You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Basi akamwambia: “Mimi ninayo desturi, pahala ninapofika<br />
hupewa ng‟ombe na kumpa Simba wangu ale, Sasa unasemaje?”<br />
“Nitampa ng‟ombe anayevuta maji”. <strong>Al</strong>isema Seyyid Abdul Qadir.<br />
<strong>Al</strong>ipokuwa anakwenda kwenye ng‟ombe alipitia pale penye<br />
banda la Farasi wa Ghawth. Pale alikaa mbwa mmoja na<br />
mwanawe. <strong>Al</strong>ipopita Sheikh Ahmad walimfuata. Yule mbwa<br />
alimweka pale alipokaa simba. Mara simba alitaka kumshambulia<br />
mbwa wa Seyyid Abdul Qadir, lakini bahati mbaya mbwa<br />
alimhujumu vikali simba yule na alimwua. Tena Sheikh Ahmad<br />
alirudi kwa Seyyid Addul Qadir na kumtaka radhi kwa<br />
yaliyotokea. Vile vile alitubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />
Kifo cha ndege mia:<br />
15. Hekaya:-<br />
Ilitokea siku moja Seyyid Abdul Qadir alikaa pahala<br />
akifanya Ibada zake. Juu kikapita kikundi kikubwa cha Ndege mia.<br />
Walipomwona Seyyid Abdul Qadir wote walishuka wakatua na<br />
wakamzunguka. Pale walipokaa wakawa wanafanya kelele. Seyyid<br />
Abdul Qadir akatazama juu akasema, “Ewe Mola hawa ndege<br />
wananishughulisha hapa”. Ndege wote walikufa saa ile ile.<br />
<strong>Al</strong>ipowaona wote ni maiti alisema “Ewe Mola unajua sababu ya<br />
kifo chao”. Kusema vile mara wote walifufuka na kwenda zao.<br />
Kujitenga kwenye magofu ya baghdad:<br />
16. Hekaya:-<br />
Seyyid Abdul Qadir alijitenga kwenye magofu kwa muda<br />
23.