Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
akashika njia akaenda zake. Jambo la kustaajabisha ni kuona kuwa<br />
Sheikh Muhammad hakushikwa na njaa wala kiu mpaka akafika<br />
kwake Misri. Na alipokitizama kile chakula alikiona kimeongezeka<br />
wala hakikuharika. Baada ya kupumzika alikula chakula hicho<br />
pamoja na watoto wake na Watu waliokuja kuonana naye.<br />
Kifo cha seyyid Abdul Qadir (Qsa):<br />
Seyyid Abdul Qadir alikufa siku ya Ijumaa, Mfungo saba,<br />
mwaka 561 (A.H). <strong>Al</strong>izikwa kwenye chuo chake<br />
“ Babuluzji”. Kafa na umri wa miaka 91.<br />
Watu wengi walimimminika mazikoni kwake, utasema<br />
labda wanakwenda Arafa kwa vile watu walivyokuwa wengi<br />
ilionekana ni bora zaidi awekwe ili azikwe usiku. Pamoja na hayo<br />
hakubakia mtu yeyote katika Baghdad ila alihudhuria Maziko<br />
yake. Katika majia, masoko na majumba yote yalijaa watu.<br />
Seyyid Abdul Qadir alisalishwa na mwanawe Sheikh<br />
Abdul Wahab na alisaliwa na watu wengi mno; Miongoni mwao<br />
ni wanawe, wanfunzi wake na marafiki zake. Kifo chake Seyyid<br />
Abdul Qadir kilitokea katika zama za Imam Yusufu bin<br />
Muktafa. Wale watu waliokosa kumsalia Sheikh, walipewa nafasi<br />
ya kumsalia wakati wa mchana ulipofunguliwa mlango.<br />
27.