Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
hapa kuna rushwa ya ufisadi na ningeomba tu Wizara<br />
iweze kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha<br />
kwamba kwa nini hawa watu wanaiibia Serikali mpaka<br />
dakika hii. Kwa nini hawalipi madeni yao na wakati<br />
sekta hii ni sekta muhimu ambayo inachangia kwenye<br />
pato la Taifa Wao ni akina nani mpaka wasilipe<br />
madeni haya kwa muda wote huu<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa kuna tatizo<br />
bandarini, tatizo la wizi, tukiangalia mwaka jana pekee<br />
zimeibiwa takriban container nne za shaba, hii nchi<br />
mnatupeleka wapi Hivi container ya shaba bandarini<br />
inaibiwaje Tukiangalia wenzetu wa Hongkong ndani<br />
ya miaka 20 wamewahi kuibiwa Mercedes Benz na<br />
ndani ya masaa machache ikapatikana, lakini bandari<br />
yetu ya Dar es Salaam zinaibiwa container nne ndani<br />
ya mwaka mmoja, hapa kuna poor security system.<br />
Kwa hiyo, napenda kumwomba Waziri afanye<br />
afanyalo ahakikishe kwamba anadhibiti wizi wa<br />
bandarini. Wizi wa bandarini imekuwa ni kero na<br />
wanaoiba sio kwamba ni vibaka kutoka mtaani ni<br />
wataalamu, wafanyakazi wa bandari, kwa hiyo,<br />
Mheshimiwa Waziri hakikisha kwamba masuala haya<br />
unayashughulikia.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kugusia<br />
suala zima la ajali. Wenzetu wa SUMATRA walikuwa<br />
wakishirikiana na wenzetu wa Zanzibar Maritime<br />
Authority, lakini baadaye inasemekana wenzetu wa<br />
Zanzibar wakajitenga lakini ajali hizi zinapotokea jamani<br />
watu wanaokufa ni wote, Watanzania Bara na wa<br />
Tanzania Zanzibar. Mimi nimefika eneo la tukio,<br />
nimewakuta wapiga kura Mheshimiwa Chenge kule