You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Seyyid Sheikh
Mtungaji:-<br />
Swahib Sujjada:<br />
Sheikh Salim Bin Mbarak (Dar-wesh – Mti mkavu)<br />
P. O. Box 8105,<br />
Zawia kuu – Arusha,<br />
Tanzania. (E.A).<br />
i.
Swahib Sujjada,<br />
<strong>Al</strong> habib Sheikh Salim Bin Mbarak.<br />
(Dar-wesh Mti Mkavu).<br />
ii.
Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan<br />
(Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz).<br />
First Addition Toleo la kwanza<br />
iii.
Swahib Sujjada:<br />
<strong>Al</strong> Habib Sheikh Salim Mbarak<br />
(Mti - Mkavu).<br />
iv.
Yaliyomo:<br />
No. Ukurasa.<br />
1. Dibaji……………………………………….. vi.<br />
2. Utangulizi…………………………………... vii.<br />
3. Jina lake la kuzaliwa……………………….. 1.<br />
4. Nasabu yake..………………………………. 2.<br />
5. Makuzi yake na kusoma Qur an.………........ 2.<br />
6. Kutafuta Ilmu ……………………………… 3.<br />
7. Masheikh zake…………………………….. 4.<br />
8. Umaarufu wake kwa kusoma……………… 5.<br />
9 Kusomesha kwake Ilmu……………..…….. 7.<br />
10. Namna ya Twariqa ilvyoenea….………….. 8.<br />
11. Siri ya Ilmu ya Tasawfu ..………………..... 10.<br />
12. Sifa za Seyyid Abdul Qadir…..…………… 11.<br />
13. Wake zake na watoto wake……………….. 12.<br />
14. Wasia wake kwa mwanawe A`bdul Razaq.. 13.<br />
15. Karama zake……………............................ 13.<br />
16. Kifo cha Seyyid Abdul Qadir Jaylani (Qsa).. 27.<br />
v.
DIBAJI:<br />
Sifa zote njema zinamstahiki ALLAH ambaye<br />
amefundisha kwa wasta wa kalamu. Na akamfundisha Mwana<br />
Adam lile asilolijua. Na Rehma na Amani Zimwendee Bwana<br />
Mtume Saw na Ahly zake watukufu na Maswahaba wake watiifu.<br />
Kwa ridhaa ya mtunzi wa kitabu hiki ambae ni kiongozi<br />
mkuu na Mlezi wa Twariqatul-Qadiriya– Rrazziqiya–Jaylaniya <strong>Al</strong><br />
habib Sheikh Salim ibn Mbarak –(Dar-weish Mti mkavu) –<br />
(Radhia ALLAH Anhu). Naandika Dibaji ya kitabu hiki kwa<br />
munassaba wa kuya yakinisha yaliyomo kwenye kitabu hiki.<br />
Kwa hakika kitabu hiki kimeelezea historia na sifa kadhaa<br />
za Bwana wa Mawalii Seyyid Sheikh Abdul-Qadiri- Jaylani<br />
(Qada-sa-Llahu-Siral-Aziz)<br />
Basi ukiwa utajaaliwa kusoma kitabu hiki utamjua vilivyo<br />
alivyo Walii wa Mwenyezi Mungu na Uasili wa Twariqa kwa<br />
ujumla.<br />
Insha-<strong>Al</strong>lah tunamuomba <strong>Al</strong>lah amjaalie kila la kheri mtunzi<br />
wa kitabu hiki Sheikh Salim amjaalie Mahaba zaidi ya kudarisisha<br />
hususan kwa kutunga vitabu vingi zaidi vitavyotoa Ilmu na<br />
muongozo wa ibada za Kitwariqa kwa misingi ya Kitassawfu.<br />
Aamiin Aamiin Aamiin wal-hamdulillahi Rabbil-A`alamiin<br />
Khalifa Mohamed Omar.<br />
Mwenyekiti wa Twariqatul-Qadiriya-Rrazziqiya-<strong>Al</strong>-Jaylaniya<br />
Makao Makuu Ya Twariqa – Zawiya Kuu<br />
S.L.P. 8105<br />
Arusha.<br />
Tanzania (E.A)<br />
vi.
UTANGULIZI:<br />
“Assalamu alay–kum warah–matullahi –Taala wabarakatuh”.<br />
Namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kunijaalia fikra<br />
na utashi wa kuandika kitabu hiki nilichokitambulisha kwa jina la<br />
Ghawth–l–A`adham, Seyyid Sheikh – Abdul – Qadir-Jaylani.<br />
(Qad-sa-Llahu-Siral-A`ziz)<br />
Makusudio yangu makubwa katika kuandika kitabu hiki ni<br />
kuelezea sifa na mwenendo wa maisha ya Bwana wa Mawalii na<br />
kipenzi cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume (Saw).<br />
Ni Matarajio yetu Historia hii tuliyoiandika ndani ya kitabu<br />
hiki itahifadhika na kujenga kumbukumbu juu ya maisha ya watu<br />
wema kwa ujumla. Kuwakumbuka watu wema na kufuatisha<br />
matendo mema ni ufunguo wa kheri hapa duniani na Akhera.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mwenyezi Mungu amjaalie kila la kheri msomaji<br />
wa kitabu hiki na amjaalie kuwa na matendo mema.<br />
“Eee Mwenyezi Mungu tujaalie sote<br />
mwishilio mwema na utujaalie kuwa<br />
watu wa peponi”<br />
(Aamiin).<br />
Sheikh Salim Ibn Mbarak – (Dar-weish – Mti Mkavu).<br />
S.L.P 8105<br />
Zawiya Kuu – Arusha.<br />
Tanzania (E.A).<br />
vii.
viii.
i. Maisha ya Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />
Seyyid Abdul Qadir ni Muajemi. Naye ni mashuhuri si<br />
katika Ardhi tu, bali hata Mbinguni pia. Yeye ni Sheikh wa<br />
Waislam na ni kiigizo kwa Mawalii na watu wema. Seyyid Abdul<br />
Qadir alikuwa Imamu wa Siddikin na A`arifiyn.<br />
Sharafu yake kwa Mawalii wenzake ni kama Sharafu ya<br />
Nabii Muhammad kwa Mitume wenzake.<br />
ii. Kuzaliwa kwake:<br />
Seyyid Abdul Qadir alizaliwa katika kijiji cha Jeilan huko<br />
Iraq. <strong>Al</strong>izaliwa usiku wa kuamkia Mwezi mosi wa Ramadhani<br />
mwaka 470. A.H.<br />
Bi Fatma alichukua mimba ya mtoto huyo na hali ya kuwa<br />
umri wake ni miaka 60. Wakati ambao hapana tamaa ya kupata<br />
mtoto yeyote.<br />
Siku hiyo aliyomzaa Seyyid Abdul Qadir ilizagaa Nuru<br />
ambayo ilitapakaa kijiji kizima. Mambo hayakuwa hayo tu, lakini<br />
hapakuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuuangalia uso wake kwa<br />
mng‟aro na haiba yake.<br />
Tabia zake zafanana na zile za Seyydina Muhammad<br />
(Saw). Uzuri wake ni ule kama wa Nabii Yusuf (A.s). Ukweli wake<br />
unalingana na Seyyidna Abu-Bakar. (R.a) Haki yake ni kama ile ya<br />
Seyyidna Omar (R.a), na upole wake wa Seyyidna Othman. (Ra).<br />
iii. (a) Nasabu yake kwa kuumeni<br />
Yeye ni Seyyid Abdul Qadir bin Mussa bin Abdillah<br />
1.
