Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mheshimiwa Spika, Watanzania wamechoka na taratibu zozote zinazoashiria kuhujumu<br />
mali za umma.<br />
Wizara ya Fedha inasimamia uuzaji wa Mashirika ya Umma (Hazina ndio Registrar)<br />
ambaye ana hisa katika mashirika hayo. Ninashauri Serikali Mashirika haya yaendelee kuuzwa kwa<br />
uwazi na uadilifu zaidi. Hisia za udanganyifu kama zilizotokea kwa UDA ni vema ziachwe ili<br />
kuisafisha Serikali katika tuhuma zisizokuwa za msingi. Serikali ikumbuke inahitaji kurudi madarakani<br />
kutawala.<br />
Mheshimiwa Spika, kero ya wastaafu wa Afrika Mashariki inaleta sura mbaya kwa Serikali<br />
ya Chama cha Mapinduzi. Nashauri Serikali ifuatilie kesi yao Mahakamani, ili imalizike na Serikali<br />
itoe tamko kila mwananchi aelewe kuwa wastaafu hao hawana cha kudai. Vinginevyo Serikali<br />
iwalipe kifuta machozi ili kuondoa manung’uniko mengi. Hata hivyo wengi wao wazee sana na<br />
wana umri mfupi wa kuishi.<br />
Mheshimiwa Spika, ziko fedha zinalipwa kama OC katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya. Fedha<br />
hizi wakati mwingine zinapangwa kiasi fulani mfano shilingi milioni 12, lakini Hazina inapeleka<br />
pungufu ya Bajeti iliyopangwa. Hali inaleta matatizo mengi katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya<br />
kiutendaji. Ikumbukwe kuwa Mkuu wa Wilaya kazi yake sio kukaa ofisini bali kwenda vijijini kutatua<br />
kero za wananchi. Kama Mkuu wa Wilaya atakuwa hana fedha ya mafuta kwa sababu ya ufinyu<br />
wa Bajeti itakuwa vigumu kutenda kazi ipasavyo.<br />
Mheshimiwa Spika, ipo capital flight kubwa inayofanyika kwa Bureau de Change<br />
kutokutoa risiti kwa wanaobadilisha fedha za kigeni. Upo pia mchezo wa Bureau hizi kupandisha<br />
bei ya kununua dola ya Marekani kuliko Bureau nyingine, kwa nia ya kukusanya dola nyingi mara<br />
moja na baada ya muda Bureau inafunga au kuuza duka kwa mfanyabiashara mwingine.<br />
Nashauri Serikali ifuatilie kwa karibu zaidi.<br />
Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali ipeleke fedha za miradi katika Halmashauri za Wilaya<br />
kwa wakati. Ucheleweshaji unafanya miradi isikamilike na kuleta usumbufu kwa wananchi.<br />
Inawezekana kabisa Serikali ikapeleka fedha kutegemeana na hali ya hewa. Mfano yapo<br />
maeneo yana mvua nyingi yatahitaji fedha za kuchimba mabwawa zipelekwe mapema kabla ya<br />
kipindi cha mvua.<br />
Mheshimiwa Spika, naiomba na kuishauri Serikali iweke mkazo na ukali kwa benki zetu ili<br />
ziwe na sera ya mikopo ya nyumba mikopo kupitia mishahara ya wafanyakazi ni kido<strong>go</strong> sana,<br />
wabuni mbinu nyingine za kuweza kurudisha fedha za nyumba ili Watanzania waweze kujenga<br />
nyumba nafuu. Katika Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro eneo la Njia Panda ni eneo<br />
ambalo limekuwa haraka kwa makazi na kiuchumi. Nashauri Serikali iishauri NMB iweke tawi ili<br />
kunusuru fedha za wananchi na Serikali, kuna mizani ambao unafanya kazi saa 24.<br />
Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali idhibiti other financial institutions ambazo zinatoa<br />
mikopo kwa riba kubwa sana (above 22%), mfano Blue Financial na kadhalika.<br />
Mheshimiwa Spika, wapo watu ambao wanakopesha walimu na wafanyakazi wengine<br />
bila kujiandikisha na payback ni 50%. Watu hawa wadai collateral kadi za ATM, vitambulisho vya<br />
Benki na kadhalika. Nashauri Serikali ifuatilie mfano ni Nzega Mjini wapo watu wa aina hii na<br />
wachukuliwe hatua za kisheria.<br />
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />
MHE. ZAKIA H. MEGHJI: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na<br />
timu yake kwa maandalizi ya Bajeti hii na kusimamia Bajeti iliyopita pamoja na matatizo mengi ya<br />
kiuchumi Kitaifa na Kimataifa.<br />
Mheshimiwa Spika, suala la kuhakikisha fedha zilizoidhinishwa kwa ajili ya nishati ili kuwa na<br />
uhakika wa umeme kupatikana kabla ya Januari, 2012 ihakikishwe kuwa fedha hizi zinapatikana.<br />
Jambo hili ni muhimu kwa sababu ni ahadi ya Serikali Bungeni na imeathiri sana ukusanyaji wa<br />
32