Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
aonane na Seyyid Abduil Qadir. Kwa uchungu wa mwanawe<br />
ilimtoka subra na akawa anamwandama Seyyid Abdul Qadir kwa<br />
maneno. <strong>Al</strong>isema: “Ewe Ghawthil Aadham, unakula kuku na<br />
unamwacha mwanangu anakula vipande vya mikate ya shairi hata<br />
amekuwa mwembamba kama uzi?“ Seyyid Abdul Qadir hakujibu<br />
chochote isipokuwa aliikusanya ile mifupa na akasema mbele ya<br />
yule mwanamke: “Ewe kuku simama kwa idhini ya Mungu<br />
mwenye kuhusisha mifupa iliyochakaa,” Mara tu baada ya kusema<br />
vile mifupa iligeuka kuku ambaye alisimama mbele ya yule<br />
mwanamke.<br />
Naam hapo Seyyid Abdul Qadir ndipo alipomneneza yule<br />
mwanamke kwa kusema: “Ninapenda mwanao aweze kama haya,<br />
kwa kupata daraja kama hili, anaweza kula chakula chochote<br />
akitakacho mwenyewe”. Mwisho yule bibi alimtaka radhi Seyyid<br />
Abdulm Qadir na akamwambia, “Ewe Seyyid Abdul Qadir,<br />
yaliyonipelekea kusema hayo ni uchungu wa mwanangu tu. Na<br />
tangu sasa hivi nakupa uhuru ufanye utakavyo juu ya mtoto huyo.”<br />
20. Hekaya:-<br />
Kushiba kwa kufyonza kidole:<br />
Sheikh Muhammad Shawry Sabty aliondoka Misri<br />
kwenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir. <strong>Al</strong>ikaa huko kwa siku<br />
nyingi. Sheikh Muhammad alipofunga safari ya kwenda nyumbani,<br />
alipewa wosia na Seyyid Abdul Qadir. Wosia wenyewe ni huu:<br />
"Usitake haja kwa mtu yeyote.“ Baada ya kuusiwa alipewa zawadi<br />
na vyakula vya kula anapokuwa safarini.<br />
Lakini kabla ya kuondoka Seyyid Abdul Qadir alikitia<br />
kidole chake ndani ya kinywa cha Sheikh Muhammad na<br />
akamwambia akifyonze. Baada ya kufanya hivyo tena<br />
26.