in Yahya bin Muhammad bin Daudi bin Mussa bin Abdillah Bin<br />
Mussa bin Abdillahi bin Hassan bin Seyyid Hassan bin <strong>Al</strong>ly bin<br />
Abi Talib. Yaani nduguye Mtume (Saw).<br />
(b). Nasabu yake kwa kukeni.<br />
Yeye ni mtoto wa Bi Fatma Bint Seyyid Abdillah Sawmaiy<br />
Bin Seyyid Mahmoud bin Issa Bin Muhammad Bin <strong>Al</strong>i Bin Mussa<br />
Bin Jaafari Swadiq Bin Muhammad Bin Seyyidna Hussein Bin<br />
<strong>Al</strong>ly Bin Abi Talib.<br />
Unapoangalia nasabu zake zote yaani kukeni na kuumeni, utaona<br />
kama zimekutana kwa Seyyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib; yaani nduguye<br />
Mtume (Saw).<br />
iv. Kukua kwake na kusoma Qur ani<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa akikua na akiishi katika hali<br />
nzuri. Mji wake uliingia neema kubwa kabisa baada ya kuzaliwa<br />
kwake. Seyyid Abdul Qadir alipewa Uwalii na hali ya kuwa ni<br />
mtoto kama Nabii Isa alivyopata Utume katika hali hiyo hiyo.<br />
Ishara zilizoonyesha kama yeye ni Walii ni nyingi na katika<br />
hizo ni:-<br />
(i) Kutamka „Hatifu‟ maneno siku ya mwanzo<br />
alipopelekwa chuoni kusoma Qur an. Maneno<br />
yenyewe ni haya “Mfanyieni nafasi ya kukaaWalii wa<br />
Mwenyezi Mungu”.<br />
(ii) Kusifiwa kwake na „Abdal‟ kwa kusema: “Mtoto<br />
2.
huyu atakuwa na mambo matukufu<br />
atakayosifiwa mwishoni kwake”.<br />
(iii). Bishara ya Mtume aliyompa Baba yake<br />
usingizini - “kwamba atamzaa mtoto ambaye<br />
atakuwa na mambo matukufu atakayosifiwa<br />
mwishoni kwake”.<br />
v. Kutafuta Ilmu:<br />
Seyyid Abdul Qadir alipotimia miaka 18, alimwomba<br />
ruhusa mama yake kusafiri kwa kutafuta Ilmu ambayo ni wajibu<br />
kwa kila Mwislamu mwanamke na mwanaume. <strong>Al</strong>iondoka kwenda<br />
Baghdad pamoja na Nabii Khidhri. Lakini kabla ya kuingia ndani<br />
ya Mji wa Baghdad; Nabii Khidhri alimpa Seyyid Abdul Qadir<br />
sharti ambalo atakapolitekeleza ndipo atapompeleka kwa Masheikh<br />
kusoma. Sharti yenyewe ni kukaa pale nje ya mji na kufanya ibada<br />
kwa muda wa miaka mitatu kamili. Seyyid Abdul Qadir alikubali.<br />
Tangu siku ile Nabii Khidhri hakupapita tena mpaka mwaka<br />
ukamalizika.<br />
Baada ya kutimia mwaka mmoja, Nabii Khidhri alikwenda<br />
kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Seyyid Abdul Qadir alipomwona<br />
Nabii Khidhri alimsimamia. Lakini Nabii Khidhri alikataa<br />
kunyanyukiwa na kumwambia akae kitako.<br />
Siri ya kuwekwa Seyyid Abdul Qadir peke yake kwa<br />
muda wote ule, apate kuitakasa roho yake na ile sehemu<br />
inayoharibiwa na Shetani. Vitisho alivyokuwa akivipata mahala<br />
pale havikuwa na mfano. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda Walii<br />
wake na akamhifadhi na kila baya na vitisho. Ulipotimia mwaka<br />
wa tatu. Nabii Khidhri alikwenda mahala pale kwa ajili ya<br />
kumchukua Seyyid Abdul Qadir.<br />
3.
Juu ya kuwa wamo ndani ya safari pamoja, Seyyid Abdul<br />
Qadir kabisa alikuwa hamjui mtu anayefuatana naye. Lakini alikuja<br />
kumjua baadaye hapo alipokwenda Baghdad kumkagua.<br />
Seyyid Abdul Qadir alisoma kwa juhudi na ari kubwa na<br />
aliwashinda wenzake wote kwa Ilmu na ufasaha wa lugha. Na<br />
alikuwa jogoo mkubwa wa Madhehebu ya Shafi na Hambali. Na<br />
alikuwa akijibu na akifutu masuali kwa Madhehebu hayo mawili.<br />
Lakini yeye mwenyewe alikuwa akifuata madhehebu ya Hambal.<br />
vi. Katika baadhi ya Ilmu alizosoma.<br />
(i) Qur an (Tafsiri)<br />
(ii) Fiqh<br />
(iii) Hadith<br />
(iv) Usuli-fiq<br />
(v) Tarikh (historia)<br />
(vi) Tasawuf<br />
(vii) Lugha. n.k.<br />
vii. Masheikh zake:<br />
Seyyid Abdul Qadir amesoma Ilmu kwa Masheikh wengi<br />
na kila mmoja katabahari katika fanni mbalimbali. Masheikh<br />
wenyewe ni:-<br />
1 Sheikh Abdil-Wafa <strong>Al</strong>i Bin Ukayl.<br />
2. Sheikh Abi Said-al-Mubaraq.<br />
3. Sheikh Abdil Khatib Mahfudh<br />
Kaludhany.<br />
4.
4. Sheikh Abi – Hassan Muhammad.<br />
5. Sheikh Kadhi Abi Said.<br />
6. Sheikh Yahya Bin <strong>Al</strong>i.<br />
7. Sheikh Abi Ghalib Muhhamad bin Abdul<br />
Karim.<br />
8 Sheikh Abu Said Muhammad bin Abdul<br />
Karim.<br />
9. Sheikh Muhammed bin Muhammed<br />
10 Sheikh Abubakar Ahmed bin Ahmed<br />
11. Sheikh Abu Jafar bin Ahmed<br />
12. Sheikh Abu Kassim <strong>Al</strong>i bin Ahmed<br />
13. Sheikh Abu Talibu Abdul Kadir bin<br />
Muhammad<br />
14. Sheikh Abdul Rahman bin Yusuf.<br />
15. Sheikh Abdul Rahaman bin Ahmed<br />
16. Sheikh Abu - Barakat Hibatullah<br />
17. Sheikh Abdul-Izzi Muhammed bi<br />
Mukhtar.<br />
18 Sheikh Abu – Nasri Muhammed<br />
19. Sheikh Abu – Ghalib Ahmad<br />
20. Sheikh Abu – Abdalla Yahya<br />
21. Sheikh Abu – Hassan Mubarak<br />
22. Sheikh Mansur Abdul Rahman<br />
23. Sheikh Abu Barakat Taibat Akuly.<br />
viii. Umaarufu wake kwa kusoma<br />
Sifa za Seyyid Abdul Qadir zilizagaa kwa Ilmu yake.<br />
Ingawa wengi walifurahi kwa mambo hayo, lakini mahasidi wake<br />
walikuwa wakikereka - Nao ni katika nafsi ya wanachuoni<br />
wenzake.<br />
Siku moja walimjia wanachuoni 100 wakati alipokuwa<br />
akisomesha ili kumhoji. Na kila mmoja katika hao alikuwa na<br />
suala mbalimbali, na muradi wao ashindwe ili afedheheke.<br />
5.
