Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mheshimiwa Spika, kuna fedha ambayo huwa inarudishwa kutoka Halmashauri zetu<br />
ambazo zinatokana watumishi kuacha kazi, watumishi kustaafu na mtumishi kufa. Je, fedha hii<br />
inaingizwa kwenye Bajeti ipi Na inatumikaje<br />
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa watumishi wengi sana waliostaafu bado hawajapata haki<br />
zao au kucheleweshewa malipo yao je, Wizara imejipanga vipi kuondokana na tatizo hili<br />
Mheshimiwa Spika, fedha za wafadhili huchelewa kufika katika sekta husika ili kukamilisha<br />
miradi iliyopangwa na kusababisha miradi kutokamilika kwa muda uliopangwa. Je, Wizara<br />
inasemaje kuhusu hilo Je, upo mkakati wa kuhakikisha fedha ya wafadhili inawasilishwa kwa<br />
muda uliopangwa kwa mpan<strong>go</strong> kazi wa mradi husika<br />
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nategemea Wizara itafanya jitihada za kuhakikisha uchumi<br />
wa nchi yetu unakua na kuimarisha mikakati ya ukusanyaji wa mapato ambayo yatasababisha<br />
kukidhi matumizi ya nchi yetu.<br />
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.<br />
MHE. LETICIA M. NYERERE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia kuhusu suala la kushuka<br />
kwa fedha ya Tanzania.<br />
Mheshimiwa Spika, Serikali inatumia mikakati gani kufanya utafiti wa kina na hatimaye<br />
kubaini tatizo linalosababisha kushuka kwa thamani ya pesa yetu<br />
Mheshimiwa Spika, naomba kupata maelezo kutoka kwa Mheshimiwa Waziri ni sheria gani<br />
ya nchi inayoruhusu matumizi ya fedha za nje hasa dola za Kimarekani katika utoaji huduma na<br />
vilevile katika malipo ya kodi ya nyumba.<br />
Mheshimiwa Spika, je, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba kushindwa kudhibiti matumizi<br />
holela ya dola za Kimarekani ndiko kulikopelekea kushusha thamani ya pesa yetu<br />
Mheshimiwa Spika, namuomba Mheshimiwa Waziri atoe maelezo ni lini sasa shilingi ya<br />
Tanzania itawekewa kinga na Serikali ili transaction zote nchini zifanywe kwa kutumia legal<br />
currency ambayo ni shilingi<br />
Mheshimiwa Spika, ni jambo la kushangaza kuona Serikali inaruhusu matumizi ya pesa za<br />
nchi za nje.<br />
Mheshimiwa Spika, naomba Serikali isimamie fedha yetu kikamilifu, kwani jambo hili<br />
halifanyiki kwa wenzetu wa nchi zilizoendelea ili kulinda nguvu ya pesa zao yaani official currency<br />
ya nchi husika.<br />
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, Kiten<strong>go</strong> cha Ushuru cha TRA ni sawa na<br />
mpiga ramli wa kienyeji cha kushangaza mimi binafsi niliagiza gari langu moja na la pili la<br />
Mheshimiwa Mipata.<br />
Mheshimiwa Spika, magari mapya nilinunua toka Oman, Muscat cha ajabu kiten<strong>go</strong> cha<br />
TRA hawakuwa tayari kukubali risiti wala maelezo yangu hata baada ya kuwaeleza kuwa kama<br />
mimi nimedanganya hata senti moja nipo tayari kusalimisha hayo magari na kuwajulisha kuwa<br />
Muscat, Oman kuna Balozi wa Tanzania wamtume aende akaulize kwenye hiyo kampuni<br />
walikataa, pia niliwaeleza nipo tayari hata kutoa nauli kwa mfanyakazi yeyote wa TRA na kama<br />
akikuta nimedanganya nipo tayari hayo magari wataifishe maana ni mapya kabisa Model 2011<br />
na yapo Show Room yanauzwa kwa mtu yeyote. Cha ajabu makadirio ya kwanza eti walikisia gari<br />
langu eti shilingi bilioni moja na la Mheshimiwa Mipata shilingi milioni 500.<br />
Mheshimiwa Spika, je, hiyo gari gani Huo si upigaji wa ramli au kutafuta rushwa tu<br />
Mwisho wa yote hata hivyo baada ya kulalamika sana haikusaidia kitu wameniibia<br />
kimachomacho labda sikutoa rushwa, gari langu wamezidisha zaidi ya shilingi 12,000,000/= gari la<br />
Mheshimiwa Mipata wamezidisha shilingi 8,000,000/= hiyo ni halali wakati nimetoa ushahidi wote<br />
36