28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Uzamili. Kutokana na jitihada hizi, kumekuwa na ongezeko la wadahiliwa kutoka 1,013 mwaka<br />

2005/2006 hadi 6,713 mwaka 2010/2011.<br />

Mheshimiwa Spika, napenda pia ieleweke kuwa Vijiji ambavyo vina Zahanati za Mashirika<br />

ya Dini, binafsi, Serikali haitajenga Zahanati nyingine bali itahakikisha Zahanati hizo zinatoa<br />

huduma kwa wananchi kwa kuzingatia viwan<strong>go</strong> vilivyowekwa na Serikali.<br />

MHE. MHONGA S. RUHWANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali<br />

moja la nyongeza. Pamoja na mpan<strong>go</strong> huo wa ujenzi wa zahanati na kuboresha zile ambazo<br />

zipo, lakini pia Hospitali za Mikoa na zile za Rufaa zinakabiliwa na matatizo kama hayo ikiwemo<br />

Hospitali ya Mkoa wa Ki<strong>go</strong>ma haina Madaktari Bingwa na vifaa vya kupimia hakuna. Je, Serikali<br />

haioni kwamba kuna umuhimu wa kuweka mkakati maalum wa kuboresha hospitali hizo za Rufaa<br />

na za Mikoa<br />

WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, ni kweli hospitali zetu za mikoa<br />

zinakabiliwa na matatizo na changamoto mbalimbali ikiwemo Madaktari Bingwa pamoja na<br />

vifaa. Hili tumeliona na katika bajeti yetu iliyopitishwa na Bunge hili, tumeonesha ni namna gani<br />

tunaweza tukakabiliana na tatizo hili, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mhonga na wakazi wa<br />

Mkoa wa Ki<strong>go</strong>ma hasa Hospitali ya Ki<strong>go</strong>ma tumeliona tatizo hilo, ni moja ya hospitali ambayo<br />

nimeelekeza kupeleka Madaktari Bingwa kwa sababu kuna uhaba mkubwa sana wa Madaktari<br />

hao katika hospitali hiyo.<br />

Na. 499<br />

Serikali Kupunguza Bei ya Uzalishaji wa Gesi<br />

MHE. JOHN J. MNYIKA (K.n.y MHE. MUSTAPHA B. AKUNAAY) aliuliza:-<br />

Umeme wa gesi asilia kuwa nishati mbadala ya umeme unaofuliwa kwa mitambo<br />

inayotumia mafuta ya diseli na ule unaotokana na nguvu ya maji (Hydroelectric power) ili<br />

kupunguza matumizi ya mkaa unaotengenezwa kwa kukata miti mingi:-<br />

Je, kwa nini Serikali isitoe ruzuku kwa wazalishaji wa gesi ili bidhaa hiyo ipatikane kwa bei<br />

nafuu ili kushawishi watu kutumia umeme wa gesi asilia zaidi majumbani badala ya mkaa na<br />

kunusuru misitu yetu<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la<br />

Mheshimiwa Mustapha Boay Akunaay, lakini kabla ya hapo kwa ridhaa yako naomba nitoe<br />

maelezo kido<strong>go</strong> kwa swali lililoulizwa jana la Mheshimiwa Lekule Laizer.<br />

Mheshimiwa Spika, jana wakati najibu swali kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini<br />

Mheshimiwa Lekule aliulizia upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Longido, katika majibu<br />

yangu nilielekeza majibu yangu ambayo yalikuwa yanaelekea kujibu matatizo au hoja zilizopo za<br />

kupeleka umeme Loliondo kwa Mheshimiwa Ole Telele, naomba nimwombe msamaha<br />

Mheshimiwa Lekule kwa mchanganyiko ule.<br />

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, Longido hakuna umeme wa jenereta, umeme ule<br />

unatoka Kenya, lakini mkakati bado upo wa kusambaza umeme pale na kazi zinaendelea<br />

pamoja na maeneo yale mengine ya Longido, Oldonyo Sambo na kwingineko. Kwa hiyo,<br />

naomba nimhakikishie Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> Lekule kwamba kazi inaendelea lakini siyo umeme<br />

wa jenereta, ni umeme wa gridi ule ambao tuna inter conector kutoka Kenya.<br />

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini<br />

napenda, kujibu swali la Mheshimiwa Mustapha Boay Akunaay M<strong>bunge</strong> wa Mbulu kama<br />

ifuatavyo:-<br />

14

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!