08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

akashika njia akaenda zake. Jambo la kustaajabisha ni kuona kuwa<br />

Sheikh Muhammad hakushikwa na njaa wala kiu mpaka akafika<br />

kwake Misri. Na alipokitizama kile chakula alikiona kimeongezeka<br />

wala hakikuharika. Baada ya kupumzika alikula chakula hicho<br />

pamoja na watoto wake na Watu waliokuja kuonana naye.<br />

Kifo cha seyyid Abdul Qadir (Qsa):<br />

Seyyid Abdul Qadir alikufa siku ya Ijumaa, Mfungo saba,<br />

mwaka 561 (A.H). <strong>Al</strong>izikwa kwenye chuo chake<br />

“ Babuluzji”. Kafa na umri wa miaka 91.<br />

Watu wengi walimimminika mazikoni kwake, utasema<br />

labda wanakwenda Arafa kwa vile watu walivyokuwa wengi<br />

ilionekana ni bora zaidi awekwe ili azikwe usiku. Pamoja na hayo<br />

hakubakia mtu yeyote katika Baghdad ila alihudhuria Maziko<br />

yake. Katika majia, masoko na majumba yote yalijaa watu.<br />

Seyyid Abdul Qadir alisalishwa na mwanawe Sheikh<br />

Abdul Wahab na alisaliwa na watu wengi mno; Miongoni mwao<br />

ni wanawe, wanfunzi wake na marafiki zake. Kifo chake Seyyid<br />

Abdul Qadir kilitokea katika zama za Imam Yusufu bin<br />

Muktafa. Wale watu waliokosa kumsalia Sheikh, walipewa nafasi<br />

ya kumsalia wakati wa mchana ulipofunguliwa mlango.<br />

27.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!