Wakati huo watapata kueneza kama hajui kitu kuliko wao. Mara tu<br />
wale wanachuoni walipofika pale walikaa kitako kumsikiliza.<br />
Baada ya kukaa, Seyyid Abdul Qadir alikiimanisha kichwa chake.<br />
Na wakati huo lilimtoka pande la Nuru kifuani mwake<br />
likanyakuwa yote waliyoyadhibiti katika vifua vyao. Mara wakawa<br />
wanababaika na kuwayawaya, huku wanapiga makelele wakirarua<br />
nguo zao mfano wa wenda wazimu. Wote walivua vilemba vyao na<br />
wakamwendea Sheikh pale alipokaa. Kila mtu alikuwa akinyanyua<br />
mguu wa Seyyid Abdul Qadir na kujiwekea kichwani kwake. Hii<br />
ni ishara kuonyesha kama wameridhika na kukinai kuwa ni<br />
Mwanachuoni na amewazidi. Na kila mtu alipokuwa akifanya hayo<br />
yeye alikuwa akimkumbatia.<br />
Waliporudi vikaoni mwao, yote waliyokuwa wameyasahau<br />
wakayakumbuka tena. Seyyid Abdul Qadir alimwambia kila mtu<br />
suala aliyokusudia kuuliza na akampa jawabu nzuri ambayo hata<br />
yeye mwenyewe hakufikiria. Wote walistaajabu na walimpa heko.<br />
ix. Muda wa kutoa waadhi<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitoa waadhi mara tatu kila<br />
wiki kwa muda wa miaka 40. Masheikh, Mafaqih na wanachuoni<br />
wengi wa Baghdad walikuwa wakimiminika kumsikiliza waadhi<br />
wake.<br />
Naam, Katika jumla ya wasikilizaji wa waadhi; Mayahudi<br />
na Manasara walikuwamo.<br />
Taathira kubwa ilipatikana kila waadhi aliokuwa akiutoa<br />
kwani Mayahudi na Manasara wengi kabisa walisilimu. Na<br />
miongoni mwa Waislamu wengi wafanyao maasi walitubu katika<br />
maasi yao.<br />
6.
Ama masomesho yake yalizidi kupatia utukufu. Kwani Bibi<br />
mmoja alijitolea nafsi yake aolewe na Seyyid Abdul Qadir bila<br />
mahari yoyote, isipokuwa alimpa sharti moja, nayo ni<br />
kuwasomosha watu Ilmu kwa muda maalum. Muda ulipotimia,<br />
Bibi yule aliolewa kama alivyotamani.<br />
X. Kusomesha kwake Ilmu:<br />
Katika chuo chake, Seyyid Abdul Qadir alikuwa<br />
akisomesha Ilmu 13 za sheria. Na katika Ilmu hizo 13, aliweka<br />
darsa moja kusomesha Madhehebu mbalimbali na darsa nyinginezo<br />
alikuwa akisomesha Hitilafu za Wanachuoni. Baada ya sala ya<br />
<strong>Al</strong>fajiri, alikuwa akisomesha Tafsir ya Qur an na akisomesha<br />
Hadithi za Mtume (Saw) Darsa hizo zilikuwa zikisomwa na kila<br />
mtu aliyetaka. Ama Ilmu za Madhehebu mbalimbali, Khitilafu za<br />
Wanachuoni, Adabu, Fiq na Usuli Dini zilikuwa zikismwa na<br />
Mawalii tu.<br />
Wakati wa Adhuhuri, ilikuwa ikisomwa Qur an kwa Kiraa<br />
(visomo) 7. Darsa ilikuwa ikihudhuriwa na wanafunzi 650<br />
waliokuwa mahodari sana. Wasomaji wake wakubwa wa Qur ani<br />
walikuwa Sheikh Masoud al Hashimiy na Sheikh Abdul Wahab bin<br />
Abdul Qadir (mwanawe).<br />
xi. Kufutu kwake masuala<br />
Katika fatwa zake, Sheikh alikuwa halazi suala wala<br />
alikuwa hafikiri, Bali alikuwa hanafutu mara moja tu. Kabla ya<br />
kufutu au kujibu suala yoyote, ilikuwa ikisomwa Qur an. Jawabu<br />
zake zilikuwa ama za kuandika au za mdomo. Na jawabu zake<br />
zilikuwa zikiwafurahisha watu kwa ustadi wake.<br />
7.
xii. Namna ya Twariqa ilivyoenea<br />
Asili ya Twariqa inatokea kwa Mwenyezi Mungu. Yeye<br />
akamfundisha Seyyidna Jibril As, na Seyyidna Jibril akamfundisha<br />
Seyyidna Muhammad (Saw), tena Nabii Muhammad akamfundisha<br />
Seyyidna <strong>Al</strong>i (R.a) Baadaye ikaendelea kwa Masheikh hawa hata<br />
nao wakaifikisha hapa Tanzania na mwenginepo:-<br />
1. Seyyidna Hassan al Busry.<br />
2. Seyyidna Arif Samdany<br />
3. <strong>Al</strong>habibul Ajemy.<br />
4. Daud Taiy<br />
5. Maaruf al Karkhy.<br />
6. Sharif Sakaty<br />
7. Abi Kasim al Juneid<br />
8. Abu Bakar Shily<br />
9. Abu Fadhi Abdul Wahid<br />
10. Abu Faraj Tusy<br />
11. Seyyidna Abdul Hassan<br />
12. Seyyidna Abu Said –al – Makhzumy.<br />
13. Seyyid Abdul Kadir al Jeilany na kadhalika.<br />
xiii. Siri ya Ilmu ya Twariqa<br />
Ilmu ya twariqa imefanywa kwa Qur an na Hadithi za<br />
Mtume (Saw) pamoja na mambo yafuatayo:-<br />
(i) Kusafisha moyo<br />
(ii) Ukarimu<br />
(iii) Ustahamilivu<br />
(iv) Kuwasamehe waliokuudhi<br />
(v) Kuacha au kujiepusha na maasi<br />
(vi) Kufanya Ibaada kwa jitihada.<br />
8.<br />
.
Faida. i.<br />
Hizi Twariqa ziko namna nyingi, nazo zinapata kama 17.<br />
Katika hizo ni Qadiry, Shadhily, Nakshahabandy, Indarusy<br />
n.k.<br />
Ama Twariqa yoyote akiifuata mtu kama<br />
inavyohitajia, basi itaweza kumfikisha kwa Mwenyezi<br />
Mungu. Kwani lengo lao ni moja tu lakini kwa yote hayo<br />
niliyoeleza inapasa kupatikana Sheikh Mwongofu wa<br />
kukupa „Ijaza‟ na kukufundisha njia za kupita na kukupa<br />
wasia. Huyu mtu anayepewa „Ijaza‟ na Sheikh huitwa<br />
„Muridi‟ Kwa hivyo kila Murid ajitahidi sana kutekeleza<br />
ahadi atakazopewa na Sheikh wake.<br />
Faida ii.<br />
Yatakiwayo kwa Muridi<br />
1. Kutubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />
2. Kufanya Ibaada kiasi ya uwezo wake.<br />
3. Kufanya mambo yalio halali<br />
4. Kuacha mambo yaliyo haramu.<br />
5. Kumdhukuru Mungu<br />
6. Kushikamamna na “Laa ila ha illa Llah” hasa baada<br />
ya kila Sala mara 165 na wakati mwngine kiasi ya<br />
kuweza kwake.<br />
7. Kusoma sana Qur an kwa kila hali.<br />
8. Kuwasamehe wenye kukuudhi.<br />
9. Kuwa mstahamilivu.<br />
10. Kuwa karimu<br />
11. Kuacha husda, kijicho, choyo, uwongo wa<br />
kuwasengenya watu.<br />
12. Kudumu na udhu.<br />
13. Kumsalia Mtume (S.a.w) kwa wingi.<br />
9.
