You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
huyu atakuwa na mambo matukufu<br />
atakayosifiwa mwishoni kwake”.<br />
(iii). Bishara ya Mtume aliyompa Baba yake<br />
usingizini - “kwamba atamzaa mtoto ambaye<br />
atakuwa na mambo matukufu atakayosifiwa<br />
mwishoni kwake”.<br />
v. Kutafuta Ilmu:<br />
Seyyid Abdul Qadir alipotimia miaka 18, alimwomba<br />
ruhusa mama yake kusafiri kwa kutafuta Ilmu ambayo ni wajibu<br />
kwa kila Mwislamu mwanamke na mwanaume. <strong>Al</strong>iondoka kwenda<br />
Baghdad pamoja na Nabii Khidhri. Lakini kabla ya kuingia ndani<br />
ya Mji wa Baghdad; Nabii Khidhri alimpa Seyyid Abdul Qadir<br />
sharti ambalo atakapolitekeleza ndipo atapompeleka kwa Masheikh<br />
kusoma. Sharti yenyewe ni kukaa pale nje ya mji na kufanya ibada<br />
kwa muda wa miaka mitatu kamili. Seyyid Abdul Qadir alikubali.<br />
Tangu siku ile Nabii Khidhri hakupapita tena mpaka mwaka<br />
ukamalizika.<br />
Baada ya kutimia mwaka mmoja, Nabii Khidhri alikwenda<br />
kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Seyyid Abdul Qadir alipomwona<br />
Nabii Khidhri alimsimamia. Lakini Nabii Khidhri alikataa<br />
kunyanyukiwa na kumwambia akae kitako.<br />
Siri ya kuwekwa Seyyid Abdul Qadir peke yake kwa<br />
muda wote ule, apate kuitakasa roho yake na ile sehemu<br />
inayoharibiwa na Shetani. Vitisho alivyokuwa akivipata mahala<br />
pale havikuwa na mfano. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda Walii<br />
wake na akamhifadhi na kila baya na vitisho. Ulipotimia mwaka<br />
wa tatu. Nabii Khidhri alikwenda mahala pale kwa ajili ya<br />
kumchukua Seyyid Abdul Qadir.<br />
3.