Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
DIBAJI:<br />
Sifa zote njema zinamstahiki ALLAH ambaye<br />
amefundisha kwa wasta wa kalamu. Na akamfundisha Mwana<br />
Adam lile asilolijua. Na Rehma na Amani Zimwendee Bwana<br />
Mtume Saw na Ahly zake watukufu na Maswahaba wake watiifu.<br />
Kwa ridhaa ya mtunzi wa kitabu hiki ambae ni kiongozi<br />
mkuu na Mlezi wa Twariqatul-Qadiriya– Rrazziqiya–Jaylaniya <strong>Al</strong><br />
habib Sheikh Salim ibn Mbarak –(Dar-weish Mti mkavu) –<br />
(Radhia ALLAH Anhu). Naandika Dibaji ya kitabu hiki kwa<br />
munassaba wa kuya yakinisha yaliyomo kwenye kitabu hiki.<br />
Kwa hakika kitabu hiki kimeelezea historia na sifa kadhaa<br />
za Bwana wa Mawalii Seyyid Sheikh Abdul-Qadiri- Jaylani<br />
(Qada-sa-Llahu-Siral-Aziz)<br />
Basi ukiwa utajaaliwa kusoma kitabu hiki utamjua vilivyo<br />
alivyo Walii wa Mwenyezi Mungu na Uasili wa Twariqa kwa<br />
ujumla.<br />
Insha-<strong>Al</strong>lah tunamuomba <strong>Al</strong>lah amjaalie kila la kheri mtunzi<br />
wa kitabu hiki Sheikh Salim amjaalie Mahaba zaidi ya kudarisisha<br />
hususan kwa kutunga vitabu vingi zaidi vitavyotoa Ilmu na<br />
muongozo wa ibada za Kitwariqa kwa misingi ya Kitassawfu.<br />
Aamiin Aamiin Aamiin wal-hamdulillahi Rabbil-A`alamiin<br />
Khalifa Mohamed Omar.<br />
Mwenyekiti wa Twariqatul-Qadiriya-Rrazziqiya-<strong>Al</strong>-Jaylaniya<br />
Makao Makuu Ya Twariqa – Zawiya Kuu<br />
S.L.P. 8105<br />
Arusha.<br />
Tanzania (E.A)<br />
vi.