28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, Watanzania wamechoka na taratibu zozote zinazoashiria kuhujumu<br />

mali za umma.<br />

Wizara ya Fedha inasimamia uuzaji wa Mashirika ya Umma (Hazina ndio Registrar)<br />

ambaye ana hisa katika mashirika hayo. Ninashauri Serikali Mashirika haya yaendelee kuuzwa kwa<br />

uwazi na uadilifu zaidi. Hisia za udanganyifu kama zilizotokea kwa UDA ni vema ziachwe ili<br />

kuisafisha Serikali katika tuhuma zisizokuwa za msingi. Serikali ikumbuke inahitaji kurudi madarakani<br />

kutawala.<br />

Mheshimiwa Spika, kero ya wastaafu wa Afrika Mashariki inaleta sura mbaya kwa Serikali<br />

ya Chama cha Mapinduzi. Nashauri Serikali ifuatilie kesi yao Mahakamani, ili imalizike na Serikali<br />

itoe tamko kila mwananchi aelewe kuwa wastaafu hao hawana cha kudai. Vinginevyo Serikali<br />

iwalipe kifuta machozi ili kuondoa manung’uniko mengi. Hata hivyo wengi wao wazee sana na<br />

wana umri mfupi wa kuishi.<br />

Mheshimiwa Spika, ziko fedha zinalipwa kama OC katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya. Fedha<br />

hizi wakati mwingine zinapangwa kiasi fulani mfano shilingi milioni 12, lakini Hazina inapeleka<br />

pungufu ya Bajeti iliyopangwa. Hali inaleta matatizo mengi katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya<br />

kiutendaji. Ikumbukwe kuwa Mkuu wa Wilaya kazi yake sio kukaa ofisini bali kwenda vijijini kutatua<br />

kero za wananchi. Kama Mkuu wa Wilaya atakuwa hana fedha ya mafuta kwa sababu ya ufinyu<br />

wa Bajeti itakuwa vigumu kutenda kazi ipasavyo.<br />

Mheshimiwa Spika, ipo capital flight kubwa inayofanyika kwa Bureau de Change<br />

kutokutoa risiti kwa wanaobadilisha fedha za kigeni. Upo pia mchezo wa Bureau hizi kupandisha<br />

bei ya kununua dola ya Marekani kuliko Bureau nyingine, kwa nia ya kukusanya dola nyingi mara<br />

moja na baada ya muda Bureau inafunga au kuuza duka kwa mfanyabiashara mwingine.<br />

Nashauri Serikali ifuatilie kwa karibu zaidi.<br />

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali ipeleke fedha za miradi katika Halmashauri za Wilaya<br />

kwa wakati. Ucheleweshaji unafanya miradi isikamilike na kuleta usumbufu kwa wananchi.<br />

Inawezekana kabisa Serikali ikapeleka fedha kutegemeana na hali ya hewa. Mfano yapo<br />

maeneo yana mvua nyingi yatahitaji fedha za kuchimba mabwawa zipelekwe mapema kabla ya<br />

kipindi cha mvua.<br />

Mheshimiwa Spika, naiomba na kuishauri Serikali iweke mkazo na ukali kwa benki zetu ili<br />

ziwe na sera ya mikopo ya nyumba mikopo kupitia mishahara ya wafanyakazi ni kido<strong>go</strong> sana,<br />

wabuni mbinu nyingine za kuweza kurudisha fedha za nyumba ili Watanzania waweze kujenga<br />

nyumba nafuu. Katika Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro eneo la Njia Panda ni eneo<br />

ambalo limekuwa haraka kwa makazi na kiuchumi. Nashauri Serikali iishauri NMB iweke tawi ili<br />

kunusuru fedha za wananchi na Serikali, kuna mizani ambao unafanya kazi saa 24.<br />

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali idhibiti other financial institutions ambazo zinatoa<br />

mikopo kwa riba kubwa sana (above 22%), mfano Blue Financial na kadhalika.<br />

Mheshimiwa Spika, wapo watu ambao wanakopesha walimu na wafanyakazi wengine<br />

bila kujiandikisha na payback ni 50%. Watu hawa wadai collateral kadi za ATM, vitambulisho vya<br />

Benki na kadhalika. Nashauri Serikali ifuatilie mfano ni Nzega Mjini wapo watu wa aina hii na<br />

wachukuliwe hatua za kisheria.<br />

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />

MHE. ZAKIA H. MEGHJI: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na<br />

timu yake kwa maandalizi ya Bajeti hii na kusimamia Bajeti iliyopita pamoja na matatizo mengi ya<br />

kiuchumi Kitaifa na Kimataifa.<br />

Mheshimiwa Spika, suala la kuhakikisha fedha zilizoidhinishwa kwa ajili ya nishati ili kuwa na<br />

uhakika wa umeme kupatikana kabla ya Januari, 2012 ihakikishwe kuwa fedha hizi zinapatikana.<br />

Jambo hili ni muhimu kwa sababu ni ahadi ya Serikali Bungeni na imeathiri sana ukusanyaji wa<br />

32

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!