Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
UTANGULIZI:<br />
“Assalamu alay–kum warah–matullahi –Taala wabarakatuh”.<br />
Namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kunijaalia fikra<br />
na utashi wa kuandika kitabu hiki nilichokitambulisha kwa jina la<br />
Ghawth–l–A`adham, Seyyid Sheikh – Abdul – Qadir-Jaylani.<br />
(Qad-sa-Llahu-Siral-A`ziz)<br />
Makusudio yangu makubwa katika kuandika kitabu hiki ni<br />
kuelezea sifa na mwenendo wa maisha ya Bwana wa Mawalii na<br />
kipenzi cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume (Saw).<br />
Ni Matarajio yetu Historia hii tuliyoiandika ndani ya kitabu<br />
hiki itahifadhika na kujenga kumbukumbu juu ya maisha ya watu<br />
wema kwa ujumla. Kuwakumbuka watu wema na kufuatisha<br />
matendo mema ni ufunguo wa kheri hapa duniani na Akhera.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mwenyezi Mungu amjaalie kila la kheri msomaji<br />
wa kitabu hiki na amjaalie kuwa na matendo mema.<br />
“Eee Mwenyezi Mungu tujaalie sote<br />
mwishilio mwema na utujaalie kuwa<br />
watu wa peponi”<br />
(Aamiin).<br />
Sheikh Salim Ibn Mbarak – (Dar-weish – Mti Mkavu).<br />
S.L.P 8105<br />
Zawiya Kuu – Arusha.<br />
Tanzania (E.A).<br />
vii.