Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
usiopungua miaka 25 akifanya Ibada. Siku moja alisikia sauti<br />
iliyomwambia, “Rudi Mjini watu wanakuhitaji kwa manufaa ya<br />
Akhera“. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir:- "Mimi nimekuja huku<br />
kufanya Ibaada kwa kutafuta salama ya Dini yangu, na kuepuka na<br />
fitina za Baghdad“. Kusikia vile tena akaambiwa.“Rudi na<br />
utasalimika Mungu akipenda“. Kusikia vile Seyyid Abdul Qadir<br />
alirudi huku moyo wake umejaa siri za Mungu.<br />
Maneno kujitokeza:<br />
17. Hekaya:-<br />
Kila alipokuwa akikaa Ghawth-A`adham walikuwa<br />
hawaondoki Mawalii – Iwapo amekaa kimya basi maneno hutaka<br />
kujitokeza na kufika mpaka kwenye koo. Basi yakifika hapo hua<br />
hawezi tena kunyamaza bali huwapa siri katika elimu ya “Hakika”.<br />
Unyayo wangu uko shingoni mwa kila walii:<br />
17. Hekaya:-<br />
Maneno haya alipewa idhini na Mtume kuyasema. Na siku<br />
alipoyatamka Baghdad, Mawalii wote wa Ulimwengu mzima<br />
waliyasikia na kila mmoja aliinamisha shingo yake kwa kuridhia<br />
maneno yaliyotamkwa.<br />
Yasemekana walii mmoja wa Damask, Sheikh Rasalam<br />
alisema: “Ewe Mwenyezi Mungu, ninakushuhudiza wewe na<br />
Malaika wako kuwa nimeyasikia maneno ya Bwana<br />
24.