwe au mti<br />

aliashiria kwa kidole chake. Na wakati huo lile jiwe au mti<br />

hung‟ara sana mfano wa mbalamwezi kali. Waliendelea na hali<br />

hiyo mpaka wakafika walikotaka na wakafanya waliyokusudia.<br />

Wakati wa kurudi Seyyid Abdul Qadir alikuwa akiashiria<br />

kwa kidole vile vile kwenye hatari na kutoka mwanga mkali<br />

kwenye kile kitu. Tena walipofika<br />

nyumbani kwa Seyyid Abdul Qadir, wale Masheikh waliaga na<br />

wakaenda zao.<br />

Mifupa kuigeuza kuku aliye hai:<br />

19. Hekaya:-<br />

Bibi mmoja alimpeleka mwanawe kwa Seyyid Abdul<br />

Qadir kusomeshwa elimu. Mtoto huyo aliwekwa mahala maalum<br />

kazi yake ni kufanya ibada tu kabla ya kusomeshwa Ilmu.<br />

Siku moja mama yake yule mtoto kuja kumkagua. Lakini<br />

hali alivyomwona nayo mwanawe kidogo haikumpendeza.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa amedhoofu sana. <strong>Al</strong>ipita ndani ili<br />

25.


aonane na Seyyid Abduil Qadir. Kwa uchungu wa mwanawe<br />

ilimtoka subra na akawa anamwandama Seyyid Abdul Qadir kwa<br />

maneno. <strong>Al</strong>isema: “Ewe Ghawthil Aadham, unakula kuku na<br />

unamwacha mwanangu anakula vipande vya mikate ya shairi hata<br />

amekuwa mwembamba kama uzi?“ Seyyid Abdul Qadir hakujibu<br />

chochote isipokuwa aliikusanya ile mifupa na akasema mbele ya<br />

yule mwanamke: “Ewe kuku simama kwa idhini ya Mungu<br />

mwenye kuhusisha mifupa iliyochakaa,” Mara tu baada ya kusema<br />

vile mifupa iligeuka kuku ambaye alisimama mbele ya yule<br />

mwanamke.<br />

Naam hapo Seyyid Abdul Qadir ndipo alipomneneza yule<br />

mwanamke kwa kusema: “Ninapenda mwanao aweze kama haya,<br />

kwa kupata daraja kama hili, anaweza kula chakula chochote<br />

akitakacho mwenyewe”. Mwisho yule bibi alimtaka radhi Seyyid<br />

Abdulm Qadir na akamwambia, “Ewe Seyyid Abdul Qadir,<br />

yaliyonipelekea kusema hayo ni uchungu wa mwanangu tu. Na<br />

tangu sasa hivi nakupa uhuru ufanye utakavyo juu ya mtoto huyo.”<br />

20. Hekaya:-<br />

Kushiba kwa kufyonza kidole:<br />

Sheikh Muhammad Shawry Sabty aliondoka Misri<br />

kwenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir. <strong>Al</strong>ikaa huko kwa siku<br />

nyingi. Sheikh Muhammad alipofunga safari ya kwenda nyumbani,<br />

alipewa wosia na Seyyid Abdul Qadir. Wosia wenyewe ni huu:<br />

"Usitake haja kwa mtu yeyote.“ Baada ya kuusiwa alipewa zawadi<br />

na vyakula vya kula anapokuwa safarini.<br />

Lakini kabla ya kuondoka Seyyid Abdul Qadir alikitia<br />

kidole chake ndani ya kinywa cha Sheikh Muhammad na<br />

akamwambia akifyonze. Baada ya kufanya hivyo tena<br />

26.


akashika njia akaenda zake. Jambo la kustaajabisha ni kuona kuwa<br />

Sheikh Muhammad hakushikwa na njaa wala kiu mpaka akafika<br />

kwake Misri. Na alipokitizama kile chakula alikiona kimeongezeka<br />

wala hakikuharika. Baada ya kupumzika alikula chakula hicho<br />

pamoja na watoto wake na Watu waliokuja kuonana naye.<br />

Kifo cha seyyid Abdul Qadir (Qsa):<br />

Seyyid Abdul Qadir alikufa siku ya Ijumaa, Mfungo saba,<br />

mwaka 561 (A.H). <strong>Al</strong>izikwa kwenye chuo chake<br />

“ Babuluzji”. Kafa na umri wa miaka 91.<br />

Watu wengi walimimminika mazikoni kwake, utasema<br />

labda wanakwenda Arafa kwa vile watu walivyokuwa wengi<br />

ilionekana ni bora zaidi awekwe ili azikwe usiku. Pamoja na hayo<br />

hakubakia mtu yeyote katika Baghdad ila alihudhuria Maziko<br />

yake. Katika majia, masoko na majumba yote yalijaa watu.<br />

Seyyid Abdul Qadir alisalishwa na mwanawe Sheikh<br />

Abdul Wahab na alisaliwa na watu wengi mno; Miongoni mwao<br />

ni wanawe, wanfunzi wake na marafiki zake. Kifo chake Seyyid<br />

Abdul Qadir kilitokea katika zama za Imam Yusufu bin<br />

Muktafa. Wale watu waliokosa kumsalia Sheikh, walipewa nafasi<br />

ya kumsalia wakati wa mchana ulipofunguliwa mlango.<br />

27.


Jihad:<br />

Kwa yeyote anayetaka kutabaruk katika Jihad hii ya<br />

kuchangia katika kuchapisha vitabu vya Dhikri, Tawwasul n.k.<br />

Kwa kuwa hiki ni toleo la kwanza, tunategemea kutoa matoleo<br />

zaidi. Awasiliane na mtunzi wa kitabu hiki moja kwa moja kupitia<br />

simu namba: 0755 547 771 au aitie michango yake kwenye<br />

Account ya Benk:<br />

NMB – CLOCK TOWER A/C. 4082300209. ARUSHA.<br />

TWARIQATUL QADIRIA ARRAZZIKIA JAILANIA.<br />

MAKAO MAKUU<br />

ZAWIA KUU.<br />

P. O. BOX 8105<br />

ARUSHA.<br />

Wabillahit Tawfiq.<br />

28.


Swahib Sujjada:<br />

KIMETOLEWA NA:-<br />

Mtungaji:-<br />

<strong>Al</strong> Habib Sheikh Salim Bin Mbarak.<br />

(Dar-wesh – Mti mkavu)<br />

P.O. Box 8105,<br />

Zawia kuu.<br />

Arusha - Tanzania.<br />

(E.A)

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!