28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kwa kuwa sasa kiwanda hiki kilishapata mwekezaji; na kwa kuwa wafanyakazi wao<br />

wapatao 567 waliahidiwa kwamba punde kiwanda kitakapopata wawekezaji, watapata<br />

kipaumbele cha kuendelea na ajira. Je, Serikali ina mpan<strong>go</strong> gani kuhakikisha kwamba mwekezaji<br />

huyu anaendelea kuwarudisha wafanyakazi hawa katika ajira yao<br />

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa wafanyakazi hao 567 bado wana madai yao<br />

mbalimbali toka mwaka 1997 na hadi leo hii hawajakamilishiwa madai yao. Serikali ina mpan<strong>go</strong><br />

gani wa kuhakikisha kwamba wafanyakazi hawa wanalipwa mafao yao sawasawa kabla<br />

mwekezaji hajaanza kazi yake ipasavyo katika kiwanda hiki<br />

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa<br />

tumemaliza m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ule na kiwanda kinatakiwa kifanye kazi, habari ya wafanyakazi, matatizo<br />

waliyokuwa nayo yatashughulikiwa kwa mujibu wa sheria za ajira. Tutashirikiana na kampuni ile,<br />

tutashirikiana na Wizara ya Kazi inayohusika kuangalia haki za wafanyakazi hao ambazo<br />

zimelindwa au zilivyo na kwa hakika kwa vyovyote vile hatutawadhulumu.<br />

Mheshimiwa Spika, tutakachokifanya ni kufuata tu sheria za ajira na haki za wafanyakazi<br />

zinalindwa namna gani. Naomba awe na subira, Serikali itazishughulikia.<br />

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kumuuliza<br />

Mheshimiwa Waziri kwamba wafanyakazi wa Mbarali NAFCO na Kampunga NAFCO, wanadai<br />

madai yao ya kulipwa fidia baada ya mashamba hayo kubinafsishwa bila mafanikio. Wamefika<br />

mpaka Mahakamani, Mahakama imeamuru walipwe, lakini mpaka sasa bado hawajalipwa. Je,<br />

Mheshimiwa Waziri atanihakikishia kwamba atasaidia kuhakikisha wananchi hawa wanapata haki<br />

zao<br />

SPIKA: Haya, swali lingine kabisa! Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu!<br />

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa Mbarali<br />

takriban wiki tatu zilizopita, sikuongea na wafanyakazi, lakini niliweza kupata malalamiko ya<br />

wafanyakazi walioko pale. Ninachoweza kusema tu ni kwamba, suala la wafanyakazi pale, kama<br />

bado wana matatizo ambayo hayajakamilika, nalo tutalishughulikia. Najua wana matatizo mengi<br />

zaidi ya hilo, ikiwa ni pamoja na mashamba ambayo walitaka yashughulikiwe. Kwa bahati<br />

nilimwambia hata Mheshimiwa Kilufi kwamba nilipokuwa kule nimetoa ahadi ya Serikali kwamba<br />

wananchi wote waliokuwa katika shamba lile, tumetoa ahadi, Serikali imetoa shilingi milioni 500,<br />

tuwatengenezee mashamba ya umwagiliaji pembeni, wakati matatizo mengine yanashughulikiwa<br />

na Serikali. Kwa hiyo, naomba pia Mheshimiwa Kilufi naye awe na subira. Lakini wakati wanasubiri<br />

hili tatizo lao la wafanyakazi, wafanyakazi wale followback position, kupata maeneo mengine<br />

tumelishughulikia tayari.<br />

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-<br />

Na. 496<br />

Mfumo wa Stakabadhi kwa Zao la Pamba<br />

Bei ya zao la pamba nchini imekuwa haitabiriki ambapo Serikali ikitoa bei elekezi ambayo<br />

ni ya chini sana na kutoa mwanya kwa wafanyabiashara wa zao hilo kununua kwa bei ndo<strong>go</strong><br />

kisha wao kuuza kwa bei kubwa na kupata faida zaidi ya wakulima ambao hubaki maskini na<br />

hivyo kutishia uzalishaji wa zao hilo:-<br />

(a) Je, Serikali ina mpan<strong>go</strong> gani wa kuboresha mfumo wa stakabadhi ghalani ambao<br />

utawalinda wakulima wa zao la pamba wasiendelee kupunjwa na wachuuzi wanaolangua<br />

pamba<br />

(b) Je, kuna ukweli wowote kuwa Benki ya NMB ina mpan<strong>go</strong> wa kudhamini mfumo wa<br />

stakabadhi ghalani<br />

10

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!