xiv. Siri ya Ilmu ya tasawuf:<br />
Ilmu ya Tasawfu imefanywa kwa mambo yafuatayo:-<br />
Faida:-<br />
(i) Ukarimu.<br />
(ii) Kuridhia hukumu ya Mungu.<br />
(iii) Subira<br />
(iv) Ishara<br />
(v) Upweke<br />
(vi) Kuvaa nguo za sufi<br />
(vii) Kwenda sana<br />
(viii) Umaskini.<br />
Katika hizo sifa nane zilizotajwa hapo juu, zimechukuliwa<br />
kutokana na Mitume wanane mbalimbali:-<br />
1. Ukarimu: Ilikuwa sifa kubwa sana ya Nabii Ibrahim<br />
(Asw).<br />
2. Ridhaa: (kuridhia), ni sifa ya Nabii Is-haq. (As).<br />
3. Subra: Ni sifa ya Nabii Ayub, (A.s)<br />
4. Ishara: Ni sifa ya Nabii Zakaria (A.s)<br />
5. Sufi: Ni kivazi cha Nabii Yahya (A.s)<br />
6. Upweke: Ni sifa ya Nabii Yusufu (A.s)<br />
7. Kwenda : Ni sifa ya Nabii Issa, (As) na ndio maana<br />
akaitwa „Masihi‟<br />
8. Umaskini: Ni sifa ya Nabii Muhammad (Saw).<br />
10.
xv. Sifa za Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa karim sana na mwenye sifa na<br />
tabia nzuri za kupigiwa mfano. <strong>Al</strong>ikuwa na kimo cha wastani, si<br />
mrefu sana wa kuchusha wala hakuwa mfupi. <strong>Al</strong>ikuwa mwekundu<br />
wa weupe. <strong>Al</strong>ikuwa na nyusi nzuri sana. Mwili wake ulikuwa<br />
mwembamba, macho yake yalikuwa yenye haiba kubwa. Kifua<br />
chake kilikuwa kipana chenye Ilmu nyingi. <strong>Al</strong>ikuwa mkali kama<br />
babu yake Sayyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib. Ama ndevu zake zilikua<br />
ndefu namna zile za Nabii Harun (As).<br />
Seyyid Abdul Qadir alikua na cheo au makamo matukufu<br />
mbelel ya Mwenyezi Mungu. Katika Ulimwengu alikuwa ni mtu<br />
mwenye kusikilizwa sana sauti. Sauti yake iliokuwa nzuri na<br />
nyororo kama lulu. Anaposema husema upesi upesi. Hakupata<br />
kupenga makamasi wala kutema makohozi. Mwisho inzi hakupata<br />
kumtua juu ya mwili wake.<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa mnyenyekvu na mkweli.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa na kawaida ya kumtolea mtu salamu mwanzo kila<br />
wanapokutana naye.<br />
Aidha alikuwa akikaa na maskini kama alivyokuwa<br />
akifanya Nabii Muhammad (Saw). Pamoja na utukufu aliokuwa<br />
nao, alikuwa akiwasimamia watoto wadogo na alikuwa<br />
akiwatukuza watu wazima kama ilivyokuwa ada yake Mtume<br />
(Saw). Ingawa alikuwa akiwasimamia watoto lakini hakupata<br />
kumsimamia mtu yeyote katika watu watukufu.<br />
Seyyid Abdul Qadir hakupata kugonga mlango wa<br />
Mfalme au waziri yeyote kwa kumtaka haja ya kilimwengu.<br />
Kazi yake ilikuwa ni kuamrisha mema na kukataza maovu.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa akila na wageni na marafiki zake.<br />
Kadhalika alikuwa akiwapa nguo na chakula maskini.<br />
Vile vile alikuwa akiwapa zawadi nzuri nzuri wanapomwendea<br />
kwake. Kwa ukarimu wake hakupata kumrejesha mtu yeyote<br />
aliyemwomba wakati wa shida, seuze wakati wa raha.<br />
11.
Mavazi yake yalikuwa ya fahari, kama mavazi ya kifalme. Mavazi<br />
hayo aliyavaa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.<br />
Siku moja alipita mtu mwenye haja na akavua nguo hizo<br />
akampa yeye. <strong>Al</strong>itoa Joho ambalo thamani yake yadi moja ni<br />
Dinari 20; yaani Sh. 240/-<strong>Al</strong>itoa na kilemba ambacho thamanai<br />
yake ni Dinari 70,000 yaani sh. 840,000/- .<br />
xvi. Wake zake<br />
Seyyid Abdul Qadir hapo mwanzoni mwake alikaaa muda<br />
mrefu sana bila ya kuoa. <strong>Al</strong>ikaa muda mrefu kwa Ibaada na<br />
alichelea kuvaana na mambo ya ndoa asije akashughulika na<br />
akapunguza Ibaada zake kwa mshughuliko wa wakeze. Siku moja<br />
aliendewa na Mtume(Saw) akamwambia aoe. Kwa kupata nasaha<br />
hiyo ndipo alipooa, na alioa wake wanne.<br />
xvii Watoto wake:<br />
Watoto aliozaa Seyyid Abdul Qadir ni 49. Katika hao 27<br />
walikuwa watoto wanaume na 22 walikuwa wanawake.<br />
Hawa wafuatao ni miongoni mwa hao watoto wa kiume wa<br />
Seyyid Abdul Qadir aliowaacha baada ya kufa:-<br />
1. Sheikh Abdul Wahab<br />
2. Sheikh Abdul Razak<br />
3. Sheikh Abdul Aziz<br />
4. Sheikh Abdul Jabbar<br />
5. Sheikh Abdul Ghafur<br />
6. Sheikh Abdul Ghina<br />
12.
Faida:-<br />
Sayyid Abdul Qadir alipokuwa akiumwa siki moja aliwahi<br />
kuzimia. Wakawa wanawe na wakeze wanalia, Mara tu baada ya<br />
kupata fahamu, alisema, “Msilie nitapona, kwani mgongoni<br />
mwangu bado yuko mtoto mmoja Yahya” wale watu walidhania ati<br />
maneno ya kigonjwa. Kumbe ni ya kizima. Kwani alipona katika<br />
ule ugonjwa, na alimzaa huyo Yahya kama alivyosema. Mtoto<br />
huyo alimpata kwa Suria wake Halima. Mtoto huyo ndiye<br />
aliyekuwa kitinda-Mimba.<br />
xviii Wasia wake juu ya mwanawe, Abdul-Razak.<br />
1. Kumcha Mungu.<br />
2. Kumtii Mungu.<br />
3. Kufuata sharia<br />
4. Kuhifadhi mipaka ya Mungu<br />
5. Kuwatunza na kuwarehemu mafukara<br />
6. Kuwatukuza Masheikh<br />
7. Kuishi na ndugu kwa wema.<br />
8. Kuacha kugombana ila kwa mambo ya Dini ikiwa<br />
inavunjwa.<br />
9. Kutomtegemea mtu kwa kumfanyia kazi zake.<br />
xvii. Karama za Seyyid Abdul Qadir.<br />
(maana ya karama).<br />
Karama ni mambo ya ajabu yenye kudhibiti kwa Mawalii.<br />
Ama mambo kama hayo yanapotokana na Mitume huitwa<br />
„Miujiza‟.<br />
13.
