Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Juu ya kuwa wamo ndani ya safari pamoja, Seyyid Abdul<br />
Qadir kabisa alikuwa hamjui mtu anayefuatana naye. Lakini alikuja<br />
kumjua baadaye hapo alipokwenda Baghdad kumkagua.<br />
Seyyid Abdul Qadir alisoma kwa juhudi na ari kubwa na<br />
aliwashinda wenzake wote kwa Ilmu na ufasaha wa lugha. Na<br />
alikuwa jogoo mkubwa wa Madhehebu ya Shafi na Hambali. Na<br />
alikuwa akijibu na akifutu masuali kwa Madhehebu hayo mawili.<br />
Lakini yeye mwenyewe alikuwa akifuata madhehebu ya Hambal.<br />
vi. Katika baadhi ya Ilmu alizosoma.<br />
(i) Qur an (Tafsiri)<br />
(ii) Fiqh<br />
(iii) Hadith<br />
(iv) Usuli-fiq<br />
(v) Tarikh (historia)<br />
(vi) Tasawuf<br />
(vii) Lugha. n.k.<br />
vii. Masheikh zake:<br />
Seyyid Abdul Qadir amesoma Ilmu kwa Masheikh wengi<br />
na kila mmoja katabahari katika fanni mbalimbali. Masheikh<br />
wenyewe ni:-<br />
1 Sheikh Abdil-Wafa <strong>Al</strong>i Bin Ukayl.<br />
2. Sheikh Abi Said-al-Mubaraq.<br />
3. Sheikh Abdil Khatib Mahfudh<br />
Kaludhany.<br />
4.