28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

imekamilika na tumelazimisha kuhamia juu na ukumbi unahitaji takriban bilioni mbili na milioni mia<br />

tano. Niombe tusaidiwe fedha hizo ili sasa mradi huu ambao ni muhimu kwa Wilaya ya pembezoni<br />

ya Kilindi tukamilishe.<br />

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kilindi haina Ofisi ya TRA. Wananchi wanalazimika kwenda<br />

Handeni kilomita 102 toka Songe, Makao Makuu. Hii inaleta ugumu katika ukusanyaji na ulipaji<br />

kodi, ila pia ni mwanya wa rushwa, kwani watumiaji wanahitajika kwenda Handeni, suala ambalo<br />

ni gharama na gumu. Kama mtu anakamatwa na traffic, pikipiki ime-expire leseni, analipa faini<br />

kisha analipia akakatiwe leseni Handeni. Inabidi asitumie pikipiki hata kama ni wiki kusubiri leseni,<br />

ilhali unakuta yeye ana bodaboda. Hivyo, akiendesha anakamatwa tena na kutoa faini. Je,<br />

anakamatwa mara ngapi mpaka leseni ije Kwa vile huduma inapanuka kila siku naomba<br />

tupatiwe ofisi ya TRA, tupo tayari kutoa jen<strong>go</strong> kwa kazi hiyo.<br />

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kuipongeza Tume ya Pamoja ya Fedha, kwa kazi<br />

nzuri wanayofanya kwa mustakabali wa Muungano wetu, naomba wapewe msukumo na<br />

uwezeshaji zaidi ili jukumu lao liwe rahisi zaidi.<br />

Mheshimiwa Spika, mwisho, TIB (Dirisha la Kilimo) siyo la wakulima wado<strong>go</strong> wado<strong>go</strong>, hii si<br />

kweli kabisa. Dirisha hili limekaa kibiashara zaidi. Kama kweli imedhamiriwa kwa wakulima<br />

wado<strong>go</strong>wado<strong>go</strong>, basi hatua za makusudi zichukuliwe, iweze kufahamika ni wakulima au vikundi<br />

vingapi hadi leo vimepata vikwazo, changamoto na matatizo ili tujue mapungufu na kutoa ushauri<br />

tuendaje.<br />

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania<br />

aliamua fedha zinazolipwa na wadau wa EPA ziende kwenye shughuli za kilimo TIB. Napenda<br />

kufahamu fedha hizo zinaporejeshwa zinakwenda moja kwa moja TIB au zinakwenda kwanza BOT.<br />

Mheshimiwa Spika, je, Wizara kama mdau mkubwa wa wizi wa Fedha za EPA, hivi karibuni<br />

kuna kesi ambazo zimemalizika na Mahakama ya Kisutu imetoa uamuzi na moja ya hukumu mbali<br />

na watuhumiwa kufungwa, ni pamoja na kufilisiwa mali zao, je, Wizara husika kama mdau,<br />

imejipanga vipi kimkakati kuhakikisha hakutokuwa na udanganyifu wa mali kwa watuhumiwa ili<br />

fedha hizo za umma ziweze kufidiwa kiuhalali.<br />

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa ni kiasi gani ambacho kimerudishwa kwa wale wote<br />

walioamua kurudisha fedha za EPA.<br />

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.<br />

MHE. REGIA E. MTEMA: Mheshimiwa Spika, kuhusu TRA. Kwanza niipongeze TRA kwa<br />

kufanya kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato hapa nchini. Lakini pamoja na ukusanyaji huu mzuri<br />

bado TRA haijapanua wi<strong>go</strong> katika ukusanyaji huu wa mapato. Napendekeza kuwa Wizara<br />

iangalie uwezekano wa kupanua wi<strong>go</strong> wa watu kutoa kodi. Misamaha ya kodi pia ipunguzwe.<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Kwanza, nawapongeza watendaji<br />

wote wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutafuta wanachama na<br />

kutoa huduma bora kwa wafanyakazi hapa nchini pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Mifuko hii<br />

lakini bado kuna changamoto mbalimbali.<br />

Mheshimiwa Spika, PSPF na PPF inakabiliwa na changamoto za kutokutoa mafao kwa<br />

wakati. Napendekeza kuwa Serikali ijitahidi kuboresha utoaji wa huduma kwa wastaafu kwa<br />

wakati. Vilevile kwa kuwa Mifuko hii ina fedha nzuri na inawekeza kibiashara basi napendekeza<br />

kuwa Mifuko hii iwekeze katika kutoa huduma nyingine kama vile umeme na kadhalika.<br />

Mheshimiwa Spika, napendekeza kwa kuwa nchi yetu ni maskini, hivyo, tupunguze<br />

kukopa. Hata kama duniani kote wanakopa lakini si lazima wakati wote tukope. Tupunguze<br />

utegemezi.<br />

40

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!