You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
8. Hekaya:-<br />
Mtu mmoja alitamani kwenda kumzuru Seyyid Abdul<br />
Qadir, kwa wingi wa sifa zake anazozisikia. Pindi alipofika<br />
Baghdad, alipita mahali ambapo, walikuwapo farasi 40 wakila<br />
majani pasina kuchungwa. Farasi hao walikua wake Seyyid Abdul<br />
Qadir. <strong>Al</strong>ipozidi kuwaangalia aliwaona wanayo minyororo ya<br />
dhahabu na fedha na matandiko yao ni ya hariri. Basi ikamjia fikra,<br />
“<strong>Al</strong>a! Vipi Walii mkubwa kama huyu ashughulikie mambo kama<br />
haya ya kilimwengu? Haya niliyoyaona kwake hata wafalme<br />
hawana.”<br />
Yule mgeni alipata maradhi makubwa sana kabla ya kufika<br />
alikokusudia. Kwa hiyo ilimbidi afikie nyumba nyingine badala ya<br />
nyumba ya Seyyid Abdul Qadir. Madaktari wengi walikwenda<br />
kumwangalia kwa kutaka kumtibu.<br />
Mwisho alikwenda Daktari mmoja wa Kinasara ambaye<br />
alisema kama mgonjwa yule dawa yake ni maini ya Farasi wenye<br />
sifa kadha. Watu walishughulika sana kuwatafuta. Lakini<br />
aliyekuwa na Farasi hao ni Seyyid Abdul Qadir tu. Siku ya pli watu<br />
walimwendea Seyyid Abdul Qadir kumwomba. Naye aliwapa bure<br />
farasi mmoja na kunywa dawa nyingine, Yule mgonjwa alipata<br />
nafuu kidogo. Kuona vile, watu walizidi kumwendea na<br />
kumwomba tena na waliendelea mpaka farasi wote 40 wakesha.<br />
Baada ya kupoa, yule mgeni alimuaga mwenyeji wake na<br />
akaenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir na kumshukuru kwa wema<br />
aliomfanyia hata akapata nafuu. Seyyid Abdul Qadir alimwambia<br />
yule mgeni “Ewe kijana, hao farasi mimi niliwanunua kwa sababu<br />
yako wewe; kwa kuona unayo mapenzi makubwa juu yangu. Na<br />
ulipotia azma ya kuja kunizuru mimi nilijua kama utaumwa na<br />
dawa yako ni maini ya farasi. Lakini wewe pale ulipopita karibu<br />
yao na ukawaona, roho yako iliharibika na ukaleta fikra mbaya juu<br />
yangu.” Tena yule kijana alimwomba msamaha na kumtaka radhi<br />
kwa tukio hilo.<br />
19.