28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

MHE. GOSBERT B. BLANDES: Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri<br />

wa Fedha, Naibu wake, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri<br />

wanayoifanya na kwa kuleta hotuba nzuri hapa Bungeni. Pamoja na pongezi hizi ninayo heshima<br />

kubwa kutoa machache na kuishauri Wizara hii. Nami nitafanya hivyo kama ifuatavyo:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwanza, matatizo ya Cash Budget. Utaratibu wa Cash budget kwa<br />

mtazamo wangu umekwamisha miradi mingi ya maendeleo kutekelezeka kwa wakati.<br />

Napenda kutoa ushauri kuwa Serikali iachane na utaratibu huu wa Cash budget badala<br />

yake Serikali itoe Warrant of fund na iwepo ceiling kila robo ya mwaka badala ya kusubiri<br />

kukusanya na ndiyo ipeleke fedha za maendeleo. Fedha haziendi kwa wakati muafaka, matokeo<br />

yake miradi inapanda (variation). Serikali ikope fedha kutoka kwa wananchi kwa njia ya Treasurer<br />

bonds ili ijazilizie pale penye upungufu na kujenga miradi kwa wakati na pale itakapokusanya basi<br />

ilipe hiyo mikopo. Hizi Treasurer bills na Treasurer bonds kazi yake iwe ni kuziba pen<strong>go</strong> na<br />

kuhakikisha miradi inamalizika au inatekelezeka kwa wakati unaofaa.<br />

Mheshimiwa Spika, pili, kupanua wi<strong>go</strong> wa kukusanya mapato. Kwa sasa Serikali inajitahidi<br />

sana kukusanya kodi katika nyanja mbalimbali ikiwemo bia, sigara, wafanyakazi na kadhalika.<br />

Bado kuna wi<strong>go</strong> mkubwa wa kodi ambazo bado hazijakusanywa mfano, wapangishaji nyumba,<br />

mafundi ujenzi wa kawaida ambao hawajasajiliwa. Ni vizuri wajenzi wado<strong>go</strong> hawa watambuliwe<br />

na Bodi ya Wakandarasi CRB, wajengewe uwezo ili waweze kulipa.<br />

Mheshimiwa Spika, tatu, noti mpya toleo la mwisho. Noti mpya zilizotolewa hivi karibuni ni<br />

nzuri kwa muonekano hata ubora. Tatizo zinaghushiwa kirahisi ni kwa nini Pia noti hizi inaelekea<br />

zilitengenezwa katika size ya kuweka kwenye pochi ili zisichakae. Noti hizi zinaonekana kulengwa<br />

watumiaji wa nchi zilizoendelea ambapo karibu kila mtu anamiliki pochi. Ndiyo maana noti hizi<br />

zinapopelekwa katika mazingira ya vijijini kwa akinamama baada ya kuuza bidhaa zao, pamoja<br />

na kuwa nzuri na zenye mvuto na pengine zenye ubora lakini inaelekea zisipotunzwa kwenye<br />

pochi zinaharibika haraka sana. Serikali iliangalie suala hili.<br />

Mheshimiwa Spika, nne, hisa za Makampuni ya nchi za nje. Hadi sasa Tanzania au<br />

wananchi wa Tanzania hawaruhusiwi kununua hisa za makampuni ya nje ikiwamo na nchi za<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati nchi wanachama wa jumuiya hizi ikiwemo nchi za Uganda na<br />

Kenya wanaruhusiwa kununua hisa za makampuni katika soko la mitaji la Dar es Salaam. Tatizo hili<br />

la Watanzania kutoruhusiwa kununua hisa nje ni kutokana na sheria za nchi yetu kutoruhusu<br />

wananchi wetu kununua hisa za makampuni nje. Je, hii sheria kuzuia watu wakati nchi<br />

wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki nchi zao zinawaruhusu na hivyo wao kufaidika na<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati Tanzania tunabaki nyuma. Nashauri sheria zote zinazozuia<br />

Watanzania kununua hisa nje ya nchi ziletwe hapa Bungeni zibadilishwe haraka.<br />

Mheshimiwa Spika, tano, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Hapa nchini tunayo Mifuko<br />

mbalimbali ya Hifadhi ya Jamii ikiwemo NSSF, LAPF, PPF, GEF ambayo hupokea michan<strong>go</strong> kutoka<br />

kwa wanachama wake kwa ajili ya mafao yao ya uzeeni au kwa muda maalum. Mafao yao<br />

hutolewa pamoja na riba lakini riba hizi zinatofautiana sana na ziko chini ya inflation rate. Mfano,<br />

NSSF hutoa riba kati ya 2% - 2.5%, LAPF 5% - 7%. Utofauti huu unawaumiza hasa wale wanaojiunga<br />

na hifadhi zinazotoa riba ndo<strong>go</strong> mfano NSSF. Pia hata riba ya 5% - 7% ni ndo<strong>go</strong> kwani iko chini ya<br />

mfumuko wa bei (inflation).<br />

Mheshimiwa Spika, sita, ombi la Matawi ya Benki. Naomba Serikali izungumzie na benki<br />

mbalimbali ikiwemo CRDB, NMB na nyinginezo nyingi zipeleke huduma za mabenki (zifungue<br />

matawi) yake katika mji wa biashara wa Omurushaka, Wilayani Karagwe. Pia Matawi ya benki<br />

yanahitajika haraka katika Miji ya Nyaishozi, Nyakaiga na Rwambaizi katika Jimbo la Karagwe,<br />

Wilayani Karagwe, Kagera. Kupeleka matawi huko kutapunguza wizi wa kutumia ujambazi na<br />

kupeleka huduma karibu na wananchi.<br />

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />

44

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!