You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
xv. Sifa za Seyyid Abdul Qadir (Qsa).<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa karim sana na mwenye sifa na<br />
tabia nzuri za kupigiwa mfano. <strong>Al</strong>ikuwa na kimo cha wastani, si<br />
mrefu sana wa kuchusha wala hakuwa mfupi. <strong>Al</strong>ikuwa mwekundu<br />
wa weupe. <strong>Al</strong>ikuwa na nyusi nzuri sana. Mwili wake ulikuwa<br />
mwembamba, macho yake yalikuwa yenye haiba kubwa. Kifua<br />
chake kilikuwa kipana chenye Ilmu nyingi. <strong>Al</strong>ikuwa mkali kama<br />
babu yake Sayyidna <strong>Al</strong>i bin Abi Talib. Ama ndevu zake zilikua<br />
ndefu namna zile za Nabii Harun (As).<br />
Seyyid Abdul Qadir alikua na cheo au makamo matukufu<br />
mbelel ya Mwenyezi Mungu. Katika Ulimwengu alikuwa ni mtu<br />
mwenye kusikilizwa sana sauti. Sauti yake iliokuwa nzuri na<br />
nyororo kama lulu. Anaposema husema upesi upesi. Hakupata<br />
kupenga makamasi wala kutema makohozi. Mwisho inzi hakupata<br />
kumtua juu ya mwili wake.<br />
Seyyid Abdul Qadir alikuwa mnyenyekvu na mkweli.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa na kawaida ya kumtolea mtu salamu mwanzo kila<br />
wanapokutana naye.<br />
Aidha alikuwa akikaa na maskini kama alivyokuwa<br />
akifanya Nabii Muhammad (Saw). Pamoja na utukufu aliokuwa<br />
nao, alikuwa akiwasimamia watoto wadogo na alikuwa<br />
akiwatukuza watu wazima kama ilivyokuwa ada yake Mtume<br />
(Saw). Ingawa alikuwa akiwasimamia watoto lakini hakupata<br />
kumsimamia mtu yeyote katika watu watukufu.<br />
Seyyid Abdul Qadir hakupata kugonga mlango wa<br />
Mfalme au waziri yeyote kwa kumtaka haja ya kilimwengu.<br />
Kazi yake ilikuwa ni kuamrisha mema na kukataza maovu.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa akila na wageni na marafiki zake.<br />
Kadhalika alikuwa akiwapa nguo na chakula maskini.<br />
Vile vile alikuwa akiwapa zawadi nzuri nzuri wanapomwendea<br />
kwake. Kwa ukarimu wake hakupata kumrejesha mtu yeyote<br />
aliyemwomba wakati wa shida, seuze wakati wa raha.<br />
11.