constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
101<br />
uchaguzi irudiwe. Education iwe ni ‘O’ level na awe ni mtu ambaye anatabia nzuri. Na miaka yake nayo iwe 35 mpaka 75.<br />
Hesabu ya kura ihesabiwe yote ya President, ya Local Authority na Parliament, yote ihesabiwe kwa station ile ambayo<br />
imetupiwa, after six O’ clock. Kwa hivyo hii document nimepatia Commission to peruse it for further recommendation. Thank<br />
you.Com. Ibrahim Lethome: Yeah ndivyo.<br />
Com. Ibrahim Lethome: Asante. Mugo Mwaura. Mugo Mwaura ni weweInterjection:<br />
(Inaudible)Com. Ibrahim Lethome: Nilikuwa nimekuita Haya endelea.Wilson Kimei:<br />
Kwa majina mimi ni Wilson Kimei Meli. Kwa upande wa ardhi tumeachwa nyuma sana, tumefinywa na hatuna sauti.Com.<br />
Ibrahim Lethome: Unapendekeza niniWilson Kimei: Tukipendekeza, kama Mbunge anashindwa na kuongea, awe<br />
akiokota maoni kwa wananchi. Na wananchi wawe wakipewa ruhusa kuongea katika District, na watangaze siku ambayo<br />
wataweza kutoa maoni yao. Tangu uhuru 1963 hakuna mapato tumepata. Mashamba hatukonayo, elimu hatujapata, maploti<br />
hata ikigawanywa hatupati. Tunaona kama tumeachiliwa nje na serikali na tunaona tuko nje ya serikali. Operation ikiendelea<br />
kufanywa, sisi hatuna uhuru kwa sababu tunalala watu watano hadi kumi katika nyumba moja, ambayo sio sheria Kenya.Com.<br />
Ibrahim Lethome: Lingine.Wilson Kimei: Haya nikiondoka hapo, elimu iwe ikionekana ni ya bure. Hospitali iangaliwe, ili<br />
madaktari wasifanye kazi mara mbili. Unakuta madaktari wengine wako private na bado wako kwa serikali. Halafu tena wako<br />
na store ya kuuza madawa. Hata C.I.D wa Kenya kumbe hawafanyi kazi, kama wako. Na kama wako, wanaokota maoni ya<br />
wananchi kuhusu wagonjwaCom. Ibrahim Lethome: Lingine.Wilson Kimei: Ya mwisho ni hali ya wild life katika Kenya.<br />
Yaani katika Laikipia hii, tunaona kama hatitusaidii. Mandovu yanakula mahindi.Com. Ibrahim Lethome: Unapendekeza<br />
niniWilson Kimei: Hata heri ndovu waondolewe Laikipia ili tuweze kuishi.Com. Ibrahim Lethome: Inaudible.Wilson<br />
Kimei: Eh binadamu aishi.Hali ya forest. Kama si forest, hatungekuwa na uhai, na kama tunachunga huko heri Mzungu<br />
mwenyewa aliye Kenya ahame, tupewe mashamba. Tuko squatters tunaelezwa tukate vipande kama uko na miaka ishirini.<br />
Com. Ibrahim Lethome: Wazungu waondolewe mashamba yapewe Waafrika Wilson Kimei: Yeah. Com. Ibrahim<br />
Lethome: La mwishoWilson Kimei: La mwisho. Kuna urithi ama kama mtu ameaga tunampeleka mortuary, mwiaka yote.<br />
Siku gani tutazika halafu tuwe tukiona kaburi ilikuwa hii, ilikuwa ya babu.Com. Ibrahim Lethome:Unataka nini<br />
(Inaudible) Wilson Kimei: Yaani upewe ardhi, halafu mtu akifa umzike hapo. Si ati unaenda<br />
Municipality kila siku kila siku. Na ma-plot yakigawanywa, yaangaliwe na serikali. Si ati mtu mmoja anapeleka. Pengine ni<br />
mtu wa DP, anapewa mia na anauza. Pengine ni ya Kanu anauza na raia wanakosa. Com. Ibrahim Lethome: Unataka aje<br />
Wilson Kimei: Kama DP inapewa kiwango fulani, iangikwe DP imepewa kiwango fulani. Na iandikwe namba mpaka<br />
mwisho. Si ati mtu mmoja anyakuwe yote.Com. Ibrahim Lethome: Basi kuwe na balancing.Wilson Kimei: Yaani balancing<br />
nikiona kama kamati ya Council iwe akitazama, ni bora. Lakini si ati ukifika Council hata uulize unaambiwa toka hakuna nafasi.<br />
Ni kama wengine hatuna uhuru. Kwaherini.<br />
Com. Ibrahim Lethome Mugo Mwaura yuko Charles Matheri Jacob Gichini Maigua Karibu. Halafu afuatwe na<br />
Onesmus Karimu Njungwa kama yuko. Ni wewe Mzee Haya mtafauatana hivyo. Dakika mbili mbili. Jacob.Mary Wanja<br />
Kamau: Mimi naitwa Mary Wanja Kamau na ningetaka kuchangia sana habari ya uwezo wa President. President ana uwezo<br />
mkubwa sana ni ndio naona hata kwa hii nchi yetu mambo yanaharibika. Kwa mapendekezo yangu ningetaka President<br />
aondolewe mamlaka ya kumchagua Permanent Secretary. Na tena aondolewe mamlaka ya kuwachagua judges na hata