08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

huyu atakuwa na mambo matukufu<br />

atakayosifiwa mwishoni kwake”.<br />

(iii). Bishara ya Mtume aliyompa Baba yake<br />

usingizini - “kwamba atamzaa mtoto ambaye<br />

atakuwa na mambo matukufu atakayosifiwa<br />

mwishoni kwake”.<br />

v. Kutafuta Ilmu:<br />

Seyyid Abdul Qadir alipotimia miaka 18, alimwomba<br />

ruhusa mama yake kusafiri kwa kutafuta Ilmu ambayo ni wajibu<br />

kwa kila Mwislamu mwanamke na mwanaume. <strong>Al</strong>iondoka kwenda<br />

Baghdad pamoja na Nabii Khidhri. Lakini kabla ya kuingia ndani<br />

ya Mji wa Baghdad; Nabii Khidhri alimpa Seyyid Abdul Qadir<br />

sharti ambalo atakapolitekeleza ndipo atapompeleka kwa Masheikh<br />

kusoma. Sharti yenyewe ni kukaa pale nje ya mji na kufanya ibada<br />

kwa muda wa miaka mitatu kamili. Seyyid Abdul Qadir alikubali.<br />

Tangu siku ile Nabii Khidhri hakupapita tena mpaka mwaka<br />

ukamalizika.<br />

Baada ya kutimia mwaka mmoja, Nabii Khidhri alikwenda<br />

kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Seyyid Abdul Qadir alipomwona<br />

Nabii Khidhri alimsimamia. Lakini Nabii Khidhri alikataa<br />

kunyanyukiwa na kumwambia akae kitako.<br />

Siri ya kuwekwa Seyyid Abdul Qadir peke yake kwa<br />

muda wote ule, apate kuitakasa roho yake na ile sehemu<br />

inayoharibiwa na Shetani. Vitisho alivyokuwa akivipata mahala<br />

pale havikuwa na mfano. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda Walii<br />

wake na akamhifadhi na kila baya na vitisho. Ulipotimia mwaka<br />

wa tatu. Nabii Khidhri alikwenda mahala pale kwa ajili ya<br />

kumchukua Seyyid Abdul Qadir.<br />

3.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!