28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Spika, baada ya hayo nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naunga mkono hoja.<br />

(Makofi)<br />

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Ahsante sana Mheshimiwa Spika, kwa nafasi hii ndo<strong>go</strong><br />

ulionipa lakini ni muhimu sana. Nimesimama kwa niaba ya Wa<strong>bunge</strong> wa Mkoa wa Mkoa wa<br />

Dodoma na wakulima wote wa zabibu Mkoani Dodoma na kwingine kokote ambako wanalima<br />

zabibu.<br />

Mheshimiwa Spika, naamini wewe mwenyewe ni mkulima wa zabibu na Mheshimiwa<br />

Waziri Mkuu pia mtoto wa mkulima naye anajifunza kulima zabibu. Imani kubwa ni kwamba hili<br />

nitakalolisema pia na nyie mna maslahi nalo. Zao la zabibu katika mkoa wetu wa Dodoma na sisi<br />

ndiyo almasi yetu na ndiyo dhahabu yetu na ni zao ambalo kwa hakika ukilinganisha na duniani<br />

nyingine wanakolima zabibu, zabibu ya Dodoma inavunwa mara mbili kwa mwaka. Hakuna nchi<br />

yoyote duniani ambayo wanaweza kuvuna zabibu mara mbili kwa mwaka. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, zao hili lilipata mwanguko miaka ya 1990 na likafa kabisa baada ya<br />

kiwanda kilichokuwa cha DOWICO kufa na hivyo wakulima wakakosa mahala pa soko la kuuza<br />

zabibu zao. Lakini kuanzia miaka ya hivi karibuni au tuseme mwaka 2004 zao hili limepata<br />

uchangamfu mpya baada ya kuanzishwa kwa viwanda, kikiwepo kiwanda cha SITAWICO<br />

ambapo kwa kushirikiana na Tanzania Distilleries Limited wamekuwa wanunuaji wakubwa wa zao<br />

hili la zabibu pamoja na viwanda vingine vido<strong>go</strong> vido<strong>go</strong> vilivyoko hapa Mkoani Dodoma.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, zao hili sasa limepata sura mpya na sasa kuanzia mwaka 2004<br />

walikuwa wanaweza kununua lita 62,520 ya zabibu. Lakini mpaka mwaka 2010/2011 wameweza<br />

kununua lita 816,000.<br />

Maendeleo haya ni makubwa na yamekuwa makubwa kwa sababu Serikali ilikuwa<br />

imefuta ushuru Excise Duty ambayo ilipelekea sasa kuwa zabibu ikitengenezwa kwa maana ya<br />

viwanda vyetu hivi inakuwa katika ushindani wa soko na zile wine zinazotoka nje ya nchi yetu.<br />

Sasa baada ya kuwa ushuru kuwa upo hivyo lakini halisi halisi ikoje.<br />

Mheshimiwa Spika, bei ya zabibu duniani ni shilingi 250 kwa kilo kwenye soko la dunia.<br />

Lakini kwa hapa Dodoma hawa hawa processors hawa wanao-produce hizi wine wananunua<br />

kwa mkulima kwa shilingi 800 hadi 1,000 kwa hapa Tanzania.<br />

Ukiangalia tofauti ya bei hii ndiyo inayopelekea huu msamaha uwe na umuhimu mkubwa<br />

sana, wakati sasa tunapozungumzia kilimo kwanza na wakati uzalishaji katika mashamba duniani<br />

wenzetu wanazalisha kwa heka moja kiasi cha tani 10.5 kwa heka moja.<br />

Lakini sisi Dodoma kwa heka moja tunazalisha tani 2.5. Sasa ili uweze kumvuta huyu<br />

mkulima ni lazima uweke msamaha fulani ili huyu mnunuaji aki-process aweze kupata faida.<br />

Vinginevyo zabibu yetu ya Dodoma itakufa na kwamba huyu anayetengeneza wine ya Dodoma<br />

hataweza kushindana na anaye-import kutoka nje. Tunasema tuko kwenye Kilimo Kwanza.<br />

(Makofi)<br />

Sasa kwa kutokufanya hivyo na maamuzi haya yamefanyika na Serikali ya kufuta hiyo<br />

wave iliyokuwepo ya ushuru huu sijui kama walitafakari umuhimu na ulazima wa Sera ya sasa ya<br />

Serikali ya Chama cha Mapinduzi juu ya Kilimo Kwanza. Kwa sababu wangekuwa wanaliona hili<br />

wasingetakiwa kusubiri wapewe taarifa na wenye viwanda kwa sababu wanaiona hiyo hali halisi<br />

ya soko ilivyo. Mimi nafikiri hapa hapakuwa na dual diligence kwamba hawakuweza kufanya<br />

utafiti wa kutosha juu ya zao hili.<br />

Sisi Wa<strong>bunge</strong> wa Mkoa wa Dodoma kwa niaba ya wenzangu wote niseme kabisa<br />

hatukufurahishwa na jambo hili. Tunaiomba sana Serikali iangalie upya jambo hili na kwa kuwa<br />

mwezi Januari kutafanyika Budget Review basi wakati wa Budge Review hii waangalie namna ya<br />

kurudisha ile waive ili ule ushuru uondolewe zabibu yetu iweze kushindana, wine yetu iweze<br />

kushindana na wine ya nje ya nchi yetu. (Makofi)<br />

28

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!