28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

zote mbili za Muungano. Isiwe watu wanakwenda huko<br />

madubwana yaliyochakaa wakatuletea hapa halafu<br />

yakaaza kuua watu na tukaambiwa eti kuna mamlaka<br />

inayodhibiti na kusimamia. Mamlaka gani hii, mbona<br />

inatumaliza<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo hivi vya baharini<br />

vyote ni vibovu. Hata hivi vya Azam Marine<br />

tunavyovitegemea, kuna vingine ni vibovu. Kwa<br />

ushahidi mimi nimeshaingia Sea Bus III, mara tatu ilizima<br />

ikiwa baharini. Meli ilipofika Dar es Salaam<br />

hawakusema wafanyakazi kama chombo kina<br />

matatizo na wakapakia abiria wengine wakawapeleka<br />

Unguja na kikaenda kikazima muda wa masaa mawili.<br />

Tunaiomba Mamlaka hii ifanye kazi yake iliyokusudiwa<br />

sio wakae tu huko ofisini wakituambia vyombo<br />

wanavikagua si kweli, haiwezekani hata siku moja.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hata vyombo vya<br />

nchi kavu vinasababisha ajali kwa wingi. Tuangalie jinsi<br />

mabasi yanavyoanguka na kuua abiria kila siku. Mamia<br />

ya Watanzania wanateketea. Barabara ziongezwe<br />

upana wake. Barabara ni nyembamba wakati wa<br />

kupishana na maroli gari nyingine zinaanguka. Hebu<br />

jamani tuangalie ni kitu gani hasa sisi kilichotupata<br />

hata ikawa usafiri wote una matatizo<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hizi ndege<br />

tulizonazo pia zina matatizo. Baadhi ya ndege hizi za<br />

abiria ni mbovu. Mimi nimeshawahi kupanda ndege<br />

moja sitaki niitaje inavuja ikinyeshewa na mvua. Jamani<br />

hii ni aibu kwa taifa hili. Hizi ndege zimechakaa, hata<br />

huko zilikotengenezwa inaonekana hazitumiki tena, sisi

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!