Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wa Mawalii na nimeyakaribisha. Tena akanyoosha shingo yake<br />
kuonyesha kuwa ameridhia.<br />
Nuru katika kidole chake.<br />
18.Hekaya:-<br />
Siku moja Seyyid Abdbul Qadir aliondoka usiku pamoja<br />
na Masheikh watatu kwenda kuzuru kaburi la Imam Aba Hanifa,<br />
Usiku huo ulikuwa na giza kubwa sana. Hapa na hapo huwezi<br />
kupaona. Lakini Seyyid Abdul Qadir alipofika penye jiwe au mti<br />
aliashiria kwa kidole chake. Na wakati huo lile jiwe au mti<br />
hung‟ara sana mfano wa mbalamwezi kali. Waliendelea na hali<br />
hiyo mpaka wakafika walikotaka na wakafanya waliyokusudia.<br />
Wakati wa kurudi Seyyid Abdul Qadir alikuwa akiashiria<br />
kwa kidole vile vile kwenye hatari na kutoka mwanga mkali<br />
kwenye kile kitu. Tena walipofika<br />
nyumbani kwa Seyyid Abdul Qadir, wale Masheikh waliaga na<br />
wakaenda zao.<br />
Mifupa kuigeuza kuku aliye hai:<br />
19. Hekaya:-<br />
Bibi mmoja alimpeleka mwanawe kwa Seyyid Abdul<br />
Qadir kusomeshwa elimu. Mtoto huyo aliwekwa mahala maalum<br />
kazi yake ni kufanya ibada tu kabla ya kusomeshwa Ilmu.<br />
Siku moja mama yake yule mtoto kuja kumkagua. Lakini<br />
hali alivyomwona nayo mwanawe kidogo haikumpendeza.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa amedhoofu sana. <strong>Al</strong>ipita ndani ili<br />
25.