Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kumbusu mtume mkono wake.<br />
3. Hekaya:<br />
Seyyid Abdul Qadir alipokwenda Madina kumzuru Mtume<br />
(Saw) muda wa siku 40 alisimama mbele ya kaburi. Ilipotimia siku<br />
ya 40 alimwomba autoe mkono wake nje (kutoka kaburini) ili<br />
aubusu. Pale pale Mtume (Saw) aliutoa mkono wake na Seyyid<br />
Abdul Qadir aliushika na kuubusu. Tena alijiwekea juu ya kichwa<br />
chake. <strong>Al</strong>hamdulillah, utukufu ulioje wa karama.<br />
Kukutana na Mtume kwenye membari.<br />
4. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alisimama kwenye<br />
membari kutoa waadhi. Mara akashuka na akasimama kimya<br />
kitambo hivi kwa adabu na heshima. Baadaye akasimama na<br />
akatoa waadhi.<br />
Mara alipokwisha kutoa waadhi, watu walimwuliza<br />
yaliyomtokea. <strong>Al</strong>ijibu ya kuwa wakati ule Mtume alikuja pale na<br />
akampisha pale alipokaa. Na alipokuwa anaondoka alimwambia<br />
asimame na atoe waadhi alioukusudia.<br />
Kufuturu nyumba 70.<br />
5. Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipewa taarifa na watu 70<br />
mablimbali, akafuturu kwao. Ulipofika wakati wa kufuturu, kila<br />
mtu alifurahi kumwona Seyyid Abdul Qadir kuhudhuria kwake.<br />
Habari hiyo ilitapakaa Baghdad nzima. Lakini mmoja katika<br />
watumishi wake alikua akikanya kama<br />
16.