28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, naiomba Wizara iwashauri PPF waendelee na ujenzi wa nyumba hizi za<br />

bei nafuu katika maeneo mbalimbali hapa nchini hususan kwenye Wilaya ya Kinondoni ili<br />

wananchi wetu waweze kupata nyumba hizo ambazo ni nzuri sana. Pia niwapongeze PPF kwa<br />

ujenzi wa Chuo Kikuu, Dodoma hasa ujenzi wa kisasa wa kituo cha Computer hapo UDOM.<br />

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo naomba PPF waangalie uwezekano wa<br />

kuwasomesha watoto wa wanachama wao waliofariki hadi Chuo Kikuu badala ya sasa<br />

kuwasomesha hadi Sekondari. Mpan<strong>go</strong> huu ni mzuri na ni faraja sana kwa wanachama wa Mfuko<br />

huu pia elimu izidi kutolewa kuhusu mpan<strong>go</strong> huu mzuri wa PPF ili wananchi wengi zaidi wajiunge<br />

na Mfuko huu ili wafaidike na mpan<strong>go</strong> huu.<br />

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, nampongeza kwa hotuba nzuri, pia<br />

nawapongeza Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara.<br />

Mheshimiwa Spika, zipo changamoto kubwa sana katika huduma kwa wastaafu na<br />

warithi. Nikichukulia tu Jimboni kwangu Busanda Wilayani Geita wastaafu wengi hawajapata<br />

mafao yao na wanahangaika sana. Wengine wamefuatilia sasa kwa zaidi ya miaka kumi na<br />

hawajafanikiwa kupata mafao yao. Wastaafu wengi hawana nauli maana wengi wanatakiwa<br />

kufuatilia Dar es Salaam. Pamoja na juhudi zilizopo za kuboresha utoaji wa huduma hii lakini<br />

huduma hii bado ni kero kubwa sana kwa wastaafu na warithi. Hivyo, naomba Wizara iangalie<br />

namna ya kuwasaidia hasa wastaafu wa vijijini wasiokuwa na uwezo hata wa nauli ili wapate<br />

mafao yao.<br />

Mheshimiwa Spika, kero ya pili ni madai ya malimbikizo ya bima kwa wanachama wake.<br />

Wanachama wengi wanalalamika sana kwa sababu wamechangia michan<strong>go</strong> yao vizuri lakini<br />

malipo kwa bima zilizoiva inakuwa ni usumbufu mkubwa sana. Kwa kuwa mapato ya bima<br />

yameongezeka kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha bajeti, ukurasa 57, basi naomba<br />

wanachama wote wenye madai yao walipwe. Kama ulivyoahidi ndani ya hotuba kwamba NIC<br />

itaendelea na kuhakiki malimbikizo na madai yote kulipa ili kurejesha imani kwa wateja, naomba<br />

hoja hii itekelezwe kwa haraka ili wanachama wawe na imani tena kwa NIC.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, naunga mkono hoja.<br />

MHE. DAVID KAFULILA:<br />

yafuatayo:-<br />

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia katika maeneo<br />

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu ubinafsishaji. Naomba Wizara ya Fedha itoe kauli<br />

mahsusi kuhusu Mwekezaji kwenye M<strong>go</strong>di wa Chumvi, Uvinza. Mwekezaji huyu ni Kampuni ya<br />

Great Lakes Mining ambaye kwa mujibu wa mkataba aliahidi kuendeleza m<strong>go</strong>di huu unaozalisha<br />

chumvi katika Plants tatu; Solar plant, Thermal plant na PVD plant. Badala ya kuendeleza<br />

Mwekezaji huyu ameamua kuuza mali za m<strong>go</strong>di huu kama mitambo na nyumba tofauti na sera ya<br />

ubinafsishaji. Tulibinafsisha m<strong>go</strong>di kwa bei ndo<strong>go</strong> ili uendelezwe sio uporwe, huu ni wizi. Naomba<br />

Wizara itoe tamko kuhusu wizi huu.<br />

Mheshimiwa Spika, pili, ni kuhusu mafao ya waliokuwa wafanyakazi kabla ya ubinafsishaji.<br />

Hapa naomba Serikali au Wizara ikutane na wafanyakazi takriban 300 walioachishwa kazi tangu<br />

mwaka 1999, lakini wamepunjwa mafao yao. Nimepitia barua za kuachishwa kazi wafanyakazi<br />

hawa, ukweli walipunjwa. Kuna wafanyakazi wamefanya kazi miaka 20 mpaka 40 lakini<br />

wameambulia mafao ya laki tisa mpaka milioni mbili tu. Naomba Wizara kupitia CHC au kadri<br />

Waziri anavyodhani inafaa watu hawa wapate kusikilizwa ili tupate ufumbuzi wa kudumu wa tatizo<br />

hili. Naomba sana.<br />

Mheshimiwa Spika, mwisho, nashauri Serikali kupitia Wizara itafute majibu ya haraka ya<br />

kukabiliana na tatizo la thamani ya shilingi (Currency devaluation). Napenda kushauri Serikali itoe<br />

46

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!