Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
mpaka shilingi 35,000, hii siyo sawa! Ninaomba<br />
muangalie utaratibu mzuri wa wananchi kukata tiketi.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa pia ninaulizia<br />
usafiri wa Tabora - Kaliua mpaka Mpanda, usafiri huu<br />
unaanza lini kwa kuwa usafiri ni mgumu sana kwa watu<br />
wanaotokea maeneo ya Mpanda.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ya Ardhi<br />
na Wizara ya Uchukuzi washirikiane kutatua matatizo<br />
ambayo yanasababishwa na TPA ambao wamekuwa<br />
na maeneo yao yaani kama wana bandari kavu lakini<br />
wamekuwa wakitaka kuingilia maeneo ya wananchi<br />
wanapokaa kwa mfano Gungu kuna eneo la Katosho,<br />
TPA wana eneo lao toka mwaka 1964 lakini sasa<br />
wametaka ku-expand kwa nini wanataka kuingia<br />
maeneo ya watu na wasiende kwenye maeneo<br />
ambayo hayana watu Kuna eneo moja karibu na<br />
Bwawa la Katosho, kuna nafasi ya kutosha, mshirikiane<br />
na wananchi ili muweze kujua mipaka yenu inaishia<br />
wapi na wao wanaishia wapi ili kuondoa matatizo<br />
ambayo yanaendelea. Ninawashukuru sana<br />
Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi na Mheshimiwa Waziri<br />
wa Ardhi wamelisimamia jambo hili na Mkuu wa Mkoa<br />
na ameweza kusimamisha, hakuna kinachoendelea<br />
sasa hivi lakini wananchi wamekaa hawaelewi ni nini<br />
kinachoendelea, mlimalize hili ili watu waendelee na<br />
shughuli zao.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, RAHCO ni kampuni<br />
ambayo ilianzishwa chini ya Sheria Namba 4 ya 2002<br />
katika kuhakikisha kuwa inakuwa msimamizi wa mali za<br />
shirika wakati reli inapokuwa imebinafsishwa lakini mimi