08.06.2013 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Wakati huo watapata kueneza kama hajui kitu kuliko wao. Mara tu<br />

wale wanachuoni walipofika pale walikaa kitako kumsikiliza.<br />

Baada ya kukaa, Seyyid Abdul Qadir alikiimanisha kichwa chake.<br />

Na wakati huo lilimtoka pande la Nuru kifuani mwake<br />

likanyakuwa yote waliyoyadhibiti katika vifua vyao. Mara wakawa<br />

wanababaika na kuwayawaya, huku wanapiga makelele wakirarua<br />

nguo zao mfano wa wenda wazimu. Wote walivua vilemba vyao na<br />

wakamwendea Sheikh pale alipokaa. Kila mtu alikuwa akinyanyua<br />

mguu wa Seyyid Abdul Qadir na kujiwekea kichwani kwake. Hii<br />

ni ishara kuonyesha kama wameridhika na kukinai kuwa ni<br />

Mwanachuoni na amewazidi. Na kila mtu alipokuwa akifanya hayo<br />

yeye alikuwa akimkumbatia.<br />

Waliporudi vikaoni mwao, yote waliyokuwa wameyasahau<br />

wakayakumbuka tena. Seyyid Abdul Qadir alimwambia kila mtu<br />

suala aliyokusudia kuuliza na akampa jawabu nzuri ambayo hata<br />

yeye mwenyewe hakufikiria. Wote walistaajabu na walimpa heko.<br />

ix. Muda wa kutoa waadhi<br />

Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitoa waadhi mara tatu kila<br />

wiki kwa muda wa miaka 40. Masheikh, Mafaqih na wanachuoni<br />

wengi wa Baghdad walikuwa wakimiminika kumsikiliza waadhi<br />

wake.<br />

Naam, Katika jumla ya wasikilizaji wa waadhi; Mayahudi<br />

na Manasara walikuwamo.<br />

Taathira kubwa ilipatikana kila waadhi aliokuwa akiutoa<br />

kwani Mayahudi na Manasara wengi kabisa walisilimu. Na<br />

miongoni mwa Waislamu wengi wafanyao maasi walitubu katika<br />

maasi yao.<br />

6.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!