Kwa hakika Seyyid Abdul Qadir alikuwa na karama nyingi mno.<br />
Karama zilikuwa ni dalili za kuonyesha kama alikuwa ni Walii. Na<br />
kila zikizidi ni ishara au ni dalili ya kuonyesha utukufu wa daraja<br />
yake kwa Mwenyezi Mungu.<br />
Kila Muridi wa Seyyid Abdul Qadir, ajue kama<br />
amebahatika mno. Kwani Muridi wake hafi ila awe ametubia, kwa<br />
Mungu, Na huko Ahera hatoingia Motoni.<br />
Mwenyezi Mungu atudumishie mapenzi yetu kwa Seyyid<br />
Abdul Qadir hasa, na Mawalii wengine kwa jumla.Tena Mwenyezi<br />
Mungu atuepushe na madhambi makubwa na madogo pia.<br />
Amin! Amin! Amin!<br />
Hizi ni baadhi ya katika karama zake:<br />
Kwenda mbinguni<br />
1. Hekaya:-<br />
Seyyid Abdul Qadir alikwenda Mbinguni, si kwa kiwili<br />
wili na roho, bali ni kwa roho tu. Huko ni kusema alikwenda<br />
Miiraji. Naye alisimama mahala pale pale „Kaaba kawsayn‟<br />
ambapo alisimama Mtume wakati alipokwenda Miiraji, Huko<br />
alimwona Seyyidna Israil, aliiona Lawhil-Mahfudh na Kursy, Si<br />
tu; bali aliiona mpaka Nuru ya Mwenyezi Mungu (Jalla -Jalaluhu).<br />
Wakati alipofika hapo “Kaaba Kawsayni” alipewa amri ya<br />
kusimama na akaambiwa “Njoo, usiogope. Tumeyakunja mapazia<br />
yetu. Hebu inama unywe upate kuniona.<br />
“Neema iliyoje, mtu kuiona Nuru ya Mwenyezi Mungu”.<br />
14.
Kuwasalisha Mawalii hewani:<br />
2. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitafutwa na<br />
Masheikh wa Baghdad wa Twariqa ya Fawqany. Waliambiwa<br />
kama amekwenda upande wa Mto Tigris. Huko walimwona<br />
anakwenda juu ya maji na huku samaki wa mle mtoni<br />
wanamwendea makundi makundi wakimtolea salam na wakimbusu<br />
mkono wake kwa mboni za macho yao.<br />
Mara tu waliponyanyua macho yao juu waliliona zulia<br />
kubwa rangi ya kijani lililopambwa kwa dhahabu na fedha yenye<br />
kung‟aa. Mtu yeyote akiliangalia atadhania kama labda ni lile zulia<br />
la Nabii Suleiman. Na pale juu ya zulia palikuwa na kitabu<br />
kielezacho utukufu wa Sayyid Abdul Qadir. (Q.s.a).<br />
Ulipoingia wakati wa Adhuhuri kiasi cha saa 6.30; wale<br />
Masheikh wa Baghdad waliwaona Mawalii wengi sana<br />
wamefuatana na wakubwa wao wanakwenda kwenye zulia. Na<br />
pale penye zulia walikuwa wamekaa “Rijalul – ghayb” (Mawalii)<br />
na mkubwa wao yuko mbele. Ulipofika wakati wa kusali, yule mtu<br />
aliyekaa mbele; alikimu Sala na walisimama Mawalii wote huku<br />
wakitazamana nani atakayesalisha. Mara alipita mbele Seyyid<br />
Abdul Qadir kusalisha. <strong>Al</strong>iwasalisha wale Mawalii pamoja na<br />
mkubwa wao, pamoja na Masheikh wa Baghdad na mkubwa wao.<br />
Baada ya kusali Seyyid Abdul Qadir alinyanyua mikono yake juu<br />
kuomba. <strong>Al</strong>iomba hivi:- “Ewe Mola Mtukufu, ninakuomba<br />
asife Murid wangu mwanamume au mwanamke mwenye<br />
kunipenda ila awe ametubia kwa Mola wake”. Baada ya<br />
kuomba, walisikia Malaika wakiitikia “Amiin”. Na walisikia sauti<br />
isemayo:<br />
“Furahi, hakika nimeikubali dua yako”.<br />
Hakika Mungu ndiye Mtukufu, na humpa utukufu yeyote<br />
amtakaye. Heri iliyoje ya kumwomba Mungu na akakujibu papo<br />
kwa papo.<br />
15.
Kumbusu mtume mkono wake.<br />
3. Hekaya:<br />
Seyyid Abdul Qadir alipokwenda Madina kumzuru Mtume<br />
(Saw) muda wa siku 40 alisimama mbele ya kaburi. Ilipotimia siku<br />
ya 40 alimwomba autoe mkono wake nje (kutoka kaburini) ili<br />
aubusu. Pale pale Mtume (Saw) aliutoa mkono wake na Seyyid<br />
Abdul Qadir aliushika na kuubusu. Tena alijiwekea juu ya kichwa<br />
chake. <strong>Al</strong>hamdulillah, utukufu ulioje wa karama.<br />
Kukutana na Mtume kwenye membari.<br />
4. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alisimama kwenye<br />
membari kutoa waadhi. Mara akashuka na akasimama kimya<br />
kitambo hivi kwa adabu na heshima. Baadaye akasimama na<br />
akatoa waadhi.<br />
Mara alipokwisha kutoa waadhi, watu walimwuliza<br />
yaliyomtokea. <strong>Al</strong>ijibu ya kuwa wakati ule Mtume alikuja pale na<br />
akampisha pale alipokaa. Na alipokuwa anaondoka alimwambia<br />
asimame na atoe waadhi alioukusudia.<br />
Kufuturu nyumba 70.<br />
5. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipewa taarifa na watu 70<br />
mablimbali, akafuturu kwao. Ulipofika wakati wa kufuturu, kila<br />
mtu alifurahi kumwona Seyyid Abdul Qadir kuhudhuria kwake.<br />
Habari hiyo ilitapakaa Baghdad nzima. Lakini mmoja katika<br />
watumishi wake alikua akikanya kama<br />
16.
