08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Ama masomesho yake yalizidi kupatia utukufu. Kwani Bibi<br />

mmoja alijitolea nafsi yake aolewe na Seyyid Abdul Qadir bila<br />

mahari yoyote, isipokuwa alimpa sharti moja, nayo ni<br />

kuwasomosha watu Ilmu kwa muda maalum. Muda ulipotimia,<br />

Bibi yule aliolewa kama alivyotamani.<br />

X. Kusomesha kwake Ilmu:<br />

Katika chuo chake, Seyyid Abdul Qadir alikuwa<br />

akisomesha Ilmu 13 za sheria. Na katika Ilmu hizo 13, aliweka<br />

darsa moja kusomesha Madhehebu mbalimbali na darsa nyinginezo<br />

alikuwa akisomesha Hitilafu za Wanachuoni. Baada ya sala ya<br />

<strong>Al</strong>fajiri, alikuwa akisomesha Tafsir ya Qur an na akisomesha<br />

Hadithi za Mtume (Saw) Darsa hizo zilikuwa zikisomwa na kila<br />

mtu aliyetaka. Ama Ilmu za Madhehebu mbalimbali, Khitilafu za<br />

Wanachuoni, Adabu, Fiq na Usuli Dini zilikuwa zikismwa na<br />

Mawalii tu.<br />

Wakati wa Adhuhuri, ilikuwa ikisomwa Qur an kwa Kiraa<br />

(visomo) 7. Darsa ilikuwa ikihudhuriwa na wanafunzi 650<br />

waliokuwa mahodari sana. Wasomaji wake wakubwa wa Qur ani<br />

walikuwa Sheikh Masoud al Hashimiy na Sheikh Abdul Wahab bin<br />

Abdul Qadir (mwanawe).<br />

xi. Kufutu kwake masuala<br />

Katika fatwa zake, Sheikh alikuwa halazi suala wala<br />

alikuwa hafikiri, Bali alikuwa hanafutu mara moja tu. Kabla ya<br />

kufutu au kujibu suala yoyote, ilikuwa ikisomwa Qur an. Jawabu<br />

zake zilikuwa ama za kuandika au za mdomo. Na jawabu zake<br />

zilikuwa zikiwafurahisha watu kwa ustadi wake.<br />

7.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!