08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

xv. Sifa za Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa karim sana na mwenye sifa na<br />

tabia nzuri za kupigiwa mfano. <strong>Al</strong>ikuwa na kimo cha wastani, si<br />

mrefu sana wa kuchusha wala hakuwa mfupi. <strong>Al</strong>ikuwa mwekundu<br />

wa weupe. <strong>Al</strong>ikuwa na nyusi nzuri sana. Mwili wake ulikuwa<br />

mwembamba, macho yake yalikuwa yenye haiba kubwa. Kifua<br />

chake kilikuwa kipana chenye Ilmu nyingi. <strong>Al</strong>ikuwa mkali kama<br />

babu yake Sayyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib. Ama ndevu zake zilikua<br />

ndefu namna zile za Nabii Harun (As).<br />

Seyyid Abdul Qadir alikua na cheo au makamo matukufu<br />

mbelel ya Mwenyezi Mungu. Katika Ulimwengu alikuwa ni mtu<br />

mwenye kusikilizwa sana sauti. Sauti yake iliokuwa nzuri na<br />

nyororo kama lulu. Anaposema husema upesi upesi. Hakupata<br />

kupenga makamasi wala kutema makohozi. Mwisho inzi hakupata<br />

kumtua juu ya mwili wake.<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa mnyenyekvu na mkweli.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa na kawaida ya kumtolea mtu salamu mwanzo kila<br />

wanapokutana naye.<br />

Aidha alikuwa akikaa na maskini kama alivyokuwa<br />

akifanya Nabii Muhammad (Saw). Pamoja na utukufu aliokuwa<br />

nao, alikuwa akiwasimamia watoto wadogo na alikuwa<br />

akiwatukuza watu wazima kama ilivyokuwa ada yake Mtume<br />

(Saw). Ingawa alikuwa akiwasimamia watoto lakini hakupata<br />

kumsimamia mtu yeyote katika watu watukufu.<br />

Seyyid Abdul Qadir hakupata kugonga mlango wa<br />

Mfalme au waziri yeyote kwa kumtaka haja ya kilimwengu.<br />

Kazi yake ilikuwa ni kuamrisha mema na kukataza maovu.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa akila na wageni na marafiki zake.<br />

Kadhalika alikuwa akiwapa nguo na chakula maskini.<br />

Vile vile alikuwa akiwapa zawadi nzuri nzuri wanapomwendea<br />

kwake. Kwa ukarimu wake hakupata kumrejesha mtu yeyote<br />

aliyemwomba wakati wa shida, seuze wakati wa raha.<br />

11.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!