08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kuwasalisha Mawalii hewani:<br />

2. Hekaya:-<br />

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitafutwa na<br />

Masheikh wa Baghdad wa Twariqa ya Fawqany. Waliambiwa<br />

kama amekwenda upande wa Mto Tigris. Huko walimwona<br />

anakwenda juu ya maji na huku samaki wa mle mtoni<br />

wanamwendea makundi makundi wakimtolea salam na wakimbusu<br />

mkono wake kwa mboni za macho yao.<br />

Mara tu waliponyanyua macho yao juu waliliona zulia<br />

kubwa rangi ya kijani lililopambwa kwa dhahabu na fedha yenye<br />

kung‟aa. Mtu yeyote akiliangalia atadhania kama labda ni lile zulia<br />

la Nabii Suleiman. Na pale juu ya zulia palikuwa na kitabu<br />

kielezacho utukufu wa Sayyid Abdul Qadir. (Q.s.a).<br />

Ulipoingia wakati wa Adhuhuri kiasi cha saa 6.30; wale<br />

Masheikh wa Baghdad waliwaona Mawalii wengi sana<br />

wamefuatana na wakubwa wao wanakwenda kwenye zulia. Na<br />

pale penye zulia walikuwa wamekaa “Rijalul – ghayb” (Mawalii)<br />

na mkubwa wao yuko mbele. Ulipofika wakati wa kusali, yule mtu<br />

aliyekaa mbele; alikimu Sala na walisimama Mawalii wote huku<br />

wakitazamana nani atakayesalisha. Mara alipita mbele Seyyid<br />

Abdul Qadir kusalisha. <strong>Al</strong>iwasalisha wale Mawalii pamoja na<br />

mkubwa wao, pamoja na Masheikh wa Baghdad na mkubwa wao.<br />

Baada ya kusali Seyyid Abdul Qadir alinyanyua mikono yake juu<br />

kuomba. <strong>Al</strong>iomba hivi:- “Ewe Mola Mtukufu, ninakuomba<br />

asife Murid wangu mwanamume au mwanamke mwenye<br />

kunipenda ila awe ametubia kwa Mola wake”. Baada ya<br />

kuomba, walisikia Malaika wakiitikia “Amiin”. Na walisikia sauti<br />

isemayo:<br />

“Furahi, hakika nimeikubali dua yako”.<br />

Hakika Mungu ndiye Mtukufu, na humpa utukufu yeyote<br />

amtakaye. Heri iliyoje ya kumwomba Mungu na akakujibu papo<br />

kwa papo.<br />

15.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!