Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
linakisiwa litakuwa na watu laki tatu, je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutuahidi wananchi wa<br />
Rungwe Magharibi kwamba wakati huo basi vigezo hivi kwa kuwa bado vitaendelea kuwa ni<br />
vigezo muhimu, Jimbo hili linaweza likapata sifa ya kuweza kugawanywa<br />
Swali la pili, kuna vijiji ambavyo viko mbali sana na Makao Makuu ya Wilaya ya Rungwe<br />
yaani Tukuyu, Vijiji vya Mkumburu, Isabula, Kipande katika Tarafa ya Ukukwe viko mbali sana na<br />
hali ya miundombinu ya barabara katika maeneo hayo ni ngumu sana hivyo hawawezi kufikia<br />
kumwona Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> huko Tukuyu. Je, Serikali inaweza kuwafikiria watu hao basi<br />
angalau kuwatengenezea barabara ambazo ni za kudumu ili waweze kusafiri kwa urahisi kufika<br />
katika Makao Makuu ya Jimbo<br />
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.<br />
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI: Mheshimiwa Spika,<br />
swali lake la kwanza linasema kwamba ifikapo mwaka 2015 idadi ya watu Jimbo la Rungwe<br />
Magharibi litafikia laki tatu na anapenda kujua kwamba kama naweza kuahidi.<br />
Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi kwamba kuna vigezo 13<br />
ikiwemo kigezo cha idadi ya watu na nikaahidi kama vigezo vitakuwa vimetimia na kwamba<br />
vinatosheleza, Serikali haitasita kuligawa Jimbo la Rungwe, lakini ni hapo ambapo vigezo<br />
vinavyotakiwa viwe vimefikiwa ikiwa ni pamoja na idadi ya watu.<br />
Pili, kwamba kuna vijiji ambapo viko mbali sana na ambapo yupo Mheshimiwa M<strong>bunge</strong><br />
na kwamba barabara ni mbovu. Kwa kweli nawapa pole wananchi hawa ambao wako mbali<br />
ambao wanapata adha ya kufika kwa M<strong>bunge</strong> wao. Ninachoweza kusema hapa ni kuishauri na<br />
kuielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe na kwa kushirikiana na wananchi wa vijiji hivyo,<br />
waone umuhimu wa kutengeneza barabara ambazo zinaweza kuwafikisha Makao Makuu ya<br />
Jimbo na vile vile kufikia huduma mbalimbali ambazo ni muhimu sana kwa wananchi.<br />
SPIKA: Mheshimiwa Kirigini swali la nyongeza.<br />
MHE. ROSEMARY K. KIRIGINI: Mheshimiwa Spika,<br />
SPIKA: Aha! Samahani Mheshimiwa Kirigini, Waziri wa Nchi TAMISEMI.<br />
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA<br />
(TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi,<br />
napenda kuwapa taarifa watu wa Rungwe kwamba kwa kutambua ukubwa wa Wilaya ya<br />
Rungwe, kwa kutambua wingi wa watu katika Wilaya ya Rungwe Waziri mwenye dhamana ya<br />
Serikali za Mitaa yaani Waziri Mkuu ameridhia kuanzishwa kwa Halmashauri ya Wilaya Busekelo<br />
katika Wilaya ya Rungwe. Kwa hiyo, tutaanza na Halmashauri hizo mbili huko mbele ya safari<br />
kama kila Halmashauri zitafuzu kuwa Jimbo basi itatazamwa kulingana na itakavyokuwa. Lakini<br />
taarifa njema kwa Rungwe ni hiyo kwamba, tunaanza na Halmashauri mpya ya Wilaya ya<br />
Busekelo.<br />
SPIKA: Lakini na ukumbi wetu tumeshapanua hatuwezi kupanua zaidi ya hapo. Hilo nalo<br />
mlifahamu. Mheshimiwa Kirigini nilikwita.<br />
MHE. ROSEMARY K. KIRIGINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii<br />
muhimu. Kwa kuwa kilio cha wananchi wa Musoma Vijijini kwa takriban miaka 10 sasa ni kuhusu<br />
kukata Jimbo hilo ambalo lina watu zaidi ya laki tano na Kata 34. Je, Serikali haioni sasa ni wakati<br />
muafaka kulikata Jimbo hili ili yaweze kuwa Majimbo mawili au hata matatu ili kuharakisha shughuli<br />
za maendeleo<br />
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA<br />
(TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, kwa kutambua kwamba Wilaya ya Musoma Vijijini ni kubwa ndio<br />
maana Mheshimiwa Rais ameamua kuanzisha Wilaya mpya ya Butiama inayozaliwa kutokana na<br />
Musoma Vijijini.<br />
4