constitution of kenya review commission ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hata nyinyi watu wa Wangige nyote si munajua hivyo? Simunajua River side? Hata tukichukua hawa, si tunaweza kuwapeleka<br />
River side, hakuna mtu hajui hiyo, kwa hivyo chief aondolewe kabisa asante.(clapping)<br />
Com. Wambua: Asante sana, tutamuita Robert Chege.<br />
Robert Chege: Habari zenu, kwa majina ni kama hayo mumesikia. Nimetoka kijiji cha Gathiga. Mimi nashukuru kwa vile<br />
mengi yametajwa hapa, ijapokuwa nataka kugusa tu mambo ya Commissioners. Hilo ni jambo langu la kwanza, kwa sababu<br />
tunaongea mambo ya kutengeneza Katiba yetu sisi wa Kenya. Kuna maswali ingine huwa sisi wa Kenya tunajiuliza, kulingana<br />
na vile sisi huwa tunaona.<br />
Ya kwanza, ni kwa nini wakati sisi tumeitisha Katiba, ndio tunaletwa Commissioners, wale watakuja kutengeneza Katiba. Na<br />
kulinga na maoni yangu, mimi naonelea katika Kanu, ndio tulipata Commissioners wengi. Ilehali katika total votes, zile tuko<br />
nazo katika Kenya. Wako na less votes kuliko party zile zingine katika hii Kenya. Tena kuna wrangles, katika commision yao.<br />
Unasikia kuna political interference, na mambo mengine mbaya, ambayo huwa inaendele tunasikia katika media. Tena hawa<br />
makamishna huenda <strong>of</strong>fisi kwa <strong>of</strong>fisi, na hali hawaendi nyumba kwa nyumba. Kwa hivyo inaonekana, kuna kitu kile wana<br />
serve, katika hii mambo ya kumaliza hii Katiba yetu. Tena tunambiwa Katiba itamalizika by December. By whose mandate, na<br />
Katiba hii ni yetu? Hii Katiba ni sisi tulipatiwa conference, tuende tulizwe ile siku, Katiba hii tumetaja tunataka imalizike. Kwa<br />
hivyo hapo tunaona tena kuna kitu ndani yake imefichwa. Tumeona kama hii Katiba haitafanyika kulingana na vile raiya<br />
wanatoa maoni yao, tutaitisha further reforms kwa miaka ingine kama kumi na tano.<br />
Nikiguza kitu kidogo mambo ya Presidency. President anafaa kuwa na powers, kuwa anapata ile mambo yote inatendeka<br />
katika bunge anapitisha. Hafai kuwa juu ya sheria. Na hiyo basi anafaa kufutiliwa mbali katika bunge. Thus, we can have a<br />
vote <strong>of</strong> no confidence from the Parliament, kama akipatikana na makosa yeyote. He should be <strong>of</strong> Kenyan origin. Awe na<br />
miaka 35 mpaka 70. Awe mtu amefikisha form four and above, na awe na sound mind. Awe ameoa, na awe akitumia bidii<br />
yake pahali inafaa. Awe mtu anajua mambo ya Mungu, na awe sio mtu ambae amehusika na mambo ya corruption, na awe<br />
anadeclare wealth yake, wakati anasimama kwa Presidency. Tuwe na President and Vice President wawili.<br />
Parties: Vyama nazo katika Kenya, ndio tusiwe na mambo ya ukabila, tuwe na vyama vitatu peke yake, katika Kenya yetu.<br />
Na kuwe na serikali ya muungano, ambayo the winning party, huyo President, awe na over 50% total votes, na wa pili awe ni<br />
wa chama hiyo ingine, awe ni first Vice chairman. Wa tatu ni wa chama hiyo ingine, awe second vice chairman.<br />
Kusiwe na mambo ya merger anymore katika Kenya. Kwa sababu mambo ya merger inaleta dictatorship, ina kuja<br />
ku-neutralize wale ma MP wengine wamekuwa swallowed. Hivyo basi, hawana nguvu ya kuongea kwa vile tayari wako chini<br />
ya mtu mwingine.<br />
51