si kweli, kwa sababu yeye alimwona kakaa juu ya takia lake wala<br />
hakutoka. Mwisho mwenyewe SEyyid Abdul Qadir<br />
aliyathibitisha maneno wayasemayo watu kuwa ni kweli.<br />
<strong>Al</strong>imwambia yule mtumishi wake, “Ni kweli nimekwenda kufuturu<br />
kwa watu 70. mmoja mmoja”.<br />
Kumfufua maiti aliyekwisha kuoza<br />
6. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipita katika kijiji, na<br />
aliwakuta watu wawili wanashindana. Mmoja kati ya hao alikuwa<br />
Mwislam na wa Pili alikuwa Mkristo. Seyyid Abdul Qadir<br />
aliwauliza sababu ya kushindana kwao. Yule Mwislam alijibu<br />
“Huyu Mkristo eti anasema kuwa Mtume wao ni bora kuliko<br />
Mtume wetu. Na mimi nasema kuwa Mtume wetu ndiye bora<br />
zaidi”. Seyyid Abdul Qadir alimwuliza yule Mkristo. “Dalili gani<br />
uliyonayo inaonyesha kuwa Nabii Isa ni bora kuliko Nabii<br />
Muhammad (Saw)?” Yule Mkristo alijibu, “ Mtume wetu alikuwa<br />
akifufua maiti.” Tena Seyyid Abdul Qadir alimwambia Mkristo.<br />
“Mimi vilevile nafufua maiti wala si mtume, bali ni mfuasi wake<br />
tu. “Tena Seyyid Abdul Qadir. alimuliza Mkirsto, “Je nikimfufua<br />
maiti utamwamini Nabii Muhammad?” “ Ndiyo, alisema Mkristo.<br />
Tena alisema Seyyid Abdul Qadir alimwambia yule Mkristo,<br />
“Nionyeshe kaburi la mtu aliyekufa zamani.”<br />
Yule Mkristo alifuatana na Seyyid Abdul Qadir na yule<br />
kijana kwenda kwenye kaburi ambalo mwenyewe keshaoza<br />
zamani. Walipofika pale Seyyid Abdul Qadir alimuliza yule<br />
Mkristo “Mtume wenu alikuwa akiwafufua maiti wenu kwa<br />
maneneo gani?” Yule Mkristo alisema, “<strong>Al</strong>ikuwa akimsemeza<br />
maiti kwa kumwambia asimame kwa idhini ya Mungu. Seyyid<br />
Abdul Qadir alimwambia Mkristo<br />
“Mimi nitamfufua kwa idhini yangu” Mara baada ya kusema<br />
17.
Vile, Seyyid Abdul Qadir alimwambia maiti “Simama kwa idhini<br />
yangu”. Saa ile ile alitoka hali ya kuwa yu hai. Yule Mkirsto<br />
kuona vile basi hakusita ila alitoa shabaha mbiombio, na<br />
kumwamini Nabii Muhammad (Saw) mbele ya Seyyid Abdul<br />
Qadir (k.s.a).<br />
Haramia kumgeuza kuwa kutbu:<br />
7. Hekaya:-<br />
Seyyid Abdul Qadir alipokuwa anarudi Madina kwenda<br />
Baghdad, alikumbana na haramia njiani akimngojea mtu ye yote<br />
apitae amnyang‟anye vitu alivyokuwa navyo. Seyyid Abdul Qadir<br />
alipofika pale alimwuliza yule mtu, “Nani wewe?” Yule mtu<br />
alisema kuwa yeye ni haramia. Pale pale Seyyid Abdul Qadir<br />
alikashfiwa na aliona jina lake ni miongoni mwa watu waovu.<br />
Lakini yule mwizi ilimpitia katika roho yake na akawaza kuwa<br />
asiwe huyu ndiye Seyyid Abdul Qadir. Mara tu alivyofikiri vile na<br />
Seyyid Abdul Qadir alimwambia, “Mimi ndiye Abdul Qadir.” Yule<br />
mtu aliposikia vile mara alianguka chini ya miguu ya Seyyid Abdul<br />
Qadir na akasema, “Ewe Bwana wangu, Abdul Qadir kipenzi cha<br />
Mungu.” Muda ule ule Seyyid Abdul Qadir alisikia akiambiwa,<br />
“Ewe Ghawth Mtukufu, mfundishe huyo mwizi njia ya haki”. Tena<br />
Seyyid Abdul Qadir alimfundisha njia ya haki yule mwizi na<br />
mwishoni alikuwa ni mmoja katika Makutbu (Mawalii).<br />
Kusilimu kafiri kwa kuona karama za seyyid<br />
Abdul Qadir.<br />
18.
8. Hekaya:-<br />
Mtu mmoja alitamani kwenda kumzuru Seyyid Abdul<br />
Qadir, kwa wingi wa sifa zake anazozisikia. Pindi alipofika<br />
Baghdad, alipita mahali ambapo, walikuwapo farasi 40 wakila<br />
majani pasina kuchungwa. Farasi hao walikua wake Seyyid Abdul<br />
Qadir. <strong>Al</strong>ipozidi kuwaangalia aliwaona wanayo minyororo ya<br />
dhahabu na fedha na matandiko yao ni ya hariri. Basi ikamjia fikra,<br />
“<strong>Al</strong>a! Vipi Walii mkubwa kama huyu ashughulikie mambo kama<br />
haya ya kilimwengu? Haya niliyoyaona kwake hata wafalme<br />
hawana.”<br />
Yule mgeni alipata maradhi makubwa sana kabla ya kufika<br />
alikokusudia. Kwa hiyo ilimbidi afikie nyumba nyingine badala ya<br />
nyumba ya Seyyid Abdul Qadir. Madaktari wengi walikwenda<br />
kumwangalia kwa kutaka kumtibu.<br />
Mwisho alikwenda Daktari mmoja wa Kinasara ambaye<br />
alisema kama mgonjwa yule dawa yake ni maini ya Farasi wenye<br />
sifa kadha. Watu walishughulika sana kuwatafuta. Lakini<br />
aliyekuwa na Farasi hao ni Seyyid Abdul Qadir tu. Siku ya pli watu<br />
walimwendea Seyyid Abdul Qadir kumwomba. Naye aliwapa bure<br />
farasi mmoja na kunywa dawa nyingine, Yule mgonjwa alipata<br />
nafuu kidogo. Kuona vile, watu walizidi kumwendea na<br />
kumwomba tena na waliendelea mpaka farasi wote 40 wakesha.<br />
Baada ya kupoa, yule mgeni alimuaga mwenyeji wake na<br />
akaenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir na kumshukuru kwa wema<br />
aliomfanyia hata akapata nafuu. Seyyid Abdul Qadir alimwambia<br />
yule mgeni “Ewe kijana, hao farasi mimi niliwanunua kwa sababu<br />
yako wewe; kwa kuona unayo mapenzi makubwa juu yangu. Na<br />
ulipotia azma ya kuja kunizuru mimi nilijua kama utaumwa na<br />
dawa yako ni maini ya farasi. Lakini wewe pale ulipopita karibu<br />
yao na ukawaona, roho yako iliharibika na ukaleta fikra mbaya juu<br />
yangu.” Tena yule kijana alimwomba msamaha na kumtaka radhi<br />
kwa tukio hilo.<br />
19.
Seyyid Abdbul Qadir alimwita yule Daktari Mnasara akampa ile<br />
minyororo ya dhahabu pamoja na yale matandiko ya hariri. Pale<br />
yule Mnasara alisilimu mbele ya Sheikh Seyyid Abdul Qadir kwa<br />
kuona mambo ya siri na karama zake.<br />
Kufuturu chakula cha peponi:<br />
9. Hekaya:-<br />
Seyyid Abdul Qadir alikaa Riadha siku 40 kwa kufanya<br />
Ibada. Siku zote hizo alikuwa ndani ya Siami (funga). Ilimpitia<br />
rohoni mwake kutokufuturu kitu chochote isipokuwa maji mpaka<br />
Mwenyezi Mungu amteremshie chakula cha peponi.<br />
Ilipofika siku ya 38, aliona sakafu ya nyumba inapasuka na<br />
alimwona mtu mwenye birika ya dhahabu katika mkono mmoja na<br />
katika mkono wa pili alikuwa amechukua sahani ya fedha yenye<br />
matunda. Tena hivyo vitu aliviweka mbele ya Seyyid Abdul Qadir.<br />
Seyyid Abdul Qadir aliuliza, “Vitu gani hivi?” Yule<br />
mtumishi alijibu, “Hivyo ni vyakula nimepewa nikuletee.” Seyyid<br />
Abdul Qadir alisema: “Mtume amekataza kulia vyombo vya<br />
dhahabu na fedha. Viondoe hivyo vitu“. Yule Rohani alitoka mbio<br />
na vyombo vyake. Lakini ulipofika wakati wa kufuturu, alishuka<br />
Malaika na sahani iliyojaaa chakula. Yule Malaika alisema: “Ewe<br />
Ghawthil-A`adham, hii ni dhifa yako inayotoka kwa Mwenyezi<br />
Mungu. Seyyid Abdbul Qadir alipokea kile chakula akala yeye<br />
pamoja na wengi wa marafiki zake. Na Mwenyezi Mungu<br />
humruzuku amtakae pasina kudhani kama ataipata riziki hiyo kwa<br />
muda huo.<br />
20.
