Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Faida. i.<br />
Hizi Twariqa ziko namna nyingi, nazo zinapata kama 17.<br />
Katika hizo ni Qadiry, Shadhily, Nakshahabandy, Indarusy<br />
n.k.<br />
Ama Twariqa yoyote akiifuata mtu kama<br />
inavyohitajia, basi itaweza kumfikisha kwa Mwenyezi<br />
Mungu. Kwani lengo lao ni moja tu lakini kwa yote hayo<br />
niliyoeleza inapasa kupatikana Sheikh Mwongofu wa<br />
kukupa „Ijaza‟ na kukufundisha njia za kupita na kukupa<br />
wasia. Huyu mtu anayepewa „Ijaza‟ na Sheikh huitwa<br />
„Muridi‟ Kwa hivyo kila Murid ajitahidi sana kutekeleza<br />
ahadi atakazopewa na Sheikh wake.<br />
Faida ii.<br />
Yatakiwayo kwa Muridi<br />
1. Kutubia kwa Mwenyezi Mungu.<br />
2. Kufanya Ibaada kiasi ya uwezo wake.<br />
3. Kufanya mambo yalio halali<br />
4. Kuacha mambo yaliyo haramu.<br />
5. Kumdhukuru Mungu<br />
6. Kushikamamna na “Laa ila ha illa Llah” hasa baada<br />
ya kila Sala mara 165 na wakati mwngine kiasi ya<br />
kuweza kwake.<br />
7. Kusoma sana Qur an kwa kila hali.<br />
8. Kuwasamehe wenye kukuudhi.<br />
9. Kuwa mstahamilivu.<br />
10. Kuwa karimu<br />
11. Kuacha husda, kijicho, choyo, uwongo wa<br />
kuwasengenya watu.<br />
12. Kudumu na udhu.<br />
13. Kumsalia Mtume (S.a.w) kwa wingi.<br />
9.