28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

hasa kwa wanafunzi wapya. Vibaka hupata mavuno katika kipindi hicho kwani vijana wakijipanga<br />

tangu asubuhi bila kupata kifungua kinywa, inapofika mchana huwa wana njaa na hata kuanza<br />

kusinzia kwa sababu huwa wamechoka, pia kutokana na kuwa huwa wameamka mapema.<br />

Mheshimiwa Spika, lakini pia ikizingatiwa kuwa mabenki ni machache sana nchini hasa<br />

kwenye maeneo ya vijijini, vijana au wazazi wote hulazimika kusafiri mwendo mrefu kwenda<br />

Makao ya Wilaya kulipa karo. Mathalani Wilaya ya Magu inazo sekondari za Kata 39, hebu fikiria<br />

wanafunzi/wazazi wanaorundikana kwenye tawi moja la NMB kulipia karo katika kipindi cha siku<br />

chache. Hakuna namna nyingine ya kulipia karo hizo Gharama ya usafiri na chakula hata malazi<br />

kwa mtu anayekwenda kulipa karo inaongeza gharama ya shule kwa wazazi maskini lakini pia ni<br />

adha kubwa. Naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha atupatie ufafanuzi wa namna ya kuondoa<br />

kero hii.<br />

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Busega Benki ya NMB, ilishatuma wataalam wake kuja<br />

kufanya utafiti wa kuanzisha tawi la benki katika Mji wa Lamadi. Sasa ni mwaka mzima tangu<br />

watu hao waje na hatuoni hatua zozote zimechukuliwa. Mji wa Lamadi wenye wakazi karibu<br />

40,000 una biashara nyingi zikiwemo za mazao, utalii, maduka, mashine za pamba, mahoteli na<br />

kadhalika.<br />

Naomba kufahamu ni lini benki hiyo itaanza kufanya kazi kwani mzunguko wa fedha<br />

uliopo ni mkubwa. Kuendesha biashara kwa fedha ya mfukoni ni hatari na inavutia ujambazi.<br />

Tunaomba tawi la benki Lamadi haraka.<br />

MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuwapongeza Waziri,<br />

Naibu Waziri na wataalam wa Wizara kwa hotuba iliyowasilishwa. Naipongeza Wizara kwa juhudi<br />

za kuimarisha ukaguzi wa ndani, matumizi ya teknolojia za kisasa katika shughuli mbalimbali za<br />

Wizara na kadhalika. Hata hivyo, bado Wizara hii inahitajika kufanya maboresho/mabadiliko katika<br />

mambo mengi kama ilivyopendekezwa na Kamati ya Fedha na Uchumi na Kambi Rasmi ya<br />

Upinzani. Kwa maoni yangu, mambo ambayo yanahitaji kufanyika haraka ni haya yafuatayo:-<br />

Kwanza tathmini makini ya utekelezaji wa sera ya ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma, pili,<br />

kuimarisha usimamizi wa Mashirika ya Umma kwa kuanzisha Ofisi ya Mashirika ya Umma<br />

(itakayosimamia Mashirika yenye hisa zaidi ya 51% za Serikali), na Kampuni/Shirikia Hodhi la Taifa<br />

(baada ya kurekebisha CHC) lenye kusimamia Mashirika yenye hisa za Serikali chini ya 51%, tatu,<br />

pendekezo la windfall tax kwenye dhahabu ili Serikali ipate mrahaba stahiki na nne, Mifuko ya<br />

Hifadhi ya Jamii ipunguzwe ili ibaki miwili tu (unaohudumia watumishi katika Serikali/Mashirika ya<br />

umma na ule unaohudumia watumishi katika Mashirika binafsi) na iwe chini ya usimamizi wa<br />

Wizara ya Kazi na Ajira.<br />

Kadhalika, watumishi waliostaafu zamani wakati mishahara (na mafao) ilipokuwa mido<strong>go</strong><br />

waongezewe mafao yao kulingana na upandaji gharama za maisha. Aidha, watumishi wa Vyuo<br />

Vikuu vya Serikali (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo na<br />

kadhalika) waliokuwa kwenye utaratibu wa pensheni wa Senior Staff Superrannuation Scheme<br />

(SSSS), waliostaafu kabla ya Machi, 2011 wapangiwe utaratibu wa kulipwa pensheni ya kila mwezi<br />

kama watumishi wastaafu wenzao wanavyolipwa. Hawa sio wengi, hivyo Serikali isiwe na<br />

kigugumizi kuhusu hili na tano kwa kuwa Wizara hii ni muhimu kwa uchumi na maendeleo ya Taifa,<br />

watumishi wa Wizara wawe makini, waadilifu na wazalendo ili usimamizi wa fedha za umma uwe<br />

imara.<br />

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iziongezee mtaji Benki za Posta na Benki ya Twiga.<br />

Benki ya Posta ni Benki ya Serikali 100%. Ina mtandao mzuri nchi nzima na ni benki inayoweza<br />

kujitandaza katika Wilaya zote kwa urahisi. Hata hivyo, haiwezi kufanya hivyo sasa hivi kwa kuwa<br />

haina mtaji wa kutosha ili iweze kufanya biashara ya kukopesha kwa mapana na kuwekeza katika<br />

maeneo mbalimbali. Benki ya Twiga (Twiga Bancorp Limited) pia inamilikiwa na Serikali 100%, lakini<br />

nayo haiwezi kupanua shughuli zake za kibiashara kwa kuwa na mtaji mdo<strong>go</strong>.<br />

Mheshimiwa Spika, mimi ninashauri kuwa badala ya kuanzisha utitiri wa mabenki ambayo<br />

yatagharimu kiasi kingi zaidi cha fedha (mathalani Benki ya Vijana na Benki ya Wakulima<br />

38

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!