28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeelekeza nguo yako<br />

hata kama imechafuka huachi kuifua. Kwa hivyo,<br />

Marine Services wameelekezwa pia kwamba wafanye<br />

usafi kadri inavyowezekana ili msafiri hata kama<br />

anaingia kwenye ile meli anaona imechoka, lakini<br />

angalau ni safi na haikatishi tamaa kuitumia. Kule Ziwa<br />

Viktoria labda niseme kwanza naona mama Mkiwa<br />

aliuliza nitakwenda wapi, kwa nini hatutoi tena<br />

huduma ndani ya Ziwa.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari maelekezo<br />

yamepelekwa kwa Marine Services kwamba wafanye<br />

survey ya bandari zote walizokuwa wanafika. Huko<br />

Ziwa Victoria kulitokea upungufu mkubwa wa kina cha<br />

maji, kilishuka sana na kwa hivyo meli zetu nyingi<br />

zilishindwa kwenda kwenye hivi visiwa ambako zilikuwa<br />

zinakwenda zamani. Kwa hiyo, tumewaelekeza<br />

wakafanye survey waone bandari zote zile ambazo<br />

kina kinaruhusu meli za Serengeti, Clarious, Butiama<br />

ambayo inafanyiwa matengenezo itakapopona<br />

zitakapoweza kwenda ili waweze kuanza kwenda<br />

kutoa huduma sehemu hizo. Wananchi wa maeneo<br />

hayo wasidhani kwamba Serikali imewatelekeza<br />

kulikuwa na tatizo kwanza la uharibifu wa meli<br />

zenyewe, lakini na kina cha maji kilipungua sana<br />

kuwawezesha kwenda kwenye vituo hivyo.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Tanganyika M.V.<br />

Liemba itafanyiwa matengenezo na Serikali ya<br />

Ujerumani. Serikali ya Ujerumani imekwishaagiza<br />

Kiwanda cha Twiga Cement kutoa euro milioni 2.5 kwa<br />

ajili ya matengenezo ya M.V. Liemba. M.V. Liemba<br />

ikitengenezwa itaendelea kutoa huduma kwa sasa<br />

mpaka pale DANIDA watakapojenga meli nyingine

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!