28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

kukimbilia kwenye bandari za Kenya. Hii inanyima mapato Serikali. Urasimu huu wa kutoa mizi<strong>go</strong> ni<br />

hata pale bidhaa inayoingia haina ushuru.<br />

Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha mfumo wa malipo ya TISS kwa malipo ya zaidi ya<br />

Shilingi milioni kumi. Mtindo huo wa malipo unatumiwa vibaya na mabenki mengine na<br />

kuchelewesha malipo wakati mwingine zaidi ya siku saba bila mtu kupata malipo. Hii siyo tu inaleta<br />

usumbufu kwa wateja, lakini pia kuchelewesha mzunguko wa fedha ambao kwa upande<br />

mwingine unadumaza uchumi wa Taifa.<br />

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni kumekuja huduma ya kifedha kutumia simu za mkononi M-<br />

PESA, TIGO-PESA. Naomba kujua ni jinsi gani Serikali inafaidika katika huduma hii ya kutumia simu<br />

hizi za mkononi.<br />

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na wizi katika mabenki yetu kupitia hii huduma ya kupeleka<br />

pesa kutumia simu za mkononi. Lakini pia kumekuwa na ripoti nyingi za wizi wa fedha kutumia ATM<br />

lakini pia kwenye mabenki na hata TRA. Hatua za haraka kudhibiti hali hii zichukuliwe kinyume cha<br />

hapo wananchi watapoteza imani na taasisi zao za kibenki.<br />

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba nimpongeze tena Mheshimiwa Waziri<br />

na naunga mkono hoja.<br />

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha (HAZINA) kuna<br />

ucheleweshwaji wa fedha kuingia Wizarani hasa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambapo<br />

mpaka sasa malimbikizo ya madeni ya mishahara ni makubwa mno, jambo ambalo linaibebesha<br />

mzi<strong>go</strong> Serikali.<br />

Mheshimiwa Spika, napendekeza kule HAZINA kuwepo na dawati la Maafisa wawili kwa<br />

kila Wizara hasa Wizara hii yenye changamoto kubwa nchini yaani Wizara ya Elimu na TAMISEMI,<br />

Afya, Mambo ya Ndani na Kilimo. Jambo hili litapunguza mrundikano wa madeni ya Walimu,<br />

Wakufunzi, Wakaguzi, Madaktari na Maafisa Kilimo na kuleta ufanisi katika utendaji.<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha kupitia Mabenki ya CRDB, nia ilikuwa Benki hii<br />

ihudumie wanachi vijijini hasa wakulima, wenye Vyama vya Ushirika, lakini Benki hii leo haihudumii<br />

jamii lengwa bali inahudumia wananchi mijini. Je, wakulima wenye mashamba makubwa na<br />

hawana nyumba bora wanafaidikaje na CRDB maana hata maana yake ni Commercial Rural<br />

Development Bank.<br />

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nashukuru kupata nafasi<br />

kuchangia katika bajeti ya Wizara hii. Aidha, napenda kuchukua fursa hii kuipongeza Wizara kwa<br />

utendaji na jitihada kubwa inazozifanya katika usimamizi wa fedha na kuinua uchumi kwa Taifa<br />

letu.<br />

Mheshimiwa Spika, katika nchi yetu tumekuwa tukitaarifiwa na Taasisi za Fedha kwamba<br />

fedha yetu inazidi kushuka thamani.<br />

Mheshimiwa Spika, kiwan<strong>go</strong> kinachochangiwa kwenye pato la Taifa kutokana na fedha<br />

za ndani ni kido<strong>go</strong> mno. Wizara ijitahidi kuweka mikakati na mipan<strong>go</strong> ya kuongeza kiwan<strong>go</strong> cha<br />

fedha kinachoweza kutuingizia mapato makubwa.<br />

Mheshimiwa Spika, kukopa kwa ajili ya miradi muhimu itakayochochea maendeleo ni<br />

jambo jema. Hata hivyo, ni muhimu tukaainisha mahitaji yetu na kuandaa mpan<strong>go</strong> mkakati<br />

utakaoainisha vyanzo mbalimbali ambapo tunaweza kupata mikopo na masharti na kujiwekea<br />

sera itakayobainisha namna ya kukopa kutoka nje na katika Benki zetu za ndani.<br />

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii ni<br />

chombo muhimu sana kwa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini. Sekta hii inakabiliwa na changamoto<br />

48

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!