Mtoto wa kike kugeuka mwanaume.<br />
10.Hekaya:-<br />
Mtu mmoja alimwendea Seyyid Abdul Qadir kumtaka<br />
amuombee dua ili apate mtoto mwanamme. Ghawth alijibu,<br />
“Nimeshakuombea kwa Mungu na atakupa huyo umtakaye”. Yule<br />
Bwana alimpata mtoto, lakini alikuwa mwanamke. Kwa hivyo<br />
alimchukua mpaka kwa Sheikh na kumwambia, “Mimi nilimtaka<br />
mtoto wa kiume, si wa kike”. Seyyid Abdul Qadir alisema: “Basi<br />
mfunike nguo na umrudishe nyumbani, utaona yatakayotokea“.<br />
Mara tu alipofika nyumbani alimwona yule mtoto wa kike<br />
amegeuka kuwa mtoto wa kiume. Kama alivyotaka hasa.<br />
Tajiri kuwaona ngamia wake waliopotea:<br />
11. Hekaya:-<br />
Siku moja Tajiri mmoja alikuwa akisubiri msafara ili<br />
afuatane nao kwenda kufamya biashara. <strong>Al</strong>ikuwa na ngamia 6<br />
ambao amewatwisha magunia ya sukari.<br />
Walipofika katikati ya njia. Ngamia wake walipotea pamoja<br />
na mizigo yao. <strong>Al</strong>iwatafuta sana, lakini hakuwaona. Basi akapiga<br />
ukelele, “Ewe Seyyid Abdul Qadir, ngamia wangu wamepotea<br />
pamoja na mizigo yao”. Kutazama mbele yake alimwona mtu<br />
amevaa nguo nyeupe anampungia mkono, <strong>Al</strong>ipokwenda kule<br />
hakumwona yule mtu bali aliwaona wale ngamia wake pamoja na<br />
mizigo yao.<br />
Ndege kusikiliza maneno:<br />
21.
12. Hekaya:-<br />
Siku moja alikaa Seyyid Abdul Qadir, anazungumza. Basi<br />
akasema: “Lau kama Mwenyezi Mungu angetaka kumleta Ndege<br />
rangi ya kijani kusikilza maneno yangu, basi angekuja”. Baada ya<br />
kumaliza kusema hivi, mara alitokea ndege mzuri wa rangi ile ile<br />
ya kijani. <strong>Al</strong>iingia ndani ya mkono wa kanzu yake kusikiliza<br />
maneno wala hakonekana tena mahala alikokwenda.<br />
Kukatika ndege vipande vipande:<br />
13. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Andul Qadir alikuwa akizungumza, Mara<br />
akaja ndege mzuri wa rangi ya kijani akatua mbele yake ili<br />
kusikiliza maneno yake. Seyyid Abdul Qadir akasma, “Lau<br />
ningemwambia huyu ndege kufa na kukatika vipande vipande basi<br />
angalikufa.” Basi pale pale alianguka na akakatika vipande.<br />
Kuhujumiwa simba mbele ya banda la farasi<br />
14. Hekaya:-<br />
<strong>Al</strong>ikuwapo Walii mmoja jina lake Sheikh Ahmad<br />
Zamdah. Sheikh Ahmad alikuwa akipanda simba na kutembea<br />
naye anapokwenda kwa Mawalii wengine. Pale anapofika humtaka<br />
mwenyeji wake ampe Ng‟ombe mmoja, yaani chakula cha simba<br />
wake. Siku moja yule Sheikh Ahmad alifika Baghdad na akaenda<br />
kwa Seyyid Abdul Qadir.<br />
22.
Basi akamwambia: “Mimi ninayo desturi, pahala ninapofika<br />
hupewa ng‟ombe na kumpa Simba wangu ale, Sasa unasemaje?”<br />
“Nitampa ng‟ombe anayevuta maji”. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir.<br />
<strong>Al</strong>ipokuwa anakwenda kwenye ng‟ombe alipitia pale penye<br />
banda la Farasi wa Ghawth. Pale alikaa mbwa mmoja na<br />
mwanawe. <strong>Al</strong>ipopita Sheikh Ahmad walimfuata. Yule mbwa<br />
alimweka pale alipokaa simba. Mara simba alitaka kumshambulia<br />
mbwa wa Seyyid Abdul Qadir, lakini bahati mbaya mbwa<br />
alimhujumu vikali simba yule na alimwua. Tena Sheikh Ahmad<br />
alirudi kwa Seyyid Addul Qadir na kumtaka radhi kwa<br />
yaliyotokea. Vile vile alitubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />
Kifo cha ndege mia:<br />
15. Hekaya:-<br />
Ilitokea siku moja Seyyid Abdul Qadir alikaa pahala<br />
akifanya Ibada zake. Juu kikapita kikundi kikubwa cha Ndege mia.<br />
Walipomwona Seyyid Abdul Qadir wote walishuka wakatua na<br />
wakamzunguka. Pale walipokaa wakawa wanafanya kelele. Seyyid<br />
Abdul Qadir akatazama juu akasema, “Ewe Mola hawa ndege<br />
wananishughulisha hapa”. Ndege wote walikufa saa ile ile.<br />
<strong>Al</strong>ipowaona wote ni maiti alisema “Ewe Mola unajua sababu ya<br />
kifo chao”. Kusema vile mara wote walifufuka na kwenda zao.<br />
Kujitenga kwenye magofu ya baghdad:<br />
16. Hekaya:-<br />
Seyyid Abdul Qadir alijitenga kwenye magofu kwa muda<br />
23.
usiopungua miaka 25 akifanya Ibada. Siku moja alisikia sauti<br />
iliyomwambia, “Rudi Mjini watu wanakuhitaji kwa manufaa ya<br />
Akhera“. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir:- "Mimi nimekuja huku<br />
kufanya Ibaada kwa kutafuta salama ya Dini yangu, na kuepuka na<br />
fitina za Baghdad“. Kusikia vile tena akaambiwa.“Rudi na<br />
utasalimika Mungu akipenda“. Kusikia vile Seyyid Abdul Qadir<br />
alirudi huku moyo wake umejaa siri za Mungu.<br />
Maneno kujitokeza:<br />
17. Hekaya:-<br />
Kila alipokuwa akikaa Ghawth-A`adham walikuwa<br />
hawaondoki Mawalii – Iwapo amekaa kimya basi maneno hutaka<br />
kujitokeza na kufika mpaka kwenye koo. Basi yakifika hapo hua<br />
hawezi tena kunyamaza bali huwapa siri katika elimu ya “Hakika”.<br />
Unyayo wangu uko shingoni mwa kila walii:<br />
17. Hekaya:-<br />
Maneno haya alipewa idhini na Mtume kuyasema. Na siku<br />
alipoyatamka Baghdad, Mawalii wote wa Ulimwengu mzima<br />
waliyasikia na kila mmoja aliinamisha shingo yake kwa kuridhia<br />
maneno yaliyotamkwa.<br />
Yasemekana walii mmoja wa Damask, Sheikh Rasalam<br />
alisema: “Ewe Mwenyezi Mungu, ninakushuhudiza wewe na<br />
Malaika wako kuwa nimeyasikia maneno ya Bwana<br />
24.
