Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kuweza kuhimili hali halisi na kuweza kumudu kulipia nyumba hizi. Mheshimiwa Waziri chini ya<br />
taasisi yako ya PPF tunawaomba sana mje Mafia na ardhi tutawapa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba tena nipongeze mifuko mingine ya<br />
pensheni. Serikali yetu tumeona katika mjadala mzima wa miezi miwili na zaidi, kila siku<br />
Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, walikuwa wakisema kuhusu mapungufu ya miradi mbalimbali. Lakini<br />
tunashukuru kwa Serikali kuona kwamba kupitia mifuko hii yetu ya jamii naamini mambo<br />
yaliyoelezwa na hasa hili la mwisho la umeme tukiweza kuitumia NSSF mimi naamini mambo yetu<br />
yatakuwa mazuri.<br />
NSSF wana uwezo, PPF wana uwezo pamoja na mifuko mingine ya jamii. Hakika, hawa<br />
watu laiti kama na haya Mashirika mengine yangekuwa wanafanyakazi kama walivyokuwa<br />
wanafanya vion<strong>go</strong>zi hawa wa taasisi hizi NSSF, PPF na wengine nasema nchi hii tusingekuwa na<br />
shida. Wapeni kazi hii NSSF na PPF na mifuko mingine ya jamii na naamini ndio itakayoweza kulinda<br />
maslahi ya taifa hili kuliko kuangalia kuuza Mashirika yetu na kuacha miradi hii inakwenda holela<br />
na matokeo yake sasa tunakuja kusemeana mbovu hapa ndani na watu wanaanza kulaumiana.<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana kwa kuweza kufanya mipan<strong>go</strong> hii na wameweza<br />
kwa mfano michan<strong>go</strong> ya NSSF, PPF na Mashirika mengine wametujengea Chuo Kikuu cha<br />
Dodoma. Hakika nawapongeza sana. Viten<strong>go</strong> mbalimbali kama vya Computer PPF na wengine<br />
mabweni wameweza kuyajenga. Nasema tuitumie mifuko hii. Mimi kupitia Ramadhani hii<br />
nawaombea Dua wale Ma-DG na watendaji wao wote wa mifuko hii Mwenyezi Mungu<br />
awazidishie hekima, awape busara awazidishie uzalando awalinde na Mahasidi na Inshallah<br />
mambo yao yatakuwa mazuri kwa sababu wameweka nia ya kutusaidia nchi hii. Naamini<br />
kwamba Mwenyezi Mungu anaisikia Dua hii na Mungu atawalinda na atawaon<strong>go</strong>za wao na<br />
familia zao. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, tumelalamika kipindi kilichopita kwa mambo mengi sana hapa<br />
tumeongea na siyo kulalamika tunaongea. Lakini yako mambo wakati mwingine Serikali<br />
tukiwaambia labda wanakuwa ama wanafanya shughuli zao kwa siri. Binafsi nilizungumza suala la<br />
UDA mimi suala hili linaniuma. Tumelizungumza na tumefuatilia na tumeona kwamba mpan<strong>go</strong> wa<br />
uuzaji wa Shirika la UDA haukuwa sahihi umefanyika uhuni na ninasema kwa sababu vithibitisho<br />
tunavyo wao katika kuuza hisa zao kama Jiji limeshindwa tunasema mali zile zirudishwe kwa<br />
Serikali. Naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha kupitia Msajili wa Hazina chukua asilimia hizi, bila<br />
hivyo mpan<strong>go</strong> wa kuliuza shirika hili, leo tuna mradi wa mabasi ya kasi, mabasi yale yatasimama<br />
wapi, yatawekwa wapi na wao halafu bahati mbaya badala ya kuzungumza mambo mazuri<br />
matokeo yake yale tunayosema hapa tunaambiwa wengine wale wanaochangia, sijui<br />
wanachangia kutoka Makalioni, wengine sijui wanachanga kwa sababu wana Wahindi sijui<br />
wanataka kuwapata.<br />
Hakuna cha Wahindi, hakuna cha nani. Tunachosema Shirika la UDA ni mali ya<br />
Watanzania ni mali ya wananchi ambao hawana magari ya kuwapeleka watoto wao shuleni.<br />
(Makofi)<br />
Angalieni tujiulize sisi, mimi, Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri na wao wenye Bodi<br />
wao watoto wao wanapanda mabasi wanatumia UDA wanapanda daladala Watoto wao<br />
wanawapeleka kwa magari na hawajui uchungu wa mtoto kumwamsha saa 11.00 alfajiri aende<br />
aka<strong>go</strong>mbee pale basi daladala inachukua watoto wawili, wengine wanabaki pale na kuweza<br />
kudhalilika wakati mwingine na shule hawafiki wanachelewa wakifika shule wanateswa.<br />
Tunaomba kama Jiji limeshindwa naomba mradi huu waangalieni uchukueni Serikali lakini<br />
mpan<strong>go</strong> wa kuliuza hatukubaliani nao. Nasema naomba wana Dar es Salaam nawaomba<br />
Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> wa Dar es Salaam wote wanafunzi wote wa Dar es Salaam wanaotumia<br />
mabasi haya UDA ndio shirika pekee litakaloweza kuwasaidia. Madaladala kila siku tunashuhudia<br />
tukidhalilishwa.<br />
18