28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

nafasi walizozitumikia katika ofisi mbalimbali nchini. Iwahusu wale ambao hawapo katika mfumo<br />

huo rasmi.<br />

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, Tanzania Investment Bank (TIB) na Tanzania<br />

Agricultural Development Bank (TADB) wakati tunajadili mpan<strong>go</strong> wa maendeleo ya miaka mitano<br />

ilikubalika kuwa kuanzia Bajeti 2011/2012 Serikali itapeleka shilingi bilioni 100 (TIB) na shilingi bilioni<br />

100 (TADB) kila mwaka wa fedha kwa mfululizo wa miaka mitano.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa nini katika hotuba ya Waziri wa Fedha hakuna mahali popote<br />

alipoonyesha ahadi hii na hakuna jedwali la mabadiliko linaloonyesha ongezeko la hizo bilioni<br />

200<br />

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Benki ya Posta (TPB) ina mtaji wa shilingi bilioni 10.5 na<br />

kwamba inapungukiwa shilingi bilioni 4.5 kufikia mtaji wa shilingi bilioni 15 inayotakiwa na sheria ya<br />

uanzishwaji wa benki hii itaiwezesha Serikali kuwa na benki imara ya biashara na kwamba<br />

itashindana na akina NMB, Barclays, Stanbic na CRDB. Faida yake ni kuwa faida inayopatikana<br />

inabaki hapa nchini (mfano mwaka jana walipata faida karibia shilingi bilioni moja).<br />

Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isiongeze mtaji wa shilingi bilioni 10, ili tuifanye benki<br />

kushindana na kuimarika<br />

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kuna pen<strong>go</strong> kubwa baina ya riba za kuweka kwenye benki<br />

na riba tunazotozwa tunapoenda kukopa, ukiweka unalipiwa riba ya 3% lakini wewe ukikopa ni<br />

18% au zaidi, pia kuna arrangement fees ambayo 1.5% au zaidi. Kufanya riba kufikia 20%, riba hii ni<br />

kubwa sana, badala ya kumwezesha mwananchi kiuchumi inamfilisi.<br />

Mheshimiwa Spika, je, Serikali kupitia BOT, ina mpan<strong>go</strong> gani kuhakikisha kuwa asilimia ya<br />

kuweka inafikia 5% na ile ya kukopa inafiki 12%<br />

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ni 12.4% ya Watanzania watu wazima wanapata huduma<br />

ya benki ambapo ni watu milioni mbili kati ya watu milioni 20. Je, Serikali kupitia BOT, itaanzisha lini<br />

Benki Jimboni Kisesa sambamba na kupanua mtandao wa huduma za fedha nchini<br />

Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali inatekeleza miradi mingapi Na imepokea fedha kiasi<br />

gani toka NEPAD<br />

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kutamka kuwa<br />

naunga mkono hoja iliyotolewa mbele yetu na Wizara ya Fedha.<br />

Mheshimiwa Spika, katika miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia ongezeko kubwa la kasi la<br />

SACCOS hapa nchini. Hata hivyo wakati hali ikiwa hivyo inasikitisha kuona sekta hii ikikabiliwa na<br />

usimamizi wa SACCOS, ndio maana sio ajabu sasa kuona SACCOS zikiachwa kuendelea kufanya<br />

shughuli za kupokea akiba za wanachama na kutoa mikopo wakati SACCOS hizi hazijafanyiwa<br />

ukaguzi wa hesabu zake kwa miaka miwili mfululizo kinyume kabisa na taratibu za fedha.<br />

Swali la kujiuliza hapa ni je, katika hali hii tunajiridhisha vipi na usalama wa akiba za<br />

mwanachama Upo ushahidi kuwa wakati wa tatizo la DECI mion<strong>go</strong>ni mwa wahanga wakubwa<br />

wa janga lile ni SACCOS ambazo zilichukua akiba za wanachama na kwenda kupanda mbegu<br />

DECI. Katika hali hii Serikali haiwezi kukwepa lawama kwa kushindwa kusimamia kikamilifu sekta ya<br />

fedha.<br />

Mheshimiwa Spika, udhaifu huu unajidhihirisha vilevile kuwa pamoja na sheria ya kutaka<br />

SACCOS zenye mtaji wa shilingi milioni 800 na kusimamiwa moja kwa moja na Benki Kuu, bado<br />

SACCOS nyingi ambazo zimevuka kiwan<strong>go</strong> hicho hazisimamiwi na Benki Kuu.<br />

Mheshimiwa Spika, VICOBA ni mfumo ambao unazidi kupata umaarufu mkubwa hapa<br />

nchini na wananchi wengi wa vijijini wanautumia mfumo huu kupata huduma za kifedha.<br />

Changamoto iliyopo ni kwamba usalama wa fedha za wananchi ambao wanaweka hisa zao<br />

30

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!