Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kuwasalisha Mawalii hewani:<br />
2. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitafutwa na<br />
Masheikh wa Baghdad wa Twariqa ya Fawqany. Waliambiwa<br />
kama amekwenda upande wa Mto Tigris. Huko walimwona<br />
anakwenda juu ya maji na huku samaki wa mle mtoni<br />
wanamwendea makundi makundi wakimtolea salam na wakimbusu<br />
mkono wake kwa mboni za macho yao.<br />
Mara tu waliponyanyua macho yao juu waliliona zulia<br />
kubwa rangi ya kijani lililopambwa kwa dhahabu na fedha yenye<br />
kung‟aa. Mtu yeyote akiliangalia atadhania kama labda ni lile zulia<br />
la Nabii Suleiman. Na pale juu ya zulia palikuwa na kitabu<br />
kielezacho utukufu wa Sayyid Abdul Qadir. (Q.s.a).<br />
Ulipoingia wakati wa Adhuhuri kiasi cha saa 6.30; wale<br />
Masheikh wa Baghdad waliwaona Mawalii wengi sana<br />
wamefuatana na wakubwa wao wanakwenda kwenye zulia. Na<br />
pale penye zulia walikuwa wamekaa “Rijalul – ghayb” (Mawalii)<br />
na mkubwa wao yuko mbele. Ulipofika wakati wa kusali, yule mtu<br />
aliyekaa mbele; alikimu Sala na walisimama Mawalii wote huku<br />
wakitazamana nani atakayesalisha. Mara alipita mbele Seyyid<br />
Abdul Qadir kusalisha. <strong>Al</strong>iwasalisha wale Mawalii pamoja na<br />
mkubwa wao, pamoja na Masheikh wa Baghdad na mkubwa wao.<br />
Baada ya kusali Seyyid Abdul Qadir alinyanyua mikono yake juu<br />
kuomba. <strong>Al</strong>iomba hivi:- “Ewe Mola Mtukufu, ninakuomba<br />
asife Murid wangu mwanamume au mwanamke mwenye<br />
kunipenda ila awe ametubia kwa Mola wake”. Baada ya<br />
kuomba, walisikia Malaika wakiitikia “Amiin”. Na walisikia sauti<br />
isemayo:<br />
“Furahi, hakika nimeikubali dua yako”.<br />
Hakika Mungu ndiye Mtukufu, na humpa utukufu yeyote<br />
amtakaye. Heri iliyoje ya kumwomba Mungu na akakujibu papo<br />
kwa papo.<br />
15.