wa Mawalii na nimeyakaribisha. Tena akanyoosha shingo yake<br />
kuonyesha kuwa ameridhia.<br />
Nuru katika kidole chake.<br />
18.Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdbul Qadir aliondoka usiku pamoja<br />
na Masheikh watatu kwenda kuzuru kaburi la Imam Aba Hanifa,<br />
Usiku huo ulikuwa na giza kubwa sana. Hapa na hapo huwezi<br />
kupaona. Lakini Seyyid Abdul Qadir alipofika penye jiwe au mti<br />
aliashiria kwa kidole chake. Na wakati huo lile jiwe au mti<br />
hung‟ara sana mfano wa mbalamwezi kali. Waliendelea na hali<br />
hiyo mpaka wakafika walikotaka na wakafanya waliyokusudia.<br />
Wakati wa kurudi Seyyid Abdul Qadir alikuwa akiashiria<br />
kwa kidole vile vile kwenye hatari na kutoka mwanga mkali<br />
kwenye kile kitu. Tena walipofika<br />
nyumbani kwa Seyyid Abdul Qadir, wale Masheikh waliaga na<br />
wakaenda zao.<br />
Mifupa kuigeuza kuku aliye hai:<br />
19. Hekaya:-<br />
Bibi mmoja alimpeleka mwanawe kwa Seyyid Abdul<br />
Qadir kusomeshwa elimu. Mtoto huyo aliwekwa mahala maalum<br />
kazi yake ni kufanya ibada tu kabla ya kusomeshwa Ilmu.<br />
Siku moja mama yake yule mtoto kuja kumkagua. Lakini<br />
hali alivyomwona nayo mwanawe kidogo haikumpendeza.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa amedhoofu sana. <strong>Al</strong>ipita ndani ili<br />
25.
aonane na Seyyid Abduil Qadir. Kwa uchungu wa mwanawe<br />
ilimtoka subra na akawa anamwandama Seyyid Abdul Qadir kwa<br />
maneno. <strong>Al</strong>isema: “Ewe Ghawthil Aadham, unakula kuku na<br />
unamwacha mwanangu anakula vipande vya mikate ya shairi hata<br />
amekuwa mwembamba kama uzi?“ Seyyid Abdul Qadir hakujibu<br />
chochote isipokuwa aliikusanya ile mifupa na akasema mbele ya<br />
yule mwanamke: “Ewe kuku simama kwa idhini ya Mungu<br />
mwenye kuhusisha mifupa iliyochakaa,” Mara tu baada ya kusema<br />
vile mifupa iligeuka kuku ambaye alisimama mbele ya yule<br />
mwanamke.<br />
Naam hapo Seyyid Abdul Qadir ndipo alipomneneza yule<br />
mwanamke kwa kusema: “Ninapenda mwanao aweze kama haya,<br />
kwa kupata daraja kama hili, anaweza kula chakula chochote<br />
akitakacho mwenyewe”. Mwisho yule bibi alimtaka radhi Seyyid<br />
Abdulm Qadir na akamwambia, “Ewe Seyyid Abdul Qadir,<br />
yaliyonipelekea kusema hayo ni uchungu wa mwanangu tu. Na<br />
tangu sasa hivi nakupa uhuru ufanye utakavyo juu ya mtoto huyo.”<br />
20. Hekaya:-<br />
Kushiba kwa kufyonza kidole:<br />
Sheikh Muhammad Shawry Sabty aliondoka Misri<br />
kwenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir. <strong>Al</strong>ikaa huko kwa siku<br />
nyingi. Sheikh Muhammad alipofunga safari ya kwenda nyumbani,<br />
alipewa wosia na Seyyid Abdul Qadir. Wosia wenyewe ni huu:<br />
"Usitake haja kwa mtu yeyote.“ Baada ya kuusiwa alipewa zawadi<br />
na vyakula vya kula anapokuwa safarini.<br />
Lakini kabla ya kuondoka Seyyid Abdul Qadir alikitia<br />
kidole chake ndani ya kinywa cha Sheikh Muhammad na<br />
akamwambia akifyonze. Baada ya kufanya hivyo tena<br />
26.
akashika njia akaenda zake. Jambo la kustaajabisha ni kuona kuwa<br />
Sheikh Muhammad hakushikwa na njaa wala kiu mpaka akafika<br />
kwake Misri. Na alipokitizama kile chakula alikiona kimeongezeka<br />
wala hakikuharika. Baada ya kupumzika alikula chakula hicho<br />
pamoja na watoto wake na Watu waliokuja kuonana naye.<br />
Kifo cha seyyid Abdul Qadir (Qsa):<br />
Seyyid Abdul Qadir alikufa siku ya Ijumaa, Mfungo saba,<br />
mwaka 561 (A.H). <strong>Al</strong>izikwa kwenye chuo chake<br />
“ Babuluzji”. Kafa na umri wa miaka 91.<br />
Watu wengi walimimminika mazikoni kwake, utasema<br />
labda wanakwenda Arafa kwa vile watu walivyokuwa wengi<br />
ilionekana ni bora zaidi awekwe ili azikwe usiku. Pamoja na hayo<br />
hakubakia mtu yeyote katika Baghdad ila alihudhuria Maziko<br />
yake. Katika majia, masoko na majumba yote yalijaa watu.<br />
Seyyid Abdul Qadir alisalishwa na mwanawe Sheikh<br />
Abdul Wahab na alisaliwa na watu wengi mno; Miongoni mwao<br />
ni wanawe, wanfunzi wake na marafiki zake. Kifo chake Seyyid<br />
Abdul Qadir kilitokea katika zama za Imam Yusufu bin<br />
Muktafa. Wale watu waliokosa kumsalia Sheikh, walipewa nafasi<br />
ya kumsalia wakati wa mchana ulipofunguliwa mlango.<br />
27.
Jihad:<br />
Kwa yeyote anayetaka kutabaruk katika Jihad hii ya<br />
kuchangia katika kuchapisha vitabu vya Dhikri, Tawwasul n.k.<br />
Kwa kuwa hiki ni toleo la kwanza, tunategemea kutoa matoleo<br />
zaidi. Awasiliane na mtunzi wa kitabu hiki moja kwa moja kupitia<br />
simu namba: 0755 547 771 au aitie michango yake kwenye<br />
Account ya Benk:<br />
NMB – CLOCK TOWER A/C. 4082300209. ARUSHA.<br />
TWARIQATUL QADIRIA ARRAZZIKIA JAILANIA.<br />
MAKAO MAKUU<br />
ZAWIA KUU.<br />
P. O. BOX 8105<br />
ARUSHA.<br />
Wabillahit Tawfiq.<br />
28.
Swahib Sujjada:<br />
KIMETOLEWA NA:-<br />
Mtungaji:-<br />
<strong>Al</strong> Habib Sheikh Salim Bin Mbarak.<br />
(Dar-wesh – Mti mkavu)<br />
P.O. Box 8105,<br />
Zawia kuu.<br />
Arusha - Tanzania.<br />
(E.A)