Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Ama masomesho yake yalizidi kupatia utukufu. Kwani Bibi<br />
mmoja alijitolea nafsi yake aolewe na Seyyid Abdul Qadir bila<br />
mahari yoyote, isipokuwa alimpa sharti moja, nayo ni<br />
kuwasomosha watu Ilmu kwa muda maalum. Muda ulipotimia,<br />
Bibi yule aliolewa kama alivyotamani.<br />
X. Kusomesha kwake Ilmu:<br />
Katika chuo chake, Seyyid Abdul Qadir alikuwa<br />
akisomesha Ilmu 13 za sheria. Na katika Ilmu hizo 13, aliweka<br />
darsa moja kusomesha Madhehebu mbalimbali na darsa nyinginezo<br />
alikuwa akisomesha Hitilafu za Wanachuoni. Baada ya sala ya<br />
<strong>Al</strong>fajiri, alikuwa akisomesha Tafsir ya Qur an na akisomesha<br />
Hadithi za Mtume (Saw) Darsa hizo zilikuwa zikisomwa na kila<br />
mtu aliyetaka. Ama Ilmu za Madhehebu mbalimbali, Khitilafu za<br />
Wanachuoni, Adabu, Fiq na Usuli Dini zilikuwa zikismwa na<br />
Mawalii tu.<br />
Wakati wa Adhuhuri, ilikuwa ikisomwa Qur an kwa Kiraa<br />
(visomo) 7. Darsa ilikuwa ikihudhuriwa na wanafunzi 650<br />
waliokuwa mahodari sana. Wasomaji wake wakubwa wa Qur ani<br />
walikuwa Sheikh Masoud al Hashimiy na Sheikh Abdul Wahab bin<br />
Abdul Qadir (mwanawe).<br />
xi. Kufutu kwake masuala<br />
Katika fatwa zake, Sheikh alikuwa halazi suala wala<br />
alikuwa hafikiri, Bali alikuwa hanafutu mara moja tu. Kabla ya<br />
kufutu au kujibu suala yoyote, ilikuwa ikisomwa Qur an. Jawabu<br />
zake zilikuwa ama za kuandika au za mdomo. Na jawabu zake<br />
zilikuwa zikiwafurahisha watu kwa ustadi wake.<br />
7.