28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la<br />

Mheshimiwa Zarina Shamte Madabida, M<strong>bunge</strong> wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama<br />

ifuatavyo:-<br />

(a) Mheshimiwa Spika, ni kweli vijana wengi wanaomaliza vyuo na kuwa na ujuzi<br />

mbalimbali wanakabiliwa na tatizo la mitaji. Kwa kutambua tatizo hili, mwaka 1996 Serikali ilitunga<br />

Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana. Pamoja na mambo mengine, Sera hii imetoa mwon<strong>go</strong>zo<br />

kwa vijana, wazazi, wadau wa elimu na hasa waelimishaji wanaotayarisha Mipan<strong>go</strong> ya<br />

Maendeleo katika sekta mbalimbali za maendeleo ya namna ya kuwawezesha vijana kushiriki<br />

kikamilifu katika shughuli za kujipatia ajira na mapato. Kwa mfano, aya ya 5.7, aya ndo<strong>go</strong> ya 5.7.1<br />

na 5.7.2 zinatoa maelekezo kwa Wizara ya Fedha ya namna ya kuwasaidia vijana kupata mitaji.<br />

(b) Mheshimiwa Spika, ili kuwasaidia wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji Serikali<br />

iliandaa Sera ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi mwaka 2004 na baadaye Sheria ya Uwezeshaji<br />

wa wananchi kiuchumi namba 16 ya mwaka 2004. Baraza la Uwezeshaji limeelekezwa kuweka<br />

mikakati mahsusi ikishirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo<br />

kutambua mahitaji ya mitaji kwa vijana kwa nia ya kuwawezesha kupitia vikundi vyao rasmi.<br />

Mheshimiwa Spika, kuna nguzo tisa za uwezeshaji na kati ya nguzo hizo zilizoainishwa<br />

kwenye sera, nguzo nne zinaweka mkakati wa namna ya kuwawezesha wajasiriamali wakiwemo<br />

vijana wa rika mbalimbali kupata mitaji kwa ajili ya kuendeshea shughuli za kiuchumi na hizo nguzo<br />

zimeorodheshwa.<br />

Mheshimiwa Spika, kutokana na sera na sheria ya kuwawezesha wananchi kiuchumi<br />

tumepata mafanikio mengi, ikiwemo kuongeza idadi ya wanaokopeshwa, kuongeza ajira, kutoa<br />

huduma za ushauri wa ugani kwa wajasiriamali kupitia SIDO na kuimarisha SACCOS mbalimbali na<br />

kwa kushirikiana na sekta binafsi kubuni mradi wa kukuza ushindani wa biashara na kadhalika.<br />

Napenda kuwashauri vijana kujiunga katika vikundi au ushirika kwa wale walio kazini na<br />

kuhakikisha wamesajiliwa.<br />

MHE. ZARINA S. MADABIDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali<br />

la nyongeza. Nashukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yako. Lakini vijana ninaowaongelea ni<br />

wale ambao wanamaliza vyuo ambao hawana kazi, hawawezi kujiunga na SACCOS kwa sababu<br />

hawana fedha. Je, Wizara yako inasemaje kuhusu vijana hao kwa sababu mpaka sasa hivi hali<br />

ilivyo hawana jinsi yoyote ya kuweza kujikwamua kimaisha. Naomba jibu.<br />

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI: Mheshimiwa Spika,<br />

napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Madabida kwa kujielekeza kwenye matatizo na mahitaji<br />

ya mitaji ya vijana.<br />

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba, vijana wanaomaliza vyuo huwa hawana kazi<br />

hawajaajiriwa na kwa hivyo pengine ni vigumu sana kujiunga na SACCOS. Lakini inawezekana<br />

vile vile wakiwa vyuoni kwa mfano, Madaktari, Wahandisi, Wahasibu wanaweza wakaunda<br />

vikundi vyao ambavyo si vya SACCOS, lakini kupitia vikundi hivyo wakaweza kuliona Baraza la<br />

Uwezeshaji ili liweze kuwapa namna ya kupata mitaji na mimi binafsi kwa sababu Baraza liko chini<br />

ya Mheshimiwa Waziri Mkuu tutawaelekeza kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi<br />

kwamba wajielekeze kwa vijana hao kwa sababu ndio nguvu kazi au rasilimali muhimu ya Taifa<br />

letu na ndio tunaowategemea kujenga uchumi wetu hasa katika soko hili huria.<br />

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Ningependa<br />

kuuliza kwamba kwa kuwa mtaji pekee wa vijana hawa ni elimu yao. Je, kwa nini Serikali<br />

isivihamasishe vyombo vya fedha vikatumia vyeti vyao halisi kama dhamana kwa ajili ya kupewa<br />

mikopo<br />

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI: Mheshimiwa Spika,<br />

napenda vile vile kumshukuru sana Mheshimiwa Selasini, M<strong>bunge</strong> wa Rombo kwa kuibua jambo<br />

2

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!