Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
zote mbili za Muungano. Isiwe watu wanakwenda huko<br />
madubwana yaliyochakaa wakatuletea hapa halafu<br />
yakaaza kuua watu na tukaambiwa eti kuna mamlaka<br />
inayodhibiti na kusimamia. Mamlaka gani hii, mbona<br />
inatumaliza<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo hivi vya baharini<br />
vyote ni vibovu. Hata hivi vya Azam Marine<br />
tunavyovitegemea, kuna vingine ni vibovu. Kwa<br />
ushahidi mimi nimeshaingia Sea Bus III, mara tatu ilizima<br />
ikiwa baharini. Meli ilipofika Dar es Salaam<br />
hawakusema wafanyakazi kama chombo kina<br />
matatizo na wakapakia abiria wengine wakawapeleka<br />
Unguja na kikaenda kikazima muda wa masaa mawili.<br />
Tunaiomba Mamlaka hii ifanye kazi yake iliyokusudiwa<br />
sio wakae tu huko ofisini wakituambia vyombo<br />
wanavikagua si kweli, haiwezekani hata siku moja.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hata vyombo vya<br />
nchi kavu vinasababisha ajali kwa wingi. Tuangalie jinsi<br />
mabasi yanavyoanguka na kuua abiria kila siku. Mamia<br />
ya Watanzania wanateketea. Barabara ziongezwe<br />
upana wake. Barabara ni nyembamba wakati wa<br />
kupishana na maroli gari nyingine zinaanguka. Hebu<br />
jamani tuangalie ni kitu gani hasa sisi kilichotupata<br />
hata ikawa usafiri wote una matatizo<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hizi ndege<br />
tulizonazo pia zina matatizo. Baadhi ya ndege hizi za<br />
abiria ni mbovu. Mimi nimeshawahi kupanda ndege<br />
moja sitaki niitaje inavuja ikinyeshewa na mvua. Jamani<br />
hii ni aibu kwa taifa hili. Hizi ndege zimechakaa, hata<br />
huko zilikotengenezwa inaonekana hazitumiki tena, sisi