Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
inatendeka kwa sababu CV ni nzuri. Naomba mzifanyie<br />
kazi.<br />
Baada ya kusema hayo, naomba nichangie<br />
mambo kama mawili au matatu. Jambo la kwanza<br />
kabisa ni kwamba, nakubaliana kabisa na msemaji<br />
aliyepita. Mambo mengi ni ya ajabu kabisa kwamba<br />
yapo lakini hayatekelezwi. Sisi Wa<strong>bunge</strong> humu ndani<br />
kama tunavyosema, kila mara tunakaa tunalalamika,<br />
lakini kwa nini tunaendelea kulalamika wakati ni sisi<br />
wenyewe ambao hayo mambo tunayajua, tunayo,<br />
lakini hatuyafikishi mwisho<br />
Kwa mfano, kama suala alilosema; mimi nilikuwa<br />
najiuliza, na nikawa nafikiri nikipata nafasi nitauliza swali<br />
kama hili, kwamba reli zetu tunajua bila kuelezwa, toka<br />
tumeanza kujifunza katika Shule za Msingi kwamba reli<br />
ndiyo chombo muhimu sana kwa ajili ya kubeba mizi<strong>go</strong><br />
na kwamba hata Wakoloni hawakuwa wajinga<br />
wakatengeneza reli kutoka kwenye vitu<br />
vinakopatikana, mfano, mazao na kadhalika, zikaenda<br />
bandarini kusudi zipeleke mizi<strong>go</strong>. Lakini sisi tulipochukua<br />
tukaanza kufanya kinyume chake. Matokeo yake tuko<br />
hapa tunalalamika. Hiyo Reli ya Kati iliyojengwa na<br />
Mjerumani ikamaliziwa na Mwingereza.<br />
Mimi nilikuwa najiuliza, baada ya Watanzania<br />
wenye nia njema na nchi hii kulalamika na kuona<br />
mambo yaliyotokea na wafanyakazi wenye uzalendo<br />
wakajitolea kwamba wangeweza kufufua vitu vingine<br />
mpaka hadi sasa hiyo reli ikarudi mikononi mwetu, lakini<br />
jamani hatujiulizi kwamba huu si ndiyo utakuwa<